Sunday, October 19, 2008

Wananchi wamechoka

'Fujo' za wananchi dhidi ya viongozi wao na watawala zina chanzo na maelezo. HII HAPA ni sababu mojawapo. Soma pia makala ya Maggid Mjengwa akinikosoa na kuniambia Rais hapigwi mawe. Usikose pia majibu yangu kwake, mwendelezo wa mjadala katika makala isemayo: Hatuvunji nyumba, tunabomoa mlango. Na wewe toa maoni yako.

Sunday, October 12, 2008

Mtawa na Obama


VIKONGWE wawili Wamarekani wenye miaka 106 ni miongoni mwa wapiga kura wa (Rais) Barack Obama. Wa kwanza ni Ann Nixon Cooper ambaye Obama alimtaja katika hotuba yake ya ushindi; na wa pili sista huyu (pichani kushoto) ambaye hajapiga kura tangu mwaka 1952, lakini sasa amesema amepiga kura, na amempigia Obama. SOMA HAPA.

Thursday, October 09, 2008

Obama na McCain wanatuhusu nini?

Urais wa Barack Obama au John McCain kwa Marekani unatuhusuje sisi tusio Wamarekani? SOMA HAPA ujue mambo yanayotuhusu wanayotaka kufanya.

Soma hapa uone mgombea mwenza wa McCain, Sarah Palin alivyoingizwa mjini na wasanii kwenye simu.

Wakati huo huo, kampeni zimepamba moto, na McCain amemfagilia Obama bila kutaka; akazomewa na mashabiki wake. Sikiliza hapa.

Sunday, October 05, 2008

Tunaondoaje ombwe la uongozi?

ZIPO njia nyingi. Napendekeza tuanze kwa kuwadhibiti waviziaji wa uongozi wa nchi. Pata maoni yangu hapa.
My photo
Nimechongwa na mambo haya: Falsafa, Fasihi, Muziki, Habari na Harakati. Sifuati mkumbo. Napenda kuhoji na kudadisi - hulka ya kifalsafa ya kuusaka ukweli - 'UKWELI ULIO UCHI.'