Friday, August 31, 2007

Hekalu la Manji?

Bwana ee! Tazama nyumba hii. Lakini Waswahili wanasema imevuka viwango vya kuitwa nyumba. Hili ni Hekalu. Na hizi hapa chini ni sehemu chache za hekalu hilo. La nani? Aliyetuma hizi ni la Yusuf Manji - yule mfadhili wa Klabu ya Yanga; "mgomvi" wa Regi Mengi (na sasa hivi Waislamu kuhusu kiwanja); mfadhili wa Chama Cha Mapinduzi (CCM); lakini mmoja wa wasomaji wa blogu hii anasema si kweli bali ni nyumba ya Rais Pervaiz Musharaf, mtu aniyejipenda kweli kweli, mchezaji hodari wa Badminton, Jenerali wa Pakistani. Iwe ya yeyote yule, inapendeza na kuvutia. Tazama!

Endelea


Sema mwenyewe


Quite Spacious


Hapa je?


Safi


Chunga, chini panateleza


mh


Mh!


Tuizunguke meza hii


Zungumza, ukichoka pumzika kidogo


Unataka kuogelea?



Labda haya ndiyo Maisha Bora. Tumuulize Kipanya hapo chini!

Thursday, August 30, 2007

Maisha Bora


Nimeipenda katuni hii ya Maosud 'Kipanya.' Wewe je?

Zitto apikiwa kashfa mpya


Habari zilizotapakaa ni kwamba wanamtandao, wakiongozwa na kinara wao, Rostam Azizi, wanapika kashfa mpya dhidi ya Zitto Kabwe (pichani kulia). Eti walitengeneza ya Amina Chifupa ikawalipukia na kuua mtu. Hawakuridhika. Wamejarbu kumdhalilisha Bungeni, akaibuka mshindi. Wananchi wanamshangilia, CCM wakazomewa. Sasa wamesikia Zitto na viongozi wa CHADEMA wanaanza kuzunguka mikoa 10 kuishitaki serikali kwa umma, wanamtandao wanakula njama mpya kwa kutumia baadhi ya vyombo vya habari 'kupika' kashfa mpya. Nia yao ni kupunguza imani ya wananchi na mvuto wa Zitto. Wamekiri, lakini inawauma, kwamba kwa sasa, Zitto amemfunika JK kwa mvuto.

Je, wahariri watakubaliana na mbinu za kina Rostam Azizi? Je, wananchi watamtosa Zitto? Kumkumbatia nani? Je, serikali itabadili sera zake kuhusu madini au itaendelea tu kuhangaika na namna ya kumsakama Zitto?

Tuesday, August 21, 2007

Uchumi ukue, bei zipande hivi?

Waziri Mkuu, Edward Lowassa, anasema uchumi unakua. Lakini wataalamu wanasema bei za bidhaa zinapanda kila siku. Ni ukuaji gani huu wa uchumi? Habari hii imeandikwa na gazeti la serikali, Daily News Agosti 21.08.2007. Soma mwenyewe uone hali ilivyo.

Inflation nears double digits

Overall inflation rate jumped to nine per cent in July, from 5.9 per cent in June, a trend which the National Bureau of Statistics (NBS) attributed to increased food and non-food prices.

“The July 2007 inflation rate has gone up by 3.1 percentage points compared to the June figure,” the Bureau said in a statement made available yesterday. “Some prices for both food and non-food items had gone up,” it added.

Analysts feared the impact of price hikes on the economy, with inflation, a key indicator for consumer comfort and investor confidence, nearly hitting the double digit mark, the highest in more than five years.

The government had for the last three years, targeted to push inflation to a manageable below 4.0 per cent, which could now prove to be quite an uphill task. Before, inflation had nearly dragged the economy to its knees with almost record over 30 per cent rate.

Planning, Economy and Empowerment Minister Professor Juma Ngasongwa told parliament in June that in 2006, average inflation was 7.3 per cent, compared to 5.0 per cent in 2005. In March, this year, inflation was recorded at 7.2 per cent.

