Picha hizi mbili zinaonyesha sehemu tu ya umati wa wakazi wa Mbeya mjini uliompokea Dk.Willibrod Slaa kumdhamini ili agombee urais 2010 kupitia Chadema (03/08/2010)
Tunahitaji kujua kwa sababu hatujui; na hatuwezi kujua kama hatujui kwamba hatujui...Hatutajua chochote iwapo hatutahoji na kudadisi. Na kadiri tunavyojua, ndivyo tunavyogundua kwamba hatujui...
Tuesday, August 03, 2010
Dk. Slaa aiteka Mbeya
Picha hizi mbili zinaonyesha sehemu tu ya umati wa wakazi wa Mbeya mjini uliompokea Dk.Willibrod Slaa kumdhamini ili agombee urais 2010 kupitia Chadema (03/08/2010)
Monday, August 02, 2010
Friday, July 09, 2010
Dk. Shein apeta
CCM Zanzibar wamepata mgombea urais. Matokeo ya kura za NEC Dodoma yanasema hivi: Shein 117: Bilal 54: Nahodha 33.Hata hivyo, taarifa kutoka ndani ya vikao vya CCM zinasema Dk. Bilali alipata kura 119 kutoka wa wajumbe. Akafuatiwa na Dk. Shein (63) na Nahodha (22). Hayo ndiyo maajabu ya CCM, ma ndiyo maana Wazanzibari hawakosi kulalamikia kitendo cha rais wao kuchaguliwa Dodoma badala ya Zanzibar. Na hivi ndivyo Dk. Bilali alivyozibwa mdomo kwa kupewa nafasi asiyoitaka ya kuwa mgombea mwenza wa JK.
Wednesday, July 07, 2010
URAIS Z'BAR: Dk. Shein akamiwa

BAADHI ya wanaCCM Zanzibar waliopo Dodoma wametishia kumburuza mahakamani Dk. Mohammed Gharib Shein na kuzuia uchaguzi iwapo chama kitampitisha kugombea urais. Wengine walio Zanzibar wanaendelea kusambaza vipeperushi vinavyokihamasisha Chama cha Wananchi (CUF) kijiandae kuingia madarakani ikiwa Dk. Shein atapitishwa kugombea urais. Wanadai Shein si chaguo la Wazanzibari, bali la vigogo wa Bara na Rais Amani Karume. Na baadhi yao wananukuu Katiba ya Zanzibar ya mwaka 1984 kuthibitisha kwamba Dk. Shein "amepoteza sifa" ya kugombea urais kwa kuwa amejiandikisha kupiga kura Bara. Ama kweli wamemkamia.
Sunday, July 04, 2010
Mdahalo wa wagombea urais Zanzibar
Tuesday, June 29, 2010
Friday, June 25, 2010
Ya Italia na Ufaransa

Mtu mmoja ameandika katika tovuti ya BBC, akizungumzia timu za Italia na Ufaransa, na kulinganisha nguvu ya timu hizo katika fainali mbili. Anasema:"Inashangaza kidogo kwamba katika fainali za 2006, Italia na Ufaransa walikutana uwanjani katika mechi ya mwisho ya fainali; katika fainali za mwaka 2010, timu hizo hizo zimekutana uwanja wa ndege" (wakiwa safarini kurejea makwao baada ya wote wawili kutolewa katika hatua ya awali).
Monday, June 21, 2010
Siasa za JK na mwanaye
Kwa habari zaidi soma magazeti. Mzee wa Maswali Magumu amelijadili hili kwa kifupi.
Monday, June 14, 2010
Saturday, June 12, 2010
Saa mbili za Maradona

SOMA hapa ujue kwa nini Kocha wa Timu ya Taifa (Soka) ya Argentina, Diego Maradona, anapenda kuvaa saa mbili - moja kila mkono.
Wednesday, June 09, 2010
'Kichwa cha Zidane' chatukuzwa

