Saturday, December 04, 2010

Elimu yetu kikwazo kwa Tanzania tuitakayo

ASASI binafsi inayoitwa UWEZO Tanzania, Mei mwaka (2010) huu ilifanya utafiti juu ya maendeleo ya elimu katika vijiji 1,140 kwenye wilaya 38, ikahoji watoto 42,033 wa shule za msingi, wenye umri kati ya miaka mitano (5) na 16, katika kaya 22,800. Matokeo ya utafiti huo, ambayo yalitangazwa rasmi Septemba 2010, kwa kifupi, yaliibua masuala yafuatayo:

1. Katika watoto watano wanaohitimu elimu elimu ya msingi (Darasa la Saba), mmoja anaweza hawezi kusoma Kiswahii cha darasa la pili.
2. Nusu ya watoto wanaohitimu Elimu ya Msingi (Darasa la Saba) hawawezi kusoma Kiingereza.
3. Katika watoto 10 wanaohitimu darasa la Saba, watatu hawawezi kufanya hesabu (hisabati) ya darasa la pili.
4. Asilimia 70 ya wanafunzi wa shule za msingi hawajui kusoma Kiswahili kwa ufasaha.
5. Hadi darasa la tatu, watoto saba kati ya 10 hawawezi kusoma Kiswahili cha msingi.
6. Watoto tisa kati ya 10 hawawezi kusoma Kiingereza cha msingi.
7. Watoto wanane kati ya 10 hawawezi kufanya hisabati za msingi.


Jambo la kukumbuka: Elimu ya Msingi ndiyo msingi wa maisha ya kila Mtanzania. Bila msingi huu, mtoto hawezi kusonga mbele kupata elimu ya sekondari au ya chuo kikuu. Hata asipoipata ya sekondari, hataweza kujiwezesha kwa lolote kwa sababu hatakuwa na stadi muhimu za kukabiliana na maisha yake pale alipo. Kumbuka kuwa Watanzania walio wengi wana elimu ya Darasa la Saba.

Maswali muhimu: Je, kwa kiwango hiki cha elimu, serikali inawatendea haki watoto wetu? Kwa elimu hii, tutaweza kujikomboa kutoka kwenye umaskini? Je, elimu hii itatuwezesha kushindana na kukabiliana na changamoto za kimataifa? Je, kwa viwango hivi, tutaipataje Tanzania tuitakayo? Tujadili.
My photo
Nimechongwa na mambo haya: Falsafa, Fasihi, Muziki, Habari na Harakati. Sifuati mkumbo. Napenda kuhoji na kudadisi - hulka ya kifalsafa ya kuusaka ukweli - 'UKWELI ULIO UCHI.'