Monday, November 14, 2005

TEKNOHAMA Kazini; Sengerema Hadi Tunis


Felician Ncheye ni mkazi wa Sengerema, mkoani Mwanza. Kazi yake ni kutoa huduma ya mawasiliano kwa njia ya mtandao wa kompyuta kwa wakazi na wapita njia wa Sengerema kwa kutumia kituo chake, Sengerema Telecentre. Katika picha hii, yupo Tunis, kwenye Banda la Tanzania, katika mkutano wa dunia kuhusu Jamii ya Habari na Mawasiliano (WSIS), alikokwenda kuwaonyesha wananchi kutoka sehemu mbalimbali za dunia kwamba naye wamo katika mtandao. (Picha na Ansbert Ngurumo 14.11.2005)

Kazi na Tabasamu


Anaitwa Amissa Chayeb, mhudumu katika mgahawa mmojawapo katika kituo cha kumbi za mkutano, KRAMA Palexpo, Tunis, unapofanyikia mkutano wa Umoja wa Mataifa ulioikusanya dunia nzima kujadili namna ya kutumia TEKNOHAMA. Kazi ya Amissa ni kuwapatia wateja huduma- chai, kahawa, maziwa na vitafuno kidogo - lakini dakika hii, hawapo. Afanyeje? Sana sana kutabasamu, akimngoja mmoja mmoja anayeingia.

TEKNOHAMA Yapamba Moto Tunis


MACHO ya dunia nzima yapo jijini Tunis, nchini Tunisia; Afrika Kaskazini. mataifa tajiri na maskini yamewakilishwa, kujadili namna ya kuzifanya teknolojia za habari na mawasiliano yamtumikie binadamu. Ujumbe wa Tanzania umeongozwa na Waziri wa Mawasiliano na Uchukuzi, Prof. Mark Mwandosya. Hapa katika picha, Prof. Mwandosya anafuatilia kikao cha maandalizi ya mkutano huo kilichohudhuriwa na mawaziri na maofisa kadhaa kutoka serikalini. Nyuma yake (aliyevaa miwani) ni Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Salim Msoma. (Picha na Ansbert Ngurumo)
My photo
Nimechongwa na mambo haya: Falsafa, Fasihi, Muziki, Habari na Harakati. Sifuati mkumbo. Napenda kuhoji na kudadisi - hulka ya kifalsafa ya kuusaka ukweli - 'UKWELI ULIO UCHI.'