Tuesday, June 29, 2010

Raila Odinga apasuliwa kichwa

SOMA habari zake hapa.

Urafiki huu ni wa kweli?




Ama kweli, swala huyu ana bahati isiyo ya kawaida ya "kupendwa" na chui!

Friday, June 25, 2010

Ya Italia na Ufaransa


Mtu mmoja ameandika katika tovuti ya BBC, akizungumzia timu za Italia na Ufaransa, na kulinganisha nguvu ya timu hizo katika fainali mbili. Anasema:"Inashangaza kidogo kwamba katika fainali za 2006, Italia na Ufaransa walikutana uwanjani katika mechi ya mwisho ya fainali; katika fainali za mwaka 2010, timu hizo hizo zimekutana uwanja wa ndege" (wakiwa safarini kurejea makwao baada ya wote wawili kutolewa katika hatua ya awali).

Monday, June 21, 2010

Siasa za JK na mwanaye

RAIS Jakaya Kikwete amemkabidhi mtoto wake Ridhiwani, fomu za kumuombea wadhamini 250 kwa mikoa 10 nchini ili kutimiza vigezo vya kuwa mgombea urais kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM. Hafla ya makabidhiano hayo ilifanyika nyumbani kwake mjini hapa ambapo zaidi ya vijana 40 watakaoongozwa na Ridhiwani walihudhuria. Mtoto huyo wa rais Kikwete, amechaguliwa kuwa kiongozi wa vijana katika kuhakikisha mgombea huyo anapata wadhamini wa kutosha kwa mujibu wa sheria na kanuni za CCM.

Kwa habari zaidi soma magazeti. Mzee wa Maswali Magumu amelijadili hili kwa kifupi.

The best thing: Brazil is winning


Nimefurahishwa na jinsi jamaa huyu alivyoripoti stori ya mechi kati ya Brazil na Ivory Coast.

Saturday, June 12, 2010

Saa mbili za Maradona


SOMA hapa ujue kwa nini Kocha wa Timu ya Taifa (Soka) ya Argentina, Diego Maradona, anapenda kuvaa saa mbili - moja kila mkono.

Wednesday, June 09, 2010

'Kichwa cha Zidane' chatukuzwa


Tazama wenzio wanavyokitumia kutangaza biashara zao na kuvuna mapesa. PICHA YA KWANZA PICHA YA PILI. PICHA YA TATU.

Thursday, June 03, 2010

Ziro ya Sumaye na Ombwe la Kikwete, kipi bora?

SOMA mjadala mpya kuelekea Uchaguzi Mkuu 2010. Usikose pia kusoma ONYO hili kwa Watanzania. Linakuhusu. Katika kuendeleza mjadala, Mtanzania mwingine amemtaka Rais Mstaafu, Benjamin Mkapa, aokoe jahazi. Kwa vipi? Soma HAPA.

Wednesday, May 12, 2010

Waingereza wapata serikali mpya

Mseto huu waweza kuwa bora kuliko miseto ya Kenya na Zimbabwe? Fuatilia muundo wa serikali mpya inayoongozwa na David Cameron.

Friday, April 23, 2010

Uchaguzi Mkuu: Mdahalo wa wanasiasa Uingereza

Watazame, wasikilize na watathmini wanasiasa hawa wanaogombea ukubwa wakijieleza katika mdahalo wao wa pili. Ni David Cameron (Conservative), Gordon Brown (Labour) na Nick Clegg (Lib Dem).

Tuesday, April 20, 2010

Mourinho haishiwi hoja kwa waandishi

Wakati Inter Milan na Barcelona zikijiandaa kuchuana katika ngwe ya kwanza ya nusu fainali, Kocha wa Inter, Jose Mourinho, amezungumza na waandishi kwa kujiamini. Msome hapa.. Na baada ya kuifunga Barcelona, aliwasifu vijana wake na kuwaponda washindani, lakini akaonya kuwa safari ya kuelekea Madrid bado ndefu. Naye Rais wa Klabu, Massimo Moratti, aliwasifu Inter, akammwagia sifa kocha, akisema: "wanatisha."

Thursday, April 08, 2010

Mgeni mwingine


Wageni bado wapo. Huyu ninayezungumza naye ni Maria Drantenberg, raia wa Norway, ambaye alinitembelea ofisini kwangu (06.Aprili.2010) kujadili hali na maendeleo ya vyombo vya habari na demokrasia Tanzania.

Wednesday, March 31, 2010

Kigogo wa kwanza CCM ajiunga CCJ


Ni Mbunge wa Kishapu, Fred Mpendazoe, ambaye amevijua uanachama wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), na kwa mantiki hiyo, kujivua ubunge. Ameandika historia. Na habari zinasema kuwa vigogo wengine wanajiandaa kumfuata. Tusubiri tuone.

Thursday, March 18, 2010

Tunajadili utendaji wa vyombo vya habari


Katika picha hii, nafafanua jambo kwa mgeni wangu Anni Lyngskaer, raia wa Denmark aliyenitembelea ofisini kwangu, kujadili utendaji wa vyombo vya habari nchini. (Picha kwa hisani ya Francis Dande Machi 17, 2010)

Monday, March 15, 2010

Wakaukosa mpira, wakatwangana wenyewe

Watatu wanamkaba mmoja kwa kuwa alikuwa anatisha! Mshambuliaji mahiri wa Salehe Mohammed wa Free Media FC (mwenye njano) akikabiliana na mabeki wa Mwananchi FC. 13.03.2010, Uwanja wa Sigara, Dsm.

Huu ndiyo mwisho wa Beckham kucheza soka?

Fuatilia uchambuzi huu.

Hata kabumbu twasakata


Mnamzungumzia Drogba? Wapo wengine, hata kama hawavumi! Siku zinasogea, lakini stamina haijapotea kabisa. Anza na hiyo. Nyingine zitafuata za Machi 13, 2010 (Free Media vs Mwananchi). Tulifungana idadi hii ya magoli. Wengine tuliacha vipande vya miguu uwanjani.
My photo
Nimechongwa na mambo haya: Falsafa, Fasihi, Muziki, Habari na Harakati. Sifuati mkumbo. Napenda kuhoji na kudadisi - hulka ya kifalsafa ya kuusaka ukweli - 'UKWELI ULIO UCHI.'