The minister attributed the upswing in inflation to increased commodity prices, especially food and petroleum products which also led to high costs of transport and generation of thermal electricity.

The minister expressed optimism on declining inflation after some parts of the country started harvesting food crops, saying in April 2007, the inflation rate had declined to 6.1 percent, from 7.2 per cent registered in March 2007.

NBS said in the statement yesterday that hiked food prices were wheat flour, bread, spaghetti, potatoes and meat. Prices of bananas, fish, cooking oils, beans, cowpeas, sugar and meals in restaurants had also gone up.

It said non-food items that had increased prices were instant coffee, rent, kerosene, electric cookers, sewing machines, kerosene stoves, laundry soap (bar and powdered), scrubbing brush, broom head, tooth brush and hair creams.

Prices that have also gone up include those of car batteries, diesel, petrol, bus fares and private secondary school fees.

However, it noted that prices of clothing, footwear, watches and cell phones had gone down.


Daily News Reporter
Daily News; Tuesday,August 21, 2007 @00:02

Sunday, August 19, 2007

Picha nyingine za Zitto na waandamanaji

Bonyeza hapa uone picha na usome mjadala mwingine mpana.

Habari Leo waua stori ya Zitto Kabwe


Magazeti ya serikali, Sunday News and Habari Leo Jumapili, 'yalikataa' kuandika habari za maandamano na mkutano wa Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe, uliofanyika Dar es Salaam Agosti 18 kulaani hatua dhalimu ya Bunge dhidi ya mbunge huyo. AIBU!
Waandishi wao waliyashuhudia maandamano, mkutanoni walikuwepo, lakini walishindwa kutekeleza wajibu wao wa kitaaluma. UZALENDO uko wapi? Kama wanawadharau hao waliokusanyika kumsikiliza Kabwe, wanamwandikia nani?
Hata hivyo, mpiga picha wao aliweza kumshawishi mhariri wake kutumia walau picha inayoonyesha sehemu tu ya umati uliokusanyika Jangwani kumsikiliza Kabwe. Tazama mwenyewe.

Karamagi anasafiri na mihuri yetu?


KAMA Waziri wa Nishati na Madini, Nazir Karamagi, anaweza kusaini mkataba wa madini nje ya nchi, London, Uingereza, wakati yuko ziarani na Rais Jakaya Kikwete, ina maana anasafiri na mihuri yetu? Pata uchambuzi wa swali hili HAPA, na toa maoni yako chini.

Saturday, August 18, 2007

Kishindo cha Zitto Kabwe


Dar es Salaam inazizima. Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe, amegeuka shujaa wa mwaka. Habari kutoka Dar zinasema amekuwa gumzo kila kona, wala mvua nzito haikuweza kuwazuia wananchi kuandamana na kusukuma gari lake kutoka Ubungo hadi viwanja vya Jangwani, Jumamosi, Agosti 18, 2007, alikohutubia mkutano mkubwa na kusema Waziri wa Nishati na Madini, Nazir Karamagi, alisaini mkataba katika Hoteli ya Churchill, London, Uingereza.

Watawala wameduwaa. Bomu walilompasulia Zitto kumdhalilisha limewalipukia wenyewe! Hiki ndicho kishindo kinachozungumzwa. Anasema "tusikumbatie walioshiba" Ipate pia kwa kimombo Hoja kamili na mjadala wake Bungeni HII HAPA. Baadaye, wawekezaji wenyewe, Barrick walijitokeza kutoa maelezo HAYA, lakini Zitto akayachambua pia maelezo hayo na kubainisha uhusiano wa karibu sana kati ya waziri na wawekezaji, huku wakitoa maelezo yanayojikanganya zaidi.
My photo
Nimechongwa na mambo haya: Falsafa, Fasihi, Muziki, Habari na Harakati. Sifuati mkumbo. Napenda kuhoji na kudadisi - hulka ya kifalsafa ya kuusaka ukweli - 'UKWELI ULIO UCHI.'