Saturday, December 04, 2010

Elimu yetu kikwazo kwa Tanzania tuitakayo

ASASI binafsi inayoitwa UWEZO Tanzania, Mei mwaka (2010) huu ilifanya utafiti juu ya maendeleo ya elimu katika vijiji 1,140 kwenye wilaya 38, ikahoji watoto 42,033 wa shule za msingi, wenye umri kati ya miaka mitano (5) na 16, katika kaya 22,800. Matokeo ya utafiti huo, ambayo yalitangazwa rasmi Septemba 2010, kwa kifupi, yaliibua masuala yafuatayo:

1. Katika watoto watano wanaohitimu elimu elimu ya msingi (Darasa la Saba), mmoja anaweza hawezi kusoma Kiswahii cha darasa la pili.
2. Nusu ya watoto wanaohitimu Elimu ya Msingi (Darasa la Saba) hawawezi kusoma Kiingereza.
3. Katika watoto 10 wanaohitimu darasa la Saba, watatu hawawezi kufanya hesabu (hisabati) ya darasa la pili.
4. Asilimia 70 ya wanafunzi wa shule za msingi hawajui kusoma Kiswahili kwa ufasaha.
5. Hadi darasa la tatu, watoto saba kati ya 10 hawawezi kusoma Kiswahili cha msingi.
6. Watoto tisa kati ya 10 hawawezi kusoma Kiingereza cha msingi.
7. Watoto wanane kati ya 10 hawawezi kufanya hisabati za msingi.


Jambo la kukumbuka: Elimu ya Msingi ndiyo msingi wa maisha ya kila Mtanzania. Bila msingi huu, mtoto hawezi kusonga mbele kupata elimu ya sekondari au ya chuo kikuu. Hata asipoipata ya sekondari, hataweza kujiwezesha kwa lolote kwa sababu hatakuwa na stadi muhimu za kukabiliana na maisha yake pale alipo. Kumbuka kuwa Watanzania walio wengi wana elimu ya Darasa la Saba.

Maswali muhimu: Je, kwa kiwango hiki cha elimu, serikali inawatendea haki watoto wetu? Kwa elimu hii, tutaweza kujikomboa kutoka kwenye umaskini? Je, elimu hii itatuwezesha kushindana na kukabiliana na changamoto za kimataifa? Je, kwa viwango hivi, tutaipataje Tanzania tuitakayo? Tujadili.

Thursday, November 18, 2010

Chadema wamkataa Kikwete hadharani

Chadema wamesisitiza hoja yao ya kukataa matokeo ya urais kwa sababu za uchakachuaji. Mdau mmoja, Bartholomew Mkinga, ameamua kufafanua uamuzi wa Chadema kumkataa rais, na kuendelea na shughuli za Bunge. Anasema:

"CHADEMA haijatamka kuwa haimtambui Kikwete kama Rais wa Tanzania, bali hawayatambui matokeo ya uchaguzi yaliyompa Kikwete mamlaka ya kuwa rais. Kwa tafsiri rahisi, ni Kikwete hana tofauti na marais wan chi nyingine wanaotumia mbinu mbalimbali kuupata urais bila ridhaa ya wananchi wanaowaongoza; amewekwa madarakani na tume ya uchaguzi, si wapiga kura.

CHADEMA haiongelei matokeo ya kura za ubunge kwa vile sheria inaruhusu kuhoji matokeo ya ubunge kwenye vyombo vya kisheria. Kwa hiyo, CHADEMA inategemea kuhoji matokeo ya kura za ubunge katika majimbo kadhaa. Kwa upande wa urais ni tofauti kwa vile sheria hairuhusu kuhoji matokeo ya urais mara tume ya uchaguzi ikishayatangaza. Kwa hiyo, jitihada pekee inayoweza kutumika ni ya kisiasa.

CHADEMA hawatahudhuria matukio yote mawili kama njia mojawapo ya kuonesha kutokuridhika na kile kilichofanywa na tume ya uchaguzi ya kuhujumu demokrasia."

Katika tukio la hivi karibuni, Alhamisi wiki hii, wabunge wa Chadema wamesusa hotuba ya Kikwete Bungeni. Mara tu alipoinuka na kuanza kuhutubia, wabunge wote, wakiongozwa na Kiongozi wa Upinzani Bungeni, Freeman Mbowe, wameondoka, wakimwacha Kikwete mdomo wazi. Kikwete amelazimika kuhutubia wabunge wa CCM, CUF, TLP na NCCR-Mageuzi.

Wednesday, November 03, 2010



Dk Slaa amesema kuwa matokeo ya kura za urais na ubunge yanayoendelea kutangazwana Tume ya Taifa ya Uchaguzi yamepikwa na Idara ya Usalama wa Taifa. Aliwaambia waandishi wa habari, makao makuu ya chama chake, kuwa Chadema kimefuatilia na kugundua kuwa takwimu za matokeo zinazotangazwa na Tume hazifanani na zile zilizo majimboni na kwenye kata, kutokana na idadi ya kura kutoka vituo vya kupigia kura. Alitoa mifano kadhaa, ukiwamo wa Geita ambako Chadema kilipata kura zaidi ya 22,000 za urais, lakini Tume ilitangaza kwamba kilipata kura 3,000.

Kwa sababu hiyo, Dk Slaa aliitaka Tume kusitisha mara moja utangazaji wa matokeo ya urais na kuandaa upya uchaguzi wa rais. Alimtaka pia Mkurugenzi wa Idara ya Usalama ajiuzulu kwa sababu amekipendelea chama kimoja badala ya kujali maslahi ya taifa.

Monday, November 01, 2010

Majimbo ya upinzani

Hadi sasa inasemekana upinzani umechukua majimbo haya. Matokeo yameshajulikana katika majimbo mengi. Lakini Tume haitangazi, hasa katika maeneo ambako CCM