Tunahitaji kujua kwa sababu hatujui; na hatuwezi kujua kama hatujui kwamba hatujui...Hatutajua chochote iwapo hatutahoji na kudadisi. Na kadiri tunavyojua, ndivyo tunavyogundua kwamba hatujui...
Thursday, April 30, 2009
Tuesday, April 28, 2009
Ni Messi au Ronaldo?
Wapenzi wa soka mnasemaje kuhusu kijana huyu Lionel Messi wa Barcelona? Kiwango chake kiko juu sana. Hebu mtazame hapa kwa dakika nne tu, halafu uamue kama wanaomlinganisha na Cristiano Ronaldo wa Manchester United wanamtendea haki.
Friday, April 24, 2009
Mengi anamsaidia Rais Kikwete?
Mwenyekiti Mtenadaji wa IPP, Reginald Mengi, amelipuka na kuwasha moto mpya dhidi ya mafisadi. Kama ilivyokuwa kwa Dk. Willibrord Slaa aliyetangaza orodha ya mafisadi kwa sifa, vyeo na majina yao Septemba mwaka juzi, Mengi naye amethubutu kutaja majina matano tu ya wale aliowaita mapapa wa ufisadi nchini. Ni wazi, wengine tuliwajua mapema, walishatajwa walishanong'onwa, wana tuhuma nzito lakini kwa sababu zinazojulikan kwa watawala, mafisadi hao hawashitakiki. Baadhi yao wako mahakamani wanashitakiwa kwa ufisadi.
Wapo watu wanaombeza Mengi kwa tamko hili; na wapo wanaomuunga mkono. Wote hao, pamoja na Mengi, tutawajadili baadaye. Lakini kijumla ni kwamba, kwa maslahi yoyote yale, Mengi amethubutu. Je, unataka kuwajua 'Mapapa wa 'Mengi?' Hawa hapa. Hawa wamemnukuu lakini wakaogopa kutaja majina. Na yeye anasema kwa kauli yake hiyo anamsaidia Rais Kikwete kupambana na ufisadi. Ni kweli? Sehemu ya pili hii hapa.
Wapo watu wanaombeza Mengi kwa tamko hili; na wapo wanaomuunga mkono. Wote hao, pamoja na Mengi, tutawajadili baadaye. Lakini kijumla ni kwamba, kwa maslahi yoyote yale, Mengi amethubutu. Je, unataka kuwajua 'Mapapa wa 'Mengi?' Hawa hapa. Hawa wamemnukuu lakini wakaogopa kutaja majina. Na yeye anasema kwa kauli yake hiyo anamsaidia Rais Kikwete kupambana na ufisadi. Ni kweli? Sehemu ya pili hii hapa.
Wednesday, April 22, 2009
Jacob Zuma ashinda urais Afrika Kusini
Afrika Kusini walipoingia katika uchaguzi wa rais na viongozi wengine wa kitaifa, kama kawaida, wananchi waligawanyika katika makundi, na walitoa maoni yao. Soma hapa. Baada ya kura kupigwa, chama tawala (ANC) kilipata ushindi mnono. Tazama Rais Mtarajiwa Jacob Zuma anavyoburudika na wapambe wake jukwaani kushangilia ushindi.
Monday, April 20, 2009
DECI, dini na siasa
Tathmini yangu fupi ni kwamba sakata la kampuni ya DECI inayoendesha upatu limechukua muda mrefu kwa kuwa wamiliki walimau kutumia dini kuhujumu wananchi maskini huku wakijificha katika kivuli cha siasa zetu. Ndiyo maana waliweza kusitawi kwa miaka mitatu bila kuguswa na vyombo vya usalama wa taifa. Walipata imani ya umma na ulinzi wa dola usio rasmi. Sasa wameshtukiwa, lakini tazama suala hili linavyojaa utata na kuchukua muda mrefu kutekelezwa. Ni dini na siasa ulingoni. Sijui wewe unasemaje.
Friday, April 17, 2009
Jogoo wa shamba kawika mjini London
Mama huyu mwanakijiji Susan Boyle amekuwa gumzo. Inawezekana wakati wewe utamtazama na kumsikiliza hapa utakuwa mtu wa milioni 17 ndani ya wiki moja. Chema kimejiuza; na jogoo wa shamba amewika mjini. Msome, msikilize; huyu hapa.
Wednesday, April 15, 2009
Watoto wa Nyerere na Amini wakutanishwa
Tanzania na Uganda zilipoingia vitani (1978-79) haikuwa vita ya kifamilia, lakini BBC imefanya jitihada za kuwakutanisha watoto wawili wa waliokuwa marais wa nchi hizo, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere na Iddi Amin Dada. Watoto wao, Madaraka na Jaffari wamekutana kijijini Butiama, na hizi hapa ndizo kauli zao. Kumbukumbu muhimu.
Sunday, April 05, 2009
Eti Malkia hakumbatiwi?
