Friday, April 23, 2010

Uchaguzi Mkuu: Mdahalo wa wanasiasa Uingereza

Watazame, wasikilize na watathmini wanasiasa hawa wanaogombea ukubwa wakijieleza katika mdahalo wao wa pili. Ni David Cameron (Conservative), Gordon Brown (Labour) na Nick Clegg (Lib Dem).

Tuesday, April 20, 2010

Mourinho haishiwi hoja kwa waandishi

Wakati Inter Milan na Barcelona zikijiandaa kuchuana katika ngwe ya kwanza ya nusu fainali, Kocha wa Inter, Jose Mourinho, amezungumza na waandishi kwa kujiamini. Msome hapa.. Na baada ya kuifunga Barcelona, aliwasifu vijana wake na kuwaponda washindani, lakini akaonya kuwa safari ya kuelekea Madrid bado ndefu. Naye Rais wa Klabu, Massimo Moratti, aliwasifu Inter, akammwagia sifa kocha, akisema: "wanatisha."

Thursday, April 08, 2010

Mgeni mwingine


Wageni bado wapo. Huyu ninayezungumza naye ni Maria Drantenberg, raia wa Norway, ambaye alinitembelea ofisini kwangu (06.Aprili.2010) kujadili hali na maendeleo ya vyombo vya habari na demokrasia Tanzania.
My photo
Nimechongwa na mambo haya: Falsafa, Fasihi, Muziki, Habari na Harakati. Sifuati mkumbo. Napenda kuhoji na kudadisi - hulka ya kifalsafa ya kuusaka ukweli - 'UKWELI ULIO UCHI.'