Tazama wenzio wanavyokitumia kutangaza biashara zao na kuvuna mapesa. PICHA YA KWANZA PICHA YA PILI. PICHA YA TATU.
Thursday, June 03, 2010
Ziro ya Sumaye na Ombwe la Kikwete, kipi bora?
Wednesday, May 12, 2010
Waingereza wapata serikali mpya
Friday, April 23, 2010
Uchaguzi Mkuu: Mdahalo wa wanasiasa Uingereza
Tuesday, April 20, 2010
Mourinho haishiwi hoja kwa waandishi
Friday, April 16, 2010
Thursday, April 08, 2010
Mgeni mwingine
Wednesday, March 31, 2010
Kigogo wa kwanza CCM ajiunga CCJ
Saturday, March 27, 2010
Thursday, March 18, 2010
Tunajadili utendaji wa vyombo vya habari
Monday, March 15, 2010
Wakaukosa mpira, wakatwangana wenyewe
Hata kabumbu twasakata
Friday, March 12, 2010
Tuesday, March 02, 2010
Thursday, February 18, 2010
Wabunge wetu vibogoyo
Sunday, February 07, 2010
Mbaya kwa wanaotaka kusomea Uingereza
Wednesday, February 03, 2010
Saturday, January 30, 2010
Ngoma ya Dodoma ichezewe Unguja?
Dare s Salaam
WANAOTILIA shaka hoja yetu ya muda mrefu kuwa Tanzania inakabiliwa na ombwe la uongozi, watazame kinachoendelea ndani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) na serikali.
Chama tawala kinaendelea kumeguka. Mwenyekiti hajui aunge mkono kundi gani katika mmeguko huo.
Anaitisha vikao vikuu vya chama, wasaidizi wake wanamgomea, naye anaviahirisha. Wabunge wa chama tawala wanamgomea Waziri Mkuu (mwenyekiti wao) wakipinga muswada wa gharama za uchaguzi. Chama tawala kinaweweseka na kutishwa na “chama hewa” cha CCJ, ambacho kimekwua gumzo nchi nzima kwa wiki nzima, ingawa hakijasajiliwa.
Hiki ni chama ambacho kimekufa kabla ya kuzaliwa, maana wenye chama chao wamekosa ujasiri wa kujitambulisha na chama chao. Wamekikana.
Lakini CCM imekiogopa mno kiasi cha kusambaza waraka nchi nzima kuwaonya wanachama wake dhidi ya CCJ; huku ikijua ifika kuwa wanachama wa CCJ ndio hao hao wa CCM!
Chama imara, chenye uongozi imara, kisingepata kizunguzungu kwa hisia za kuundwa kwa chama kingine. Lakini CCM kimetudhihirishia kwamba nguvu pekee inayokipa uhai ni dola.
CCM bila dola – bila majeshi, bila tume za uchaguzi, bila serikali na taasisi nyingine zinazokitegemeza – hakipo.
Yanayokitikisa CCM ni mengi, hata nguvu ya chama chenyewe upande wa Zanzibar, ambayo sasa imeakisi nguvu halisi ya Rais wa Zanzibar, Amani Abeid Karume.
Rais Karume ametunisha msuli, CCM (Bara) imenywea; Serikali ya Muungano imenyong’onyea. Na kwa hali ya kisiasa ya sasa nchini, tunaweza kusema kwamba walau sasa Karume ameonyesha maana ya kuwa rais wa nchi.
Rais wa nchi ni yule anayesimama kidete kutetea kwa nguvu zote masilahi ya watu wake, hata ikibidi atofautiane na wenzake.
Rais Karume ameona bora kutofautiana na viongozi wenzake wa Muungano, iwapo kwa kufanya hivyo, ataweza kutetea maslahi ya kile kinachomfanya aitwe rais.
Katika miezi miwili iliyopita, Karume amekuwa na utambuzi wa ajabu wa nguvu na umuhimu wake katika siasa za Tanzania. Amekohoa, wenzake wa Bara wamepata mafua!
Ameamua kuwa muasi. Sasa wao wanamuita msaliti. Lakini hakuanza leo. Kumbukumbu zinaonyesha kuwa usaliti wa Karume ulianzia Butiama, mwanzoni mwa mwaka 2008, alipoathiri mwelekeo wa hoja ya serikali ya mseto Zanzibar; akapendekeza isitekelezwe bila kura ya maoni.
CCM, ambayo ilikuwa imeshaafikiana na Chama cha Wananchi (CUF) kupitia kamati ya mwafaka, kwamba iwepo serikali ya mseto Zanzibar, ilinywea na kuimba wimbo wa Karume.
Kwa hiyo hata sasa hivi, (wapinzani wa Karume) wanapojitapa kwamba wanafuata maazimio ya Butiama, ukweli ni kwamba wanafuata mapendekezo ya Karume. Na yeye anayasisitiza maazimio hayo kwa sababu ni zao la maoni yake. Hajapoteza!
Bahati mbaya Karume alichelewa kutambua nguvu yake. Siku zote alijiona yeye ni makamu mwenyekiti wa CCM, Visiwani. Alisahau kwamba yeye ni rais, kiongozi wa nchi.
Wengine tunadhani kwamba kilichomfanya awe mnyonge ni mchakato wa kisiasa uliomfikisha Ikulu. Haukuwa mchakato sahihi, wala haukuwa huru na wa haki. Alijua kuna walioshinda na waliotawala. Yeye alikuwa kwenye kundi la watawala, lakini hakuwa katika kundi la washindi.
Imemchukua miaka tisa (9) kujiamini na kutumia urais wake kutetea Wazanzibari. Katika miaka tisa iliyopita, ngoma ilikuwa inapigwa Dodoma, Karume anaichezea Zanzibar.
Sasa ameshtuka. Ameamua ngoma ya Wazanzibari ipigwe na kuchezewa Unguja! Ametuma ujumbe mzito kwa CCM na serikali. Wenye akili wameshaupokea; kwamba si haki na si sahihi kwa CCM kumchukulia Karume kama wanavyomchukulia Makamu Mwenyekiti wa CCM, Bara, Pius Msekwa, au Katibu Mkuu wa CCM, Yusuph Makamba.
CCM (Muungano) ilipoandaa vikao vya Kamati Kuu na Halmashauri Kuu Wazanzibari wakagoma ikaahirisha, na baadaye ikaandaa kikao cha dharura Karume na wenzake wakagoma kuhudhuria, ikaahirisha tena; imedhihirisha kwamba haiwezi kwenda bila nguvu ya Karume.
Sisi siri kwamba kama Karume angehudhuria vikao hivyo, wenzake wa Bara wangevitumia (kwa wingi wao na ubabe wa kihistoria) kumbana na kumwadabisha.
Kwa hatua yake ya sasa, ya kuwagomea na kuitisha kikao maalumu huko Zanzibar, amethibitisha kwamba ana uwezo wa kuzichonga siasa za Zanzibar zikawa tofauti na jinsi ambavyo wenzake wasio Wazanzibari wanataka ziwe.
Amewafungua macho wana CCM wenzake wa Zanzibar kwamba wakiamua, wanaweza kuleta mageuzi makubwa katika taifa lao. Sasa wametambua, na wamedhihirisha kwamba wao si mkoa ndani ya Tanzania, bali ni taifa ndani ya taifa.