Michelle Obama alivunja mwiko akamkumbatia Malkia Elizabeth II, naye akamkumbatia. Wala hajakatika mikono. Ona hapa!
Saturday, April 04, 2009
Urithi wa siku 1200 za Kikwete Ikulu
Bado hajamaliza, lakini tayari Rais Jakaya Kikwete amekwangua siku 1202 akiwa Ikulu. Kwa kuwa dalili zinaonyesha ameshaanza kujiandalia ngwe ya pili, tujiulize: hizo alizomaliza zimewaachia Watanzania urithi gani? Tujadili.
Friday, April 03, 2009
Vituko vya kidiplomasia vya Berlusconi

Wapo viongozi wa nchi wanaofahamika kwa vituko vya kidiplomasia. Kwa Ulaya, nadhani Waziri wa Italia, Silvio Berlusconi, anaongoza. Mwaka 2005 aliiudhi serikali ya Finland kwa 'mizaha ya kitoto' aliyomfanyia rais Tarja Halonen. Mwaka mmoja baadaye aliingia kwenye mgogoro na serikali ya China baada ya kudai kwamba chini ya utawala wa Mao Zedong, Wachina walikuwa 'wanachemsha watoto wachanga.' Kuna wakati aliwahi kuangusha kichwa cha mimbari mbele ya Rais George Bush na waandishi wa habari. Aliwahi kutoa kauli tete juu ya rangi ya ngozi ya Barack Obama, mara alipochaguliwa Novemba mwaka 2008 kuwa rais wa Marekani. Mwaka jana alimchezea Kansela wa Ujerumani, Angela Merkel, mchezo ule ujulikanao kama 'hide-and-seek.' Hata juzi akiwa jijini London kwenye mkutano wa G20, Berlusconi alipayuka hadharani akimuita Rais Obama mara baada ya kupiga picha ya pamoja na Malikia wa Uingereza, Elizabeth II, jambo ambalo hata malkia mwenyewe anasemekana hakulipenda! Ikumbukwe kuwa huko nyuma aliwahi kujikuta kwenye mzozo na Wajerumani kwa utani wa KINAZI dhidi ya mbunge mmoja wa Ujerumani. Aliwahi pia kumsifia waziri Mkuu wa Denmark kuwa ni handsome kuliko viongozi wote wa Ulaya! Hata majuzi katika mkutano wa NATO alichelewesha ufunguzi wa mkutano huo baada ya kuganda kwenye simu nje ya ukumbi, huku mmoja wa wenyeji wa mkutano, Merkel, akimsubiri bila mafanikio. Mtazame hapa. Una kituko kingine cha Berlusconi au kigogo yeyote? Kwa Afrika ni kiongozi gani 'anasifika' kwa vituko vya kidiplomasia?
Thursday, April 02, 2009
Maazimio ya kina Obama haya hapa
Wakubwa wa nchi 20 kubwa duniani wamemaliza mkutano wao jijini London na wamekubaliana misingi kadhaa katika kuinua na kumarisha uchumi. Hii hapa. Tazama na hapa. Na mtazame mwenyeji wao, Gordon Brown, akifunga mkutano huo na Rais Barack Obama akitoa majumuisho mbele ya waandishi wa habari.
Wednesday, April 01, 2009
Obama atua London

Rais wa Marekani Barack Obama yupo London akiwa na mkewe Michelle kushiriki mkutano wa nchi 20 zenye nguvu zaidi kiuchumi. Huyu hapa akishuka kwenye ndege yake na kuelekea kwenye 'chopa' kwenda Ubalozi wa Marekani nchini Uingereza. Hizi hapa ndizo mbwembwe zinazoambatana na msafara wa 'kiranja wa marais' duniani (wapo katika picha ya pamoja chini kulia).
Matukio mengine: Obama, Gordon Brown na waandishi wa habari. Obama na 'Kwini.' Obama na vigogo wengine 19. Siasa za tabasamu za wake wa wakubwa (tazama picha hapo juu kushoto) na video kadhaa zinazoonyesha harakati za Michelle akiwa London - Cheki hapa na hapa. Brown akifungua mkutano. Baada ya mkutano Obama alikwenda Ufaransa, Ujerumani na nchi nyingine za Ulaya. Muone hapa akimudu jukwaa mbele ya umma Ufaransa.
Matukio mengine: Obama, Gordon Brown na waandishi wa habari. Obama na 'Kwini.' Obama na vigogo wengine 19. Siasa za tabasamu za wake wa wakubwa (tazama picha hapo juu kushoto) na video kadhaa zinazoonyesha harakati za Michelle akiwa London - Cheki hapa na hapa. Brown akifungua mkutano. Baada ya mkutano Obama alikwenda Ufaransa, Ujerumani na nchi nyingine za Ulaya. Muone hapa akimudu jukwaa mbele ya umma Ufaransa.
