Wednesday, November 29, 2006

Kura Za Mzee Wa Kombati Zilikwenda Wapi?


CCM walidai kwamba Mbowe alipata watu wengi kwenye kampeni kwa sababu watu walikwenda kushangaa helikopta. Nikiitazama picha hii naona jambo tofauti. Helikopta ipo uwanjani lakini hawaitazami. Wameiacha nyuma, wanamkodolea macho Mbowe (hayupo pichani). Tazama nyuso zao. Waliofuatilia kampeni zake wanajua hali ilikuwa hivyo kila mkutano wake wa kampeni Oktoba - Desemba 2005. Tazama mmoja wa washindani wake. Nimesikia watu wakijiuliza. Nami najiuliza. Na sasa nawauliza nyie wasomaji. Tuulizane. Hivi kura za Mbowe zilikwenda wapi?

Tuesday, November 21, 2006

Tazama Ubunifu


Rafiki yangu mmoja aitwaye Alex Kaija amenitumia picha hii. Nimemuuliza alikoipata akasema naye ametumiwa. Hamjui aliyeitengeneza. Nimevutiwa na ubunifu wake; nikaona vema niwashirikishe wasomaji wa blogu hii. Mnasemaje?

Sunday, November 19, 2006

Unasemaje juu ya vitisho vya Lowassa?


Waziri Mkuu, Edward Lowassa, amekuwa akitumia mabavu kukabiliana na wananchi wanaomkosoa, hasa magazetini. Makala HII imemuonya na kumtahadharisha juu ya athari za ubabe huo; hasa kwa mtu ambaye tayari ameshaonyesha nia ya kuwania urais baada ya Jakaya Kikwete. Una maoni gani?

Wednesday, November 08, 2006

Mbunge Huyu Ana Hoja, Asikilizwe


HII ni sehemu tu ya upungufu wa katiba ya nchi yetu ambayo tunaendelea kusisitiza kuwa iandikwe upya ili iendane na matakwa ya sasa. Kwa nini tulazimishane kuongozana kwa matakwa ya miaka 50 iliyopita? Kwa nini hatuoni kwamba na kizazi hiki kina mchango wake katika kukua kwa taifa?

Monday, November 06, 2006

Kifo cha Saddam Hussein


Hajafa, lakini mazingira yanaonyesha kuwa atakufa. Unasemaje kuhusu hukumu dhidi yake? Soma maoni ya "dunia," sifa zake na historia yake.

Thursday, November 02, 2006

Anaharibu hapa anahamishiwa pale

Kuna sababu za msingi za serikali yetu kuwalinda maofisa wanaofuja pesa zetu kwa kuwahamisha badala ya kuwachukulia hatua? Soma hapa kwanza, halafu utoe maoni.
My photo
Nimechongwa na mambo haya: Falsafa, Fasihi, Muziki, Habari na Harakati. Sifuati mkumbo. Napenda kuhoji na kudadisi - hulka ya kifalsafa ya kuusaka ukweli - 'UKWELI ULIO UCHI.'