Wana serikali yao; katiba yao; bendera yao; Bunge (Baraza la Wawakilishi) lao; tume yao ya uchaguzi; wimbo wao wa taifa.
Utaifa huu wa Zanzibar ndiyo uliowafanya Karume na hasimu wake mkuu kisiasa, Katibu Mkuu wa CUF, Maalim Seif Shariff Hamad, kukutana na kujadili mustakabali wa taifa lao.
Kwa Karume na Maalim Seif, Uzanzibari wao ni muhimu kuliko Utanzania wao. Imesemwa mara nyingi, na sasa wao wamethibitisha, kwamba linapofika suala la maslahi ya Zanzibar, CUF na CCM ni kitu kimoja.
Kwao, maendeleo ya Zanzibar, kwa muda mrefu, yameathiriwa na kile wanachokiita “ukoloni wa Bara.” Hawa ni watu wanaopigana kujinasua kwenye “ukoloni” wa Serikali ya Muungano.
Ndiyo maana Karume na Maalim Seif wameungana sasa. Kwao, Zanzibar kwanza; Tanzania baadaye.
Si hilo tu, lakini pia wanazingatia ukweli kuwa Wazanzibari wasipoamua kushughulikia matatizo yao wenyewe, wakiamua kuwaachia wabara wayamalize kwa niaba yao, hayatakoma.
Wamechoka kuendesha siasa za Zanzibar kutoka Dodoma; maana wanaweza kufanya hivyo wakiwa Unguja.
Rais Karume aliingia madarakani kwa nguvu, jeuri na aibu. Sasa anajiandaa kuondoka madarakani kwa heshima na utukufu uliowashinda watangulizi wake.
Watafiti na wachambuzi wa masuala ya kisiasa Zanzibar wanajua na wamesema mara kadhaa kwamba Rais Karume aliupata urais wake bila ushindi utokanao na wingi wa kura halali.
Sasa amepata ushindi dhidi ya nguvu kongwe za CCM zitokazo katika Serikali ya Muungano (Bara), na ameanza kushinda hila za wasaidizi wake na washindani wake wa Zanzibar wanaohaha kumrithi baadaye mwaka huu.
Karume huyu hawezi kuendeshwa kwa maazimio yanayotokana na ushawishi au nguvu ya hoja za akina Msekwa au Katibu Mkuu wa CCM, Yusuph Makamba. Kwake, hawa nao ni sehemu ya “wakoloni” hao wa Muungano.
Ndiyo maana wanaojua siasa za Zanzibar wanakiri kwamba kama Karume asingekuwa nyuma ya ajenda ya CUF kutaka katiba irekebishwe, kuanzishwe serikali ya mseto na mchakato huo usimamiwe na Karume mwenyewe, wana CCM katika Baraza la Wawakilishi wasingeunga mkono hoja ya chama hicho cha upinzani.
Na kama kuna ujumbe CCM inapaswa kuupata kutoka kwenye uamuzi wa baraza kuridhia hoja ya CUF ni mmoja – kwamba umma wa Wazanzibari sasa unaandaliwa kwa kura ya maoni itakayokuwa kama watakavyo watawala.
Ndiyo maana baadhi yetu tunaiona serikali ya mseto Zanzibar inakuja. Ndiyo tafsiri ya kauli ya Karume kwamba rais kutoka Pemba si dhambi. Ndiyo maana naye sasa ana ujasiri wa kuimba wimbo ule ule wa wapinzani, wa muda mrefu, kuwa mafuta ya Zanzibar (kama yapo) yasiwe suala la Muungano.
Wala hatulalamiki, maana huu ni uamuzi uliochelewa. Zanzibar yenye amani haiwezi kuongozwa kwa siasa za ubabe, jeuri, vinyongo na visasi. Wala haiwezi kuwa chini ya chama kimoja tu, maana hata wanaotangazwa kuwa wameshindwa wanakuwa na karibu nusu ya kura zote zilizopigwa.
Lakini kuna jambo ambalo CUF wanalisisitiza; kwamba baada ya miaka 10 madarakani, Rais Karume hana tena uchu wa madaraka. Amekua, ameongoka na yuko tayari kutambua na kutimiza matakwa ya Wazanzibari.
Yupo tayari kuwaunganisha Wazanzibari na kustaafu kwa mbwembwe. Anatafuta ushujaa ambao rais yeyoye mpya atakayeingia madarakani angependa kuutafuta baada ya miaka 10 Ikulu.
Kwa hiyo, ni vema Karume anayemaliza na mwenye nia, apewe fursa (ya walau miezi 6 hadi miaka miwili) asimamie utekelezaji wa makubaliano yake na Maalim Seif.
Katiba irekebishwe, sheria za uchaguzi zirekebishwe, tume ya uchaguzi irekebishwe, wapiga kura wandikishwe upya (vema) na kadhalika. Baada ya hapo, uitishwe uchaguzi huru na wa haki; atakayeshinda amkaribishe aliyeshindwa (maana itakuwa kwa asilimia ndogo tu) waunde serikali ya mseto.
Mwisho wa yote, Karume atastaafu kama shujaa; na Wazanzibari watakuwa wameanza siasa mpya za ushindani usio na uhasama. Nani asiyeitaka Zanzibar ya namna hii?
Ni wazi, wapo baadhi wanaonufaika na siasa za Zanzibar kwa jinsi zilivyo leo. Wapo pia wanaojiandaa kugombea urais baada ya Karume, na wasingependa kuendeleza urithi wa Karume na Maalim Seif.
Kete yao ni moja. Iwapo Karume ataondoka bila kuyaingiza kwenye mfumo mazungumzo yake na Maalim Seif, yatafutika siku ya kwanza ya utawala mpya, naye ataishi maisha ya kula pensheni ya aibu.
Hadi sasa, Karume, kwa hiki kidogo alichofanya, amekuwa shujaa mbele ya Watanzania wengi. Amefuta aibu ya muda mrefu, na amevaa ujasiri wa ajabu unaojitokeza kwa sura ya uasi na usaliti.
Akitaka kuupoteza ushujaa wake huu, alegeze kamba, apoteze nia, awasikilize wanaomsonga kutoka Bara na visiwani. Aatapoteza ushujaa na heshima yake binafsi, na ataitokomeza amani ya Zanzibar ambayo sasa iameanza kuchanua.
Wakristo wanaamini kwamba kama Yuda asingemsaliti Yesu, kile wanachokiita ukombozi wao kisingepatikana. Yawezekana Karume pia amegundua kwamba asipomsaliti Rais Jakaya Kikwete na CCM yake, ukombozi wa Wazanzibari hautapatikana.
Kwa nini asiasi kama amegundua kuwa wakubwa hawana nia njema na Zanzibar? Na kama tunataka ukombozi wa Zanzibar, kwa nini tusimsaidie Karume kuwadhibiti “wahuni” wa Bara wanaohaha kumzuai asiasi zaidi?
ansbertn@yahoo.com +255 653 172 665
Saturday, December 19, 2009
Sindiketi za watawala
Thursday, December 17, 2009
Wakubwa waumbuliwa na vitu vidogo vidogo
Monday, December 14, 2009
Waitaliano wambonda Waziri Mkuu wao
Monday, December 07, 2009
Sunday, November 29, 2009
Chafya ya Rais Mkapa
Sunday, November 22, 2009
Sunday, November 01, 2009
Pinda kaishitaki Ikulu; wabunge wataishinda?