Sunday, March 22, 2009
Buriani Jade Goody
MSANII maarufu wa runinga nchini Uingereza, Jade Goody, aliyekuwa anasumbuliwa na Kansa, ambaye aliolewa (shukrani zake hapa) na kubatizwa pamoja na watoto wake wawili, ameaga dunia usiku wa kuamkia leo Jumapili 22, 03, 2009. Mwanamuziki Darren Hayes amemsindikiza Jade kwa kibao cha I miss you . Humjui Jade Goody? Maelezo haya yanaweza kukusaidia kumfahamu. Alijiandalia mazishi yake mwenywe, na alitaka yawe ya kifahari, iwe hafla ya kusherehekea maisha yake mafupi ya miaka 27, hata kama yatapambwa na machozi ya baadhi ya baadhi ya waombolezaji. Apumzike kwa amani!
Saturday, March 21, 2009
Rajoelina: Mimi ni rais
Madagascar ina kiongozi mpya Andry Rajoelina (34) ambaye ameapishwa Machi 21, 2009 baada ya kuiangusha serikali ya Marc Ravalomanana. Naona wamepuuza vitisho na kemeo la SADC na AU; na ingawa hata mabalozi wamesusa hafla ya kuapishwa kwake, habari ndiyo hiyo. Rajoelina anasema, 'nimeshakuwa rais.'
Papa Benedicto XVI na Kondomu
KAULI ya hivi majuzi ya Papa Benedicto XVI kupinga matumizi ya kondomu katika vita ya UKIMWI imezua mjadala mpya, huku wengine wakimlaani kwamba anakwamisha mafanikio ya jitihada za kupambana na maambukizi ya UKIMWI na kwamba hakupaswa kutoa kauli hiyo. Wengine wamemkosoa kwamba si kweli kwamba matumizi ya kondomu yanaongeza kasi ya maambukizi ya UKIMWI kwa sababu taarifa za kitafiti zinaonyesha umuhimu wa kondomu katika kuzuia maambukizi. Hata hivyo, taarifa hizo hizo zinadai kwamba kinga ya kutumia kondomu si ya asilimia 100.
Lakini Papa ni kiongozi wa dini, na ujumbe wake unazingatia maadili yanayosimamiwa na madhehebu ya imani yake. Kama huo ndiyo msimamo wa kanisa lake, tulitarajia aseme nini? Ahubiri nini? Asiposema hayo aliyosema atakuwa Papa tena? Na kama kondomu haizuii kwa asilimia 100 Papa amekosea nini?
Lakini Papa ni kiongozi wa dini, na ujumbe wake unazingatia maadili yanayosimamiwa na madhehebu ya imani yake. Kama huo ndiyo msimamo wa kanisa lake, tulitarajia aseme nini? Ahubiri nini? Asiposema hayo aliyosema atakuwa Papa tena? Na kama kondomu haizuii kwa asilimia 100 Papa amekosea nini?
Thursday, March 19, 2009
Tuesday, March 17, 2009
Wananchi wachukua Ikulu Madagascar
Ndo hivyo! Rais Marc Ravalomanana wa Madagascar ameondolewa madarakani. Alipewa muda aondke mwenyewe kwa hiari, akashindwa kusoma alama za nyakati. Sasa yametimia! Jeshi limeingilia kati, na aliyekuwa kiongozi wa upinzani, Andry Rajoelina (34) kaingia Ikulu. Ona hapa eti wanaondoa mapepo ya Ravalomanana Ikulu!
Lucy Kibaki kashika hatamu au mpini?
Ukisikia mke kushika hatamu, Mke wa Rais Mwai Kibaki wa Kenya amedhihirisha hilo. Hakika huyu ameshika zaidi ya hatamu - ameshika mpini; mumewe ameshika makali. Lakini si wapimane ubavu kimya kimya, katika faragha? Kwa nini wanamwaga mtama mbele ya kuku wengi? Ndiyo maana nasema wote wawili wamenichefua. Bofya hapa ucheke kwa furaha au hasira.
Saturday, March 14, 2009
Uongozi unaoahirisha majukumu utafanikiwa?
Waislamu wameibuka tena wanataka serikali itekeleze ahadi yake juu ya Mahakama ya Kadhi. Nilishawashauri, na nilisisitiza hivyo katika makala yangu mojawapo ya Novemba mwaka jana. Nasisitiza kuwa wasipowabana wakubwa ahadi hii nayo itayeyuka kama lilivyo suala la Mwafaka wa Zanzibar. Vyovyote itakavyokuwa, litawatesa wakubwa ifikapo 2010.
Subscribe to:
Posts (Atom)
- Ansbert Ngurumo
- Nimechongwa na mambo haya: Falsafa, Fasihi, Muziki, Habari na Harakati. Sifuati mkumbo. Napenda kuhoji na kudadisi - hulka ya kifalsafa ya kuusaka ukweli - 'UKWELI ULIO UCHI.'
