Sunday, June 29, 2008

Wanalinda skendo zao

Wabunge hawa ni hatari kwa taifa, lakini wanaakisi tu msimamo halisi wa wakubwa wao waliowatuma.

Friday, June 27, 2008

Happy Birthday Nelson Mandela!


Rais Mstaafu wa Afrika Kusini, Nelson Mandela, amesherehekea miaka 90 ya kuzaliwa, na miaka 10 ya ndoa yake na mkewe, Grace Machel. Bonyeza hapa umsikilize Graca akisimulia maisha yake ya kifamilia na Mandela; akizungumzia jambo moja ambao Mandela anasikitikia maishani mwake, na zawadi kuu ambayo yeye (Grace) amempatia Mandela katika miaka 10 ya ndoa yao. Lakini pia, Mandela anatoa rai kwa matajiri wa Afrika Kusini kutumia sehemu ya utajiri wao kusaidia maskini katika nchi hiyo.

Monday, June 23, 2008

Wabongo kwa ubunifu!

Sijui aliyeanzisha hii. Imenifikia, nikasema ngoja niwawekee wasomaji wa blogu hii. Isome mwenyewe hapa chini uone ubunifu wa Wabongo:


* Benjamin Mkapa Institute of Political Entrepreneurship and Openness

* David Balali Schoolof Central Banking and Foreign Debt Management

* AndrewChenge College of Applied Contractual Law

* AliHassan Mwinyi University of Inflation Control

* Karamagi Institute of Mining Licensing and Administration of Mining Contracts

* Zakia Meghji college of Tourism and Protection of Public Funds and Natural Resources

* Ditopile Mzuzuri School of Conveyance and Welfare of Public Drivers

* Mwalimu Nyerere University College of Privatization

* Mkono Institute of Legal Fraud Prevention

* Lowassa School of Prevention of Fake Companies

Fomu za Kujiunga zinapatikana Bank M. Nyote Mnakaribishwa.

Sunday, June 22, 2008

Raila "aongoza" watawala Afrika

Tatizo la Afrika ni kukosa viongozi wenye mitazamo ya kisasa. Waliopo sasa wamefungwa kwenye minyororo ya "ukale" wanaoendelea kuung'ang'ania. Lakini waziri Mkuu wa Kenya, Raila Odinga, anawataka watawala wa Afrika wachukue visu, wakate minyororo hii. Msikilize katika video hii. Amekuwa wa kwanza kumkaripia Rais Robert Mugabe wa Zimbabwe, na anataka viongozi wa Afrika waamke na kumkabili Mugabe, ili kudhibiti ukatili anaouendeleza dhidi ya watu wake.

Usafi wa Lowassa, uchafu wa CCM


CCM imesafisha Lowassa. Je, yenyewe imejisafisha? Tujadili.

Sunday, June 15, 2008

Wachache wameshinda

Mwaka mmoja uliopita umedhihirisha ushindi wa wachache dhidi ya wengi. Hoja yangu hii hapa.

Swali refu kuliko yote?

Swali hili limeulizwa Marekani, lakini hata Bongo wapo watu wanaouliza maswali mabaya kama hili hapa, linalodhaniwa kuwa swali refu kiliko yote.

Saturday, June 14, 2008

Dinner with Mugabe


Itazame video inayomjadili Rais wa Zimbabwe Robert Mugabe katika uchambuzi mfupi wa kitabu DINNER WITH MUGABE cha Heidi Holland.

Wednesday, June 11, 2008

Unabii wa Mpayukaji

Mpayukaji sasa amekuwa nabii. Na anahoji. "Maiti itazikwa au la?"

Monday, June 09, 2008

Mtanzania afariki Italia


Raia mmoja wa Tanzania, Omar Jaffar Ngwaya (pichani), amefariki dunia leo Jumatatu Juni 09, 2008, nchini Italia kwa ajali ya gari. Kwa mujibu wa Katibu wa Jumuiya ya Watanzania waishio nchini Italia, Kaguta NM, mipango ya mazishi ya marehemu Ngwaya inafanyika kwa kushirikiana na Balozi wetu nchini Italia. Taarifa za nyongeza zinapatikana katika tovuti hiyo hapo juu. Mungu ailaze roho yake mahali pema peponi! Amina!

Sunday, June 08, 2008

Kikwete anaweza kuwa mwalimu

Rais Mstaafu Benjamin Mkapa amekuwa mwalimu wa Rais Jakaya Kikwete; naye anaweza kuwafundisha wengine. Katika hili? Soma hapa.

Saturday, June 07, 2008

Clinton ampigia debe Obama


Seneta Hillary Clinton (pichani kushoto) amekubali rasmi kushindwa, amehitimisha kampeni zake na kumuunga mkono mshindi, Seneta Barack Obama, katika kinyang'anyiro cha urais wa Marekani mwaka huu kupitia chama ha Democratic. Sikiliza sehemu ya hotuba ya Hillary ya kumkubali Obama. Hotuba nzima ya Clinton hii hapa. Barack atachuana na Seneta John McCain katika uchaguzi mkuu Novemba 2008. Kundi la wagombea waliopambana na Obama katika chama chao, ambao amewashinda, ni hawa hapa.

Hii ndiyo pensheni ya Mkapa?

Rais Mstaafu Benjamin Mkapa amenukuliwa akisema kuwa yeye anaishi kwa pensheni kama alivyo Mzee Ali Hassan Mwinyi; kwamba hana utajiri wowote, na kwamba wanaomhusisha na biashara akiwa Ikulu na ufisadi mwingine unaozungumzwa wanamwonea kwa sababu eti alikataa kuwapendelea alipokuwa rais. Lakini Mzee Mkapa hajakanusha ujasiriamali wake wa Ikulu unaowakera wananchi. Baadhi ya yanayosemwa juu ya Mkapa, ambayo hajayakanusha kabisa, ni haya hapa. Je, hii ndiyo pensheni anayozungumzia?

Wednesday, June 04, 2008

Barack Obama: This is Our Moment


Msikilize Barack Obama hapa au hapa akihutubia mashabiki wake siku ya mwisho ya kampeni za awali, siku ambapo aliibuka mshindi na mgombea urais wa chama cha Democratic dhidi ya Hillary Rodham Clinton. Obama anasema huu ndio wakati wa Wamarekani kuleta mabadiliko wanayokusudia. Msikie Obama hapa katika mojawapo ya mahojiano aliyofanya kabla ya kukamilisha ushindi wake.

Tuesday, June 03, 2008

Sometimes size matters


Nimepokea picha hii kutoka kwa rafiki yangu, nikadhani inawafaa pia wasomaji wa blogu hii. Inafikirisha na kuburudisha.

Sunday, June 01, 2008

My photo
Nimechongwa na mambo haya: Falsafa, Fasihi, Muziki, Habari na Harakati. Sifuati mkumbo. Napenda kuhoji na kudadisi - hulka ya kifalsafa ya kuusaka ukweli - 'UKWELI ULIO UCHI.'