Ni kielelezo cha uwezo mdogo wa serikali kimkakati kutumia TAKUKURU kuwaandama wabunge wale wale wanaoituhumu TAKUKURU hiyo hiyo. Taifa liko gizani kwa sababu ya maamuzi mabovu na ufisadi wa watawala; maazimio ya Bunge kuhusu Richmond hayajatekelezwa; taifa linasubiri taarifa ya serikali kuhusu suala hili, kumbe wao wanaleta utoto wa 'posho mbili' zao?
Nani amewaruhusu Ikulu na TAKUKURU kupachika ajenda dhaifu katika nafasi ya ajenda kuu? Nani amewaruhusu kuandama wabunge wale wale ambao katika mjadala wa kashfa ya Richmond ndio waliopendekeza kigogo wa TAKUKURU achukuliwe hatua?
Hivi mtu akikutuhumu na wewe ukamtuhumu unakuwa mtu safi kuliko yeye, na unapata nguvu ya kumchukulia hatua? Ikulu na TAKUKURU wanadhani njia sahihi ya kujisafisha ni kuwaandama wanaoituhumu TAKUKURU na Richmond yao?
TAKUKURU ambayo haikuona ufisadi wa Richmond kulipwa milioni 152 kwa siku, tena bila kuzalisha umeme; TAKUKURU ambayo haikujua suala la EPA hadi lilipoibuliwa Bungeni; TAKUKURU ambayo haikujua wizi wa Deep Green Finance: TAKUKURU iliyoshindwa kushughulikia ufisadi katika ununuzi wa rada na ndege ya rais; TAKUKURU iliyoshindwa kuona ufisadi katika uuzwaji wa mgodi wa Kiwira; TAKUKURU inayoshindwa kuchunguza upotevu wa mabilioni ya pesa za Watanzania katika miradi michafu ya vigogo (orodha ni ndefu), ndiyo hii inayoona uchungu wa shilingi 50,000 za posho ya wabunge?
Hata kama posho hizo zina utata, watu wenye akili na uchungu na taifa wanaweza kuruhusu suala hili lifunike mjadala wa ufisadi wa Richmond? Huu ndiyo uwezo na upeo wa Ikulu na TAKUKURU kulinda watu wasiozidi wanne na Richmond yao kwa kunyamazisha na kutisha wanaohoji ufisadi huo?
Watu hawa wanajua kuwa ipo siku wataondoka Ikulu au TAKUKURU? Wanajua kuwa kuna maisha baada ya hila zao hizi za kisiasa au wanadhani watafia katika ofisi hizo ili tusiwahoji? Baada ya Ikulu kulinda na kusaidia watuhumiwa wengine wa Richmond kustaafu kwa heshima, inaona hii ndiyo njia mwafaka ya kuiondoa TAKUKURU katika matope ya Richmond? Hivi wanadhani kwamba hata kama wabunge wakiogopa wakanyamaza, wakaacha kuihoji serikali juu ya Richmond, vigogo hawa wanakuwa watumishi safi mbele ya umma na dhamiri zao wenyewe?
Mkakati huu wa Ikulu na TAKUKURU si uhuni mwingine uliovuka mipaka kwa serikali inayoongozwa na wale wale waliotuambia majuzi kuwa hawana nia ya kuwaziba midomo wabunge? Tusikilize kauli zao au tutazame matendo yao?
Hivi serikali inadhani watu pekee wenye akili wako Ikulu na TAKUKURU, kiasi cha kutupangia ajenda dhaifu ndani ya ajenda kuu, na kutarajia sisi tufuate upepo wao wa kisiasa na kucheza ngoma yao 'isiyokesha?'
Kama huu ndiyo mtiririko wetu wa kufikiri, viko wapi vipaumbele vya kitaifa? Ni haki tupotoshwe na propaganda za Ikulu na TAKUKURU, tuanze kuwajadili na kuwazomea wabunge ambao wamegundua janja hii ya Ikulu na TAKUKURU, wakawa jasiri kugoma na kutoa kauli thabiti?
Ni lini taifa hili litaacha kulea na kuenzi ukondoo, likatukuza ushujaa hata kama ni wa wachache wanaoweza kuwaambia watawala "hapana?"
Katika wakati ambapo taifa zima liko gizani kwa sababu ya maamuzi mabovu ya watawala hao hao, tuache kujadili athari za Richmond tujadili posho mbili za wabunge? Kama walikuwa na nia njema na suala hili si wangelitafutia nafasi yake baada ya kuturidhisha na utekelezaji wa maagizo ya Bunge kuhusu Richmond?
Mbona tunajua kuwa hata rais mwenyewe na mawaziri wake wanaposafiri mikoani na kwingine wanapewa takrima hizo hizo na wenyeji wao? Ni Ikulu na TAKUKURU ipi itamchunguza rais?
Ni haki Watanzania wanyimwe fursa ya kujua hatima ya Richmond kwa ajili ya kuridhisha matakwa ya Ikulu na TAKUKURU kabla wakosaji wa TAKUKURU hawajawajibishwa?
Tumefika mahali ambapo serikali inatukuza na kulinda vigogo na Richmond yao kuliko maisha ya Watanzania milioni 40?
Wala Pinda hakuhitaji kusisitiza maagizo ya Ikulu kwa TAKUKURU, kabla hajatueleza nani aliiagiza TAKUKURU kuisafisha Richmond. Tunachojua ni kwamba TAKUKURU ipo chini ya ofisi ya rais. Hivyo, Ikulu na TAKUKURU ni kitu kimoja. Pinda anaweza kutusaidia kujibu Ikulu, TAKUKURU na Richmond ni vitu vingapi?
Hivi Pinda anadhani tumesahau kauli yake kwamba suala la hatua za serikali dhidi ya mkurugenzi wa TAKUKURU liko mbele ya rais linafanyiwa kazi? Kumbe ndiyo kazi yenyewe hii? Na Pinda anadhani ameipa Ikulu sifa?
Je, vitisho hivi vya Ikulu na TAKUKURU kwa wabunge ndiyo tafsiri ya kauli ya Mbunge wa Monduli, Edward Lowassa, kwamba yeye na Rais Jakaya Kikwete wametoka mbali hawawezi kutenganishwa?
Au ndiyo tafsiri ya kauli ya Lowassa, muda mfupi kabla ya kujiuzulu uwaziri mkuu mwaka jana, alipowaonya wabunge akisema 'sote hapa ni wanasiasa, tukiamua kushughulikiana nani atabaki?'
Au ndiyo utekelezaji wa kauli ya Mkurugenzi wa TAKUKURU, Dk. Edward Hosea, alipobanwa na wabunge katika moja ya semina alizowaandalia katika hoteli ya Whitesands, Dar es Salaam, wakamhoji kwa nini hajawajibika kutokana na uzembe wa ofisi yake katika sakata la Richmond, naye akakasirika na kusema atawashughlikia wao kwanza?
Pinda alidhani akisema TAKUKURU imetumwa na Ikulu wabunge wote wangeogopa na kutakatifuza makosa ya watawala? Je, hii si dalili kwamba serikali inaficha udhaifu na uchafu wa Ikulu kwa kutumia TAKUKURU kuwatisha wanaohoji kilichopo nyuma ya pazia?
Na hapa ndipo tunapowageuzia kibao wabunge wenyewe. Tuliwaambia, tukawashauri mapema wakati serikali ilipoleta muswada wa kubadili Taasisi ya Kuzuia Rushwa (TAKURU) kuwa TAKUKURU; tukasema taasisi hii haiwezi kufanya kazi ya kudhibiti wala kuzuia rushwa kama itaendelea kuwa chini ya ofisi ya rais.
Tulijua kwamba ofisi ya rais nayo inahitaji kuchunguzwa na kudhibitiwa, na kuwa serikali haitaki kuiondoa ofisi hiyo chini ya rais ili kuwalinda ama rais mwenyewe, au wasaidizi wake au rafiki zake au jamaa zake iwapo watakumbwa na masuala yanayohitaji mkono wa TAKUKURU.
Tulipendekeza iundwe chini ya chombo kinachojitegemea ili kiweze kusaidia kumulika kote kote bila woga wala upendeleo. Lakini dhamira ya serikali ilipitishwa na wabunge wale wale waliojifanya wanakipenda sana chama chao (CCM) kuliko taifa.
Katika hili la sasa, wabunge hawa wanaopambana na TAKUKURU wanapaswa kujua kwamba wanapambana na nguvu nyingine nyuma yake. Wataweza kuishinda? Je, wananchi watabariki hila za Ikulu na TAKUKURU?
Je, wabunge wetu sasa wameanza kuelewa hekima yetu ya kuiondoa TAKUKURU ofisini kwa rais? Maana hekima ya kawaida inatujulisha kuwa si marais wote watakuwa waadilifu. Wabunge wanajua mchezo unaochezwa na watawala, maana baadhi yao walikuwamo katika kikao cha Halmashauri Kuu (NEC) ya CCM kilichomchachafya na kumtisha Sitta na wenzake.
Viongozi wale wale wa vikao vya NEC ndio hao hao wanaoituma TAKUKURU iwarudie kina Sitta kwa hila mpya. Si wamalize sula la Richmond kwanza tuone jeuri yao? Je, wabunge wataweza kuinyamazisha Ikulu na TAKUKURU?
Watawala wanadhani wabunge na wananchi hawajui walengwa wanaotafutwa na wanaolindwa katika sakata hili? Hivi Ikulu haiwezi kuwa imara bila kuwakumbatia mafisadi?
MAKALA hii inapatikana pia katika tovuti ya TanzaniaDaima
Friday, October 30, 2009
Wednesday, October 28, 2009
Sasa tumejua, tatizo ni rais
Wednesday, October 14, 2009
Tunayojivunia ndiyo haya?
Sunday, October 11, 2009
JK akianguka tena daktari wake atasemaje?
Thursday, October 01, 2009
Hotuba ya Mke wa Gordon Brown
Wednesday, September 30, 2009
Sunday, September 20, 2009
Salaam za Eid El Fitr 2009
Sunday, September 13, 2009
Rais Kikwete amefanikiwa kujidanganya

