Saturday, September 27, 2008

Midahalo ya Obama na McCain


Sikiliza na fuatilia midahalo kati ya wagombea urais wa Marekani, Barack Obama na John McCain. Fanya tathimini na uchambuzi kujua nani zaidi.


1
. Mdahalo wa Kwanza: 27.09.2008.

2. Mdahalo wa Wagombea wenza (Joe Biden na Sarah Palin) 03.10.2008

3. Mdahalo wa Pili: 07.10.2008 au HAPA 4. Mdahalo wa Tatu: 15.10.2008

Wengine wameshatoa tathmini na kugawa alama B+ na B. Wewe unatoa ngapi?

Thursday, September 25, 2008

Tuwajadili Mabilionea wa Kikwete

Mabilionea wa Rais Jakaya Kikwete ni akina nani? Baadhi yao ni HAWA HAPA.

Monday, September 15, 2008

Zimbabwe kama Kenya


Mahasimu wa kisiasa nchini Zimbabwe, Rais Robert Mugabe na Kiongozi wa Upinzani, Morgan Tsvangirai, wamesaini makubaliano ya kugawana madaraka - baada ya usuluhishi uliofanywa na Rais wa Afrika Kusini, Thabo Mbeki. Mugabe ataendelea kuwa rais na mkuu wa nchi, huku Tsvangirai akiwa Waziri Mkuu na msimamizi wa Baraza la Mawaziri. Hata hivyo, hotuba za viongozi hao mara baadaya kusaini makubaliano hayo, zinaonyesha waziwazi tofauti walizonazo. Msikilize Mugabe hapa; na Tsvangirai hapa.

Sunday, September 14, 2008

Njiani kuelekea nyumbani


Hapa ni Brenda Zulu, Timothy Kasolo (Zambia) na mimi, tukiwa katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Oliver Tambo, Johannesburg, Afrika Kusini, njiani kuelekea makwetu baada ya mkutano wa Highway Africa. 13.09.2008

Sunday, September 07, 2008

Nipo Highway Africa

Wiki (6.9.2008 - 13.9.2009) hii nitakuwa Afrika Kusini, katika Chuo Kikuu cha Rhodes, kuhudhuria kongamano la kila mwaka la Highway Africa linalojadili matumizi ya teknolojia za kisasa katika kukuza mawasiliano na kuboresha maisha. Mada kuu ya mwaka huu ni Uandishi wa Kiraia: Uandishi kwa Manufaa ya Raia. Wapo Watanzania kadhaa nimekutana nao hapa, wakiwamo Mhariri Mtendaji wa Mwananchi, Theophil Makunga; Mtangazaji wa DTV, Dina Chahali; Mpiga picha na mwanablogu, Philemon Msangi (Bob Sankofa); Mwandishi anayeibukia, Furaha Thonya; Mhariri wa Mtanzania Jumapili, Eric Anthony na Ofisa Uhusiano wa CRDB, David Mbulumi. Habari zaidi za Highway Africa zinapatikana hapa. Sikiliza na matangazo mafupi ya redio kuhusu dhana ya mkutano.

Monday, September 01, 2008

Marafiki walimuonya Kikwete

Alionywa akapuuza. SOMA onyo lao hapa. Wenzake sasa wanamuhoji: Ni kazi ya serikali kubatiza au kusilimisha Watanzania?
My photo
Nimechongwa na mambo haya: Falsafa, Fasihi, Muziki, Habari na Harakati. Sifuati mkumbo. Napenda kuhoji na kudadisi - hulka ya kifalsafa ya kuusaka ukweli - 'UKWELI ULIO UCHI.'