Monday, April 20, 2009

DECI, dini na siasa

Tathmini yangu fupi ni kwamba sakata la kampuni ya DECI inayoendesha upatu limechukua muda mrefu kwa kuwa wamiliki walimau kutumia dini kuhujumu wananchi maskini huku wakijificha katika kivuli cha siasa zetu. Ndiyo maana waliweza kusitawi kwa miaka mitatu bila kuguswa na vyombo vya usalama wa taifa. Walipata imani ya umma na ulinzi wa dola usio rasmi. Sasa wameshtukiwa, lakini tazama suala hili linavyojaa utata na kuchukua muda mrefu kutekelezwa. Ni dini na siasa ulingoni. Sijui wewe unasemaje.

No comments:

My photo
Nimechongwa na mambo haya: Falsafa, Fasihi, Muziki, Habari na Harakati. Sifuati mkumbo. Napenda kuhoji na kudadisi - hulka ya kifalsafa ya kuusaka ukweli - 'UKWELI ULIO UCHI.'