Friday, September 04, 2009
Zitto Kabwe ataweza?
Sunday, August 16, 2009
Saturday, August 08, 2009
Tunamsafisha Kikwete kwa majitaka?
Tuesday, August 04, 2009
Tujadili migogoro ya Sitta

Thursday, July 23, 2009
Your girlfriends at a birthday party
Wednesday, July 22, 2009
Migiro opens School of Journalism

Monday, July 20, 2009
Sunday, July 12, 2009
Ujumbe wa Obama kwa Afrika
Saturday, July 11, 2009
Obama anatazama nini?
Friday, July 10, 2009
Swali gumu kwa Obama
Obama na Papa Benedict XVI wakubali kutofautiana

Rais wa Marekani Barack Obama amemtembelea Papa Benedict XVI, na wawili hao wamekubaliana na kutofautiana katika masuala ya msingi. Wasome hapa. Na kwa mara ya kwanza baada ya muda mrefu, mke wa rais, Michelle Obama amevaa vazi linalofunika haswa mwili wake.
Thursday, July 09, 2009
Saturday, July 04, 2009
Mahakama ya Kadhi: Ahadi nzito iliyoshindikana
Sarah Palin abwaga manyanga

Sunday, June 28, 2009
Michael Jackson: Skendo Tupu

Saturday, June 27, 2009
Serikali inataka kulikoroga jeshi letu?

Serikali imeamua kulipaka jeshi letu matope ya ufisadi, kulifanya ngao ya ufisadi wa vigogo, huku ikisisitiza kwamba ni kwa maslahi na usalama wa taifa. Je, inajua madhara yake? Ni haki kulitumia jeshi letu kulinda matumbo machafu ya wanasiasa? Huu ndio mjadala wa Maswali Magumu wiki hii.
Wednesday, June 24, 2009
Ijue Nguvu ya Sikio lako la Kulia
Tuesday, June 23, 2009
Uingereza wapata Spika mpinzani
Sunday, June 21, 2009
Rostam Mbunge Bubu

