Friday, October 30, 2009

Wednesday, October 28, 2009

Sasa tumejua, tatizo ni rais

Baada ya Rais Jakaya Kikwete kukiri kwamba wasaidizi wake walimshauri apumzike akakataa, ndiyo sababu akazidiwa hadharani pale Mwanza, sasa kumeibuka hoja mpya. Je, kama rais anadiriki kuwapuuza wasaidizi wake katika suala nyeti la afya yake, nao wananywea; atawezaje kuwasikiliza wasaidizi na washauri wake katika masuala ya uchumi, siasa, usitawi wa jamii na mengine? Si inawezekana rais ana washauri wazuri wa mambo mengi tu lakini hawasikilizi? Hii si sehemu ya ushahidi kwamba rais ndiye tatizo?

Wednesday, October 14, 2009

Tunayojivunia ndiyo haya?

Kwa mazingira haya ya elimu tunajivunia sera zilizopo na utekelezaji wake?

Sunday, October 11, 2009

JK akianguka tena daktari wake atasemaje?

SI vema kudhani kwamba viongozi wetu hawawezi kuumwa. Lakini ndivyo madaktari wa Rais Jakaya Kikwete wanavyotaka tuamini. Kwani wanadhani wakisema rais anaumwa tutamnyanyapaa? Kwani yeye si binadamu tu? Taarifa yao kwa umma, ambayo inakanusha tetesi za rais kuumwa, wakati yeye anazidiwa hadharani, si dalili kwamba wenyewe wanamnyanyapaa? Hili ndilo swali gumu la wiki hii. SOMA HAPA.

Thursday, October 01, 2009

Hotuba ya Mke wa Gordon Brown

Msikilize na mtazame Sarah Brown akimpigia debe mumewe, ingawa maji ya kisiasa yako shingoni mwa mumewe. Hotuba yake inaweza kuwavutia wanachama wa Labour. Je,itawashawishi wapigakura waliokwishachukia na kuamua kuleta mabadiliko?
My photo
Nimechongwa na mambo haya: Falsafa, Fasihi, Muziki, Habari na Harakati. Sifuati mkumbo. Napenda kuhoji na kudadisi - hulka ya kifalsafa ya kuusaka ukweli - 'UKWELI ULIO UCHI.'