Monday, August 01, 2005

Utani Kwa Wachagga!

Mzee mmoja toka Machame (Bwana Oforo) ambaye alikuwa
mkali sana kwa binti yake aitwae Manka, anaamka
asubuhi na kutaarifiwa kwamba binti yake ana mimba!

Bwana Oforo: "Aisee we Manka, nakwenda kazini,
nikirudi leo ni lazima uniambie ni nani kafanya uchafu
huu" Anafoka na kuondoka kuelekea ofisini.

Mchana akapigiwa simu na Mama Manka na kuambiwa kwamba
yule jamaa aliyempa mimba bintiye yupo nyumbani
anamsubiri kwa mazungumzo!

Mzee akachukua panga lake na kulinoa kabisaaa kwa
ajili ya kwenda kumteketeza mwanaharamu huyo.

Kufika nyumbani mambo yanakuwa hivi:

Kijana aliyempa mimba binti: "Mmmh Mzee ni kweli mi
ndiye nimempa mimba binti yako, na kusema kweli sina
mpango wa kumuoa. Lakini akizaa mtoto wa kiume
nitakupa TShs 1 million na ghorofa Kariakoo kisha
nachukua mtoto. Akizaa mtoto wa kike nakupa TShs 1
million na duka Sinza! Lakini je mzee, ikitokea bahati
mbaya mimba hii ikaharibika itakuwaje? "
Mzee Oforo: "Aisee babaangu eeeh itabidi tu umpe mimba
nyingine, hakuna jinsi!"
My photo
Nimechongwa na mambo haya: Falsafa, Fasihi, Muziki, Habari na Harakati. Sifuati mkumbo. Napenda kuhoji na kudadisi - hulka ya kifalsafa ya kuusaka ukweli - 'UKWELI ULIO UCHI.'