Thursday, June 18, 2009
Hukumu muhimu kwa wanablogu: Kublogu na siri haviendani
Sunday, June 14, 2009
Saturday, June 13, 2009
Yajue manono ya Ronaldo
Sunday, June 07, 2009
Vijana CCM Bukoba acheni kujikomba
Wakilinganishwa na vijana waliowatangulia, vijana wa leo wana vipaumbele gani vilivyo bora? Na wakilinganishwa na wazee wa leo, vijana wa leo wanaonyesha matumaini gani ya kuwa na uzee mwema hapo baadaye?
Je, Tanzania yetu hii tukiikabidhi kwa vijana hawa tulionao, itakuwa salama zaidi kuliko ilivyo leo mikononi mwa wazee wanaong’ang’ania ujana? Je, wanaowabeza vijana wa Tanzania, wana haki ya kufanya hivyo? Au kuna sampuli ya vijana wanaosababisha bezo linalowaumiza vijana wote?
Je, Umoja wa Vijana wa CCM una haki tena ya kujiona wao ndio wawakilishi wa fikra, tabia na mwelekeo halisi wa vijana wa Tanzania? Je, vijana wa Tanzania, kwa ujumla wao, wanaonyesha jeuri, ujuzi, umakini, nguvu, upeo, wepesi, udadisi, moyo wa kujituma na wa harakati kuliko waliowatangulia?
Mfumo wetu wa elimu na malezi, umetulelea vijana wenye sifa hizo au umetufyatulia vibaraka na wapambe wa mfumo uliopo walio wepesi kunyanyaswa, kupuuzwa na kutumiwa kwa maslahi ya walio madarakani, hata kwa kuteketeza maslahi ya taifa la kesho?
Je, dhana ya taifa la kesho ipo kweli, au maisha yote yanakamilika na kumalizika leo tu? Kama kesho ipo, ni nani anabaki kuwa mlinzi wa hiyo kesho?
Nimejiuliza maswali haya na mengine baada ya kusikia kilichotokea Bukoba Mjini wiki hii, ambapo Umoja wa Vijana wa CCM, umetoa hundi ya shilingi milioni moja (1,000,000/-) kumlipia Rais Jakaya Kikwete kiasi anachohitaji kuchukulia fomu ya kugombea tena urais mwaka 2010.
Wamempa pia Mbunge wa Bukoba Mjini, Balozi Khamis Sued Kagasheki, hundi ya laki moja (100,000/-) ili aweze kulipia fomu ya kugombea ubunge kwa tiketi ya CCM mwaka 2010.
Najua kampeni zinazoendelea ndani ya CCM. Siwaonei wivu Rais Kikwete na Balozi Kagasheki. Naelewa pia kwamba vijana hao wametoa michango hiyo kama hamasa ya kisiasa. Ni kampeni za kuelekea Uchaguzi Mkuu 2010.
Lakini najiuliza, hizi ndizo siasa zinazowafaa watu wanaojiita vijana katika karne ya 21? Kwa staili hii, wao wanajifanya watu wa kuiga au wa kuigwa? Hii ndiyo sampuli ya vijana wa Bukoba? Wanaleta aibu au sifa kwa vijana wenzao kimkoa na kitaifa?
Hii dhana ya kumchangia pesa rais inatokana na nini? Ni kwamba Rais Kikwete ni mhitaji wa pesa kwa kiwango hicho cha kutegemea misaada ya kuchangiwa au kupewa? Je, vijana hawa wana fedha nyingi za kugawa hata kwa Rais Kikwete?
Je, vijana hawa wamejitosheleza au wana miradi mikubwa kiasi kwamba pesa hiyo inatokana na faida kubwa waliyopata, na sasa wameamua kutoa mchango kwa ‘maskini Kikwete na Kagasheki?’
Ni kweli kwamba katika bajeti yao ya mwaka huu pesa hiyo ilitengwa kwa ajili ya kununulia fomu ya Rais Kikwete mwaka ujao? Ni kweli Rais Kikwete alihitaji kuchangiwa milioni moja na kundi kama hili? Je, hii pesa ni ya vijana hao au wamepewa ili wafanyie mbwembwe na harakati za kisiasa?
Najua kinachofanyika hapa ni kampeni; ni propaganda; ni mbwembwe; ni kujitangaza. Lakini hii ndiyo staili ambayo inawafaa vijana wetu, tena baadhi yao wasomi? Je, siasa za namna hii zitatuendeleza?
Je, CCM Bukoba imeendelea, imeridhika na ina ziada ya pesa kiasi cha kutoa misaada kwa wengine wanaohitaji, nje ya mkoa, akiwamo rais?
Vijana hawa hawa ambao wamekuwa wanakinga bakuli kwa Mbunge wao, ambao baadhi yao wamekuwa wakitumika kumsifia mchana na kumshambulia usiku, leo wamepata wapi jeuri ya pesa ya kumsaidi yeye badala ya kukarabati majengo ya ofisi zao zilizochakaa na kuweka mikakati ya kuboresha vipato vya watendaji katika ofisi zao?
Balozi Kagasheki amekuwa akitumia fedha zake nyingi kufadhili miradi mbalimbali katika jimbo lake. Vijana hawa waliwahi kumchangia katika kufadhili mradi gani kwa ajili ya maendeleo ya wakazi wa Bukoba?
Jambo moja ni wazi. Hatuwezi kuwapangia matumizi ya pesa za chama. Lakini tunaweza kuwashauri. Kwa sehemu kubwa, matumizi kama haya yanaonyesha udhalili wa wahusika; na yanawafanya waonekane wanajikomba kwa maslahi finyu ya kisiasa.
Nisingehoji sana kama pesa hizi zingetolewa na jumuiya isiyo ya vijana. Wala nisingewasema sana kama zingekwenda kwa watu wanaozihitaji, ambao wanataka kugombea ubunge au urais lakini vipato vyao haviwawezeshi kupata viwango hivyo vya pesa.
Wapo wananchi wanataka kugombea ubunge, lakini wanatengwa na mfumo unaothamini pesa kuliko utu. Baadhi yao wangeweza kuwa wawakilishi wazuri tu, lakini kwa kuwa hawana pesa ya kununua fomu na kuhonga wakati wa kampeni, wanatupwa nje ya ulingo wa siasa.
Kama vijana hawa wangewatambua watu wa aina hii, wakawapa hamasa kwa kuwachangia pesa, tungeona wamefanya jambo la maana. Lakini pia, vijana ndio wangetarajiwa kukisaidia chama chao kuondoa taratibu kongwe na za kibaguzi zinazoleta matabaka kwenye chama chao na katika taifa kwa ujumla.
Badala ya kukaa tu na kuabudu mifumo hii, vijana wangekuwa wabunifu na jasiri zaidi kwa kuwashawishi wazee kuondokana na mifumo mikongwe ndani ya chama.
Zaidi ya hayo, vijana hawa ndio wangepaswa kukikosoa chama, kukipa changamoto ndani na nje ya vikao, kukitetemesha na kukitikisa ili kirejee katika misingi ya chama cha wakulima na wafanyakazi; chama cha mlalahoi, Mtanzania mlipa kodi; chama wa waadilifu na watu wenye uchungu na nchi hii.
Sifa wanazomwaga kwa viongozi walioshindwa kazi, ni dalili tosha kwamba vijana wenyewe wamezeeka kabla ya wakati wao; wamegeuka wachafuzi na wakorogaji wa siasa za Tanzania; wamekuwa waviziaji na wazengeaji wa vyeo vya kuteuliwa; wanajikomba na kujidhalilisha; wanatanguliza maslahi yao finyu.
