Friday, December 28, 2007

Matokeo ya Uchaguzi Kenya

Fuatilia matokeo ya Uchaguzi Mkuu wa Kenya 2007 hapa. Inaeleka wenzetu wameamua kufanya 'mapinduzi ya awali ya uongozi.' Hadi sasa Raila Odinga wa ODM anaongoza; Mwai Kibaki wa PNU anafuata nyuma. Kalonzo Musyoka wa ODM-Kenya yuko mbali sana. Muujiza alioutarajia haujatokea! Umebaki kanisani! KANU kimeanza kupotea katika historia ya utawala wa Kenya. Endelea. Linganisha na hii pia.

Monday, December 24, 2007

Krismasi Njema


Napenda kuwatakia Krismasi Njema! Krismasi ni tukio lenye maana mbalimbali kwa watu mbalimbali. Kwa wengine ni 'kumbukumbu' ya kiroho ya kuzaliwa kwa Yesu Kristo zaidi ya miaka 2007 iliyopita. Kwa wengine ni tukio kubwa lililoigawa historia katika ngwe mbili - Kabla ya Kristo na Baada ya Kristo. Kwa wengine (hasa Ulaya Magharibi) ni wakati wa kumaliza mwaka, kujipongeza na kujiandaa kwa mwaka mwingine; ni kipindi cha manunuzi na matanuzi. Kwa wengine halina maana kabisa, lakini wanajikuta wakiungana na wenzao wanaosherehekea Krismasi. Kwa wote hao, nasema Heri ya Krismasi na Mwaka Mpya 2008.

Wednesday, December 19, 2007

CHADEMA na CCM: nani mwizi wa sera?

Vyama vya siasa vinaposhutumiana kwa kuibiana sera maana yake nini? Je, kati ya CHADEMA na CCM, ni kipi kimedhihirika 'kuiba' sera za mwenzake? Kuna mifano hai? Inaaminika? Tutafakari.
My photo
Nimechongwa na mambo haya: Falsafa, Fasihi, Muziki, Habari na Harakati. Sifuati mkumbo. Napenda kuhoji na kudadisi - hulka ya kifalsafa ya kuusaka ukweli - 'UKWELI ULIO UCHI.'