Sunday, December 24, 2006

Baada ya mwaka Ikulu: Kikwete anayo furaha?

Baada ya mwaka mmoja Ikulu, Rais Jakaya Kikwete amebakiza miaka mitatu (si minne) madarakani. Anayo furaha aliyokuwa nayo awali? Watanzania wanayo furaha? Ameweza au ameshindwa nini? Bofya hapa tuulizane maswali.

Wednesday, December 20, 2006

Hii ni aibu baada ya miaka 45 ya Uhuru

Hata baada ya miaka 45 ya uhuru, tunashindwa kufanya vitu vidogo kama hivi, kuokoa Watanzania wenzetu! Je, wasio sehemu ya watawala wataokolewa na nani? Aibu!

Sunday, December 17, 2006

Blogu hii bomba!

Tangazo: Unataka kusafiri? Bofya hapa ujue bei ya tiketi ya ndege.

Sunday, December 10, 2006

Hii kali

Sina maelezo. Isome mwenyewe. Tafakari. Halafu jadili.

Mzee wa viwango na kasi anayongwa au anajinyonga?


Siku alipochaguliwa kuwa Spika wa Bunge la Tanzania, Samuel Sitta alijitangaza kuwa spika wa 'viwango na kasi.' Mwaka mmoja baadaye anaweza kujitambulisha kwa maeneno hayo? Anakuwa kinyonga au anajinyonga? Kama hukuridhika soma hii ndefu.

Monday, December 04, 2006

Ahadi za JK zaanza kutekelezwa


Wakati wa kampeni za urais mwaka 2005, JK alisema: "Tanzania Yenye Neema Inawezekana." Aliahidi "kushamirisha demokrasia." Na zaidi ya yote, aliahidi "maisha bora kwa kila Mtanzania" kwa ari mpya, kasi mpya na nguvu mpya. Mwaka mmoja umepua tangu aingie madarakani. Haya ndiyo matokeo ya ahadi hizo?

Friday, December 01, 2006

Mbowe na Obasanjo warejea darasani


Wanasiasa hawa wawili, Rais wa Nigeria, Olusegun Obasanjo, na aliyekuwa mgombea urais wa Tanzania mwaka 2005, Freeman Mbowe, wamefanana katika jambo moja mwaka huu - kurejea shule, kunoa ubongo. Tusisahau Waziri Mkuu, Frederick Sumaye, naye alijiunga na Chuo Kikuu cha Havard mapema mwaka huu.
My photo
Nimechongwa na mambo haya: Falsafa, Fasihi, Muziki, Habari na Harakati. Sifuati mkumbo. Napenda kuhoji na kudadisi - hulka ya kifalsafa ya kuusaka ukweli - 'UKWELI ULIO UCHI.'