Friday, July 09, 2010

Dk. Shein apeta

CCM Zanzibar wamepata mgombea urais. Matokeo ya kura za NEC Dodoma yanasema hivi: Shein 117: Bilal 54: Nahodha 33.

Hata hivyo, taarifa kutoka ndani ya vikao vya CCM zinasema Dk. Bilali alipata kura 119 kutoka wa wajumbe. Akafuatiwa na Dk. Shein (63) na Nahodha (22). Hayo ndiyo maajabu ya CCM, ma ndiyo maana Wazanzibari hawakosi kulalamikia kitendo cha rais wao kuchaguliwa Dodoma badala ya Zanzibar. Na hivi ndivyo Dk. Bilali alivyozibwa mdomo kwa kupewa nafasi asiyoitaka ya kuwa mgombea mwenza wa JK.

Wednesday, July 07, 2010

URAIS Z'BAR: Dk. Shein akamiwa


BAADHI ya wanaCCM Zanzibar waliopo Dodoma wametishia kumburuza mahakamani Dk. Mohammed Gharib Shein na kuzuia uchaguzi iwapo chama kitampitisha kugombea urais. Wengine walio Zanzibar wanaendelea kusambaza vipeperushi vinavyokihamasisha Chama cha Wananchi (CUF) kijiandae kuingia madarakani ikiwa Dk. Shein atapitishwa kugombea urais. Wanadai Shein si chaguo la Wazanzibari, bali la vigogo wa Bara na Rais Amani Karume. Na baadhi yao wananukuu Katiba ya Zanzibar ya mwaka 1984 kuthibitisha kwamba Dk. Shein "amepoteza sifa" ya kugombea urais kwa kuwa amejiandikisha kupiga kura Bara. Ama kweli wamemkamia.

Sunday, July 04, 2010

Mdahalo wa wagombea urais Zanzibar

Taasisi huru ya habari nchini, Vox Media Centre Ltd, kwa kushirikiana na kituo cha Televisheni cha Star Tv, jana Jumapili, Julai 4, 2010ilifanya mdahalo kwa wagombea urais wa Zanzibar kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), katika Hoteli ya Ocean View Hotel, saa 3.30 asubuhi hadi 7.00 mchana. Mdahalo huo, ambao ni wa kwanza katika historia ya siasa za Zanzibar, utarushwa na kituo cha Star Tv baadaye katika wakati utakaotangazwa baadaye mwanzoni mwa wiki hii. Wanahabari wengi za Zanzibar walishiriki, na kituo cha redio cha HITS FM kilirusha moja kwa moja matangazo ya mdahalo huo. Huu ni wa kwanza katika mlolongo wa midahalo ya kisiasa inayotarajiwa kufanyika mwaka huu kuelekea Oktoba 2010. Star Tv watarusha mdahalo huo Jumatano saa 4.30 - 5.30 usiku.
My photo
Nimechongwa na mambo haya: Falsafa, Fasihi, Muziki, Habari na Harakati. Sifuati mkumbo. Napenda kuhoji na kudadisi - hulka ya kifalsafa ya kuusaka ukweli - 'UKWELI ULIO UCHI.'