Duniani kote, uhai na maendeleo ya taifa hutegemea zaidi vijana; si tu kwa misuli yao bali hasa kwa akili na ubunifu, ujasiri na moyo wa kuthubutu kubadilisha mazoea.
Lakini sehemu kubwa ya vijana wa Tanzania, hasa wenye nafasi katika mfumo wa utawala wan chi hii, wanashangilia mazoea ya muda mrefu, na yaliyochoka na kuchokwa hata na baadhi ya walioyaasisi. Kuna tatizo gani?
Tunapowaza kutengeneza sera za maendeleo yetu, tunalenga mustakabali wa taifa miaka 30 na zaidi ijayo. Hapa tunazungumzia kizazi kijacho – watoto na wajukuu wetu. Tunazungumzia urithi tutakaowaachia watoto tunaowazaa leo na watoto wao.
Hatuwazi kutafuna na kuteketeza kila kilichopo leo, kana kwamba tunawakomoa wale tuliowatangulia kuzaliwa. Uchungu na ugomvi wa baadhi yetu na watawala, tunapojadili uoza na ufisadi wao, unatokana na fikra hii kwamba walio madarakani na wapambe wao, wameendekeza dhana ya kukomoa kizazi kijacho.
Laiti vijana wa leo wangejua kuwa ni jukumu lao kuwazuia watawala na kudhibiti ukomoaji huu unaoendelea kulitafuna taifa lililojaliwa raslimali nyingi mno, lakini linasifika duniani kote kwa amani na utulivu katikati ya umaskini uliokithiri.
Wanaotusifu wana sababu zao. Si zetu. Sifa za watu wa nje hazileti chakula mezani kwetu. Hazilipi kodi ya nyumba; hazitujengei shule wala hazitulipii karo ya watoto wetu. Hazitibu wagonjwa wetu.
Lakini sifa hizo zinalegeza mioyo yetu, na zinawahakikishia wanaotusifu fursa ya kutumia raslimali zetu kuendeleza mataifa yao; kuwawekea hazina vijana na watoto wa mataifa yao kwa kutumia jasho la vijana na watoto wetu. Ni wajibu wetu, hasa vijana wa leo wa Tanzania, kusema, ‘hapana!’
Si sifa ya kujivunia kwa watawala wetu kumeza ndoani za mataifa makubwa, huku wakivikwa vilemba vya ukoka na kutunukiwa tuzo na shahada za bure ili waendelee kutengeneza na kuchonga mirija mirefu, mikubwa na imara zaidi ya kuhamishia utajiri wa nchi zetu kwa wakoloni wapya, wababe wa utandawazi.
Ni jukumu la vijana kuhakikisha kuwa ujana wao na wa watoto wao haunyonywi na vijana wa wakoloni weusi au weupe au wowote wale, kwa kisingizio chochote kile.
Tukubali, tukatae; kesho ni ya vijana. Lakini kesho hiyo hiyo inaanza leo, na inatengenezwa na leo yetu.
Bahati mbaya, sioni kama vijana wenyewe wanatambua hilo au wanahangaika kuitengeneza kesho hiyo, au kuwazuia waharibifu wa leo yetu inayoleta maangamizi ya kesho yao. Kama wapo hawatoshi.
Kwa sababu ya kasumba za muda mrefu na propaganda za kisiasa zilizodumaza uwezo wa wananchi kufikiri; kwa sababu ya mfumo wa elimu ya kunakiri na kukariri; wananchi wetu wengi, vijana wakiwamo, wamekuwa mateka wa mifumo ambayo wangepaswa kusimama kidete kuihoji, kuipinga na kuiangusha.
Sina ugomvi na utendaji wa Balozi Kagasheki katika jimbo lake. Ni mmoja wa wabunge wachache wanaotumia raslimali zao binafsi kuendeleza majimbo yao. Lakini hii siyo siasa tunayotaka kujenga. Si kazi ya mtu mmoja kuwajenga wananchi milioni mbili madaraja, madarasa, barabara, nyumba za kuishi, miradi ya maji na afya, kuwanunulia magari ya wagonjwa, na kadhalika.
Tunahitaji siasa endelevu, ambazo zinakiwezesha chama na serikali ya wakati huo kuweka mifumo ya utendaji kazi, hata kama mbunge mwenyewe hachaguliwi tena au anajiuzulu. CCM Bukoba Mjini wamekuwa wakimsaliti mna kumzunguka Kagasheki, wakijua upinzani mkuwa alio nao dhidi ya Chama cha Wananchi (CUF).
Kama kuna msaada walipaswa kumpa, si pesa; sila ki moja. Huu ni uhuni, ni matusi. Kagasheki nahitaji nguvu na umoja wa kichama, ushirikiano katika kujenga mikakati ya maendeleo na ushindani wa kistaarabu; mifumo endelevu ya kuleta maendeleo ya wana Bukoba.
Kama walitaka kusaidia, basi hiyo laki moja wangemchangia mwanachama mwingine anayetaka kuchuana na Kagasheki ndani ya chama, lakini ha uwezo wa kuipata. Tungewaita mashujaa, wanademokrasia wanaokua na vijana wa kutegemewa na taifa zima.
Kwa uapnde mwingine, tungewaona mashujaa kama miongoni mwao angejitokeza kiaja anayetaka kuchukua fomu kuchuana na Rais Kikwete katika kugombea urais mwaka kesho, kwa sababu sote tunajua kwamba katika miaka mitatu hii iliyopita, mambo yamemuwia magumu!
Tunajua ugumu wa kupambana na rais aliye madarakani. Si lazima umshinde, lakini ni vema kuandika historia kwamba vijana wa Tanzania wana uwezo kukataa kusifia kasoro na udhaifu wa wakubwa.
Wana CCM wenye akili, ambao hawaridhiki na utendaji wa serikali ya awamu ya nne, lakini hawana ujasiri wa kutosha kuwanyooshea wakubwa kidole, wananyamaza. Sawa ni waoga, lakini ni bora kuliko kujidhalilisha!
Naomba nieleweke. Vijana wote hawawezi, na hawapaswi kuwa na msimamo mmoja; au kuwa katika chama kimoja; au kuwa nje ya chama. Lakini wanaotaka kumsaidia rais au nchi yao, wanaweza kufanya hivyo ndani ya chama kwa kukipa changamoto na kukibadilisha ili kiendane na zama zao.
Wanaweza kufanya kazi nzuri tu bila kutumia kama mihuri ya maamuzi ya wakubwa. Wanaweza kuingiza nguvu mpya ya kiakili na kimwili katika chama, na kukipa mwelekeo mpya ulio imara.
Siasa za kutafuta maslahi kwa kujikomba na kumwaga sifa zisizostahili ni siasa dhalili zinazoweza kufanywa na wale tu ambao wanatambua kuwa nafsi zao hazina thamani, wala utu wao hauna nafasi, na ni kivuli tu, mbele ya nafsi za wakubwa.
Kuishi, kula na kufanikiwa kwao kunategemea fadhila, uteuzi na huruma ya wakubwa. Hizi si siasa za kufanywa na vijana. Na kwa hili, tuwaulize vijana hawa wa CCM Bukoba: ‘ipo wapi jeuri, ujuzi, umakini, nguvu, upeo, wepesi, udadisi wao kisiasa?’ Tukubaliane. Wametudhalilisha
Thursday, June 04, 2009
Obama awaahidi Waislamu 'mwanzo mpya'

Sunday, May 31, 2009
Thursday, May 28, 2009
Ferguson akiri kuzidiwa kete
Monday, May 25, 2009
Friday, May 22, 2009
Friday, May 01, 2009
Bibi harusi mfupi sana

Mtoto jiniasi kuliko wote

Thursday, April 30, 2009
Tuesday, April 28, 2009
Ni Messi au Ronaldo?
Friday, April 24, 2009
Mengi anamsaidia Rais Kikwete?
Wapo watu wanaombeza Mengi kwa tamko hili; na wapo wanaomuunga mkono. Wote hao, pamoja na Mengi, tutawajadili baadaye. Lakini kijumla ni kwamba, kwa maslahi yoyote yale, Mengi amethubutu. Je, unataka kuwajua 'Mapapa wa 'Mengi?' Hawa hapa. Hawa wamemnukuu lakini wakaogopa kutaja majina. Na yeye anasema kwa kauli yake hiyo anamsaidia Rais Kikwete kupambana na ufisadi. Ni kweli? Sehemu ya pili hii hapa.
Wednesday, April 22, 2009
Jacob Zuma ashinda urais Afrika Kusini
Monday, April 20, 2009
DECI, dini na siasa
Friday, April 17, 2009
Jogoo wa shamba kawika mjini London
Wednesday, April 15, 2009
Watoto wa Nyerere na Amini wakutanishwa
Sunday, April 05, 2009
Eti Malkia hakumbatiwi?
Saturday, April 04, 2009
Urithi wa siku 1200 za Kikwete Ikulu
Friday, April 03, 2009
Vituko vya kidiplomasia vya Berlusconi

Thursday, April 02, 2009
Maazimio ya kina Obama haya hapa
Wakubwa wa nchi 20 kubwa duniani wamemaliza mkutano wao jijini London na wamekubaliana misingi kadhaa katika kuinua na kumarisha uchumi. Hii hapa. Tazama na hapa. Na mtazame mwenyeji wao, Gordon Brown, akifunga mkutano huo na Rais Barack Obama akitoa majumuisho mbele ya waandishi wa habari.
Wednesday, April 01, 2009
Obama atua London

Matukio mengine: Obama, Gordon Brown na waandishi wa habari. Obama na 'Kwini.' Obama na vigogo wengine 19. Siasa za tabasamu za wake wa wakubwa (tazama picha hapo juu kushoto) na video kadhaa zinazoonyesha harakati za Michelle akiwa London - Cheki hapa na hapa. Brown akifungua mkutano. Baada ya mkutano Obama alikwenda Ufaransa, Ujerumani na nchi nyingine za Ulaya. Muone hapa akimudu jukwaa mbele ya umma Ufaransa.
Sunday, March 22, 2009
Buriani Jade Goody
Saturday, March 21, 2009
Rajoelina: Mimi ni rais
Papa Benedicto XVI na Kondomu
Lakini Papa ni kiongozi wa dini, na ujumbe wake unazingatia maadili yanayosimamiwa na madhehebu ya imani yake. Kama huo ndiyo msimamo wa kanisa lake, tulitarajia aseme nini? Ahubiri nini? Asiposema hayo aliyosema atakuwa Papa tena? Na kama kondomu haizuii kwa asilimia 100 Papa amekosea nini?
Thursday, March 19, 2009
Tuesday, March 17, 2009
Wananchi wachukua Ikulu Madagascar
Lucy Kibaki kashika hatamu au mpini?
Saturday, March 14, 2009
Uongozi unaoahirisha majukumu utafanikiwa?
Friday, March 13, 2009
Wapime watawala wetu kwa swali hili dogo
Monday, March 09, 2009
Watawala wetu mitumba ya kisiasa?
- Ansbert Ngurumo
- Nimechongwa na mambo haya: Falsafa, Fasihi, Muziki, Habari na Harakati. Sifuati mkumbo. Napenda kuhoji na kudadisi - hulka ya kifalsafa ya kuusaka ukweli - 'UKWELI ULIO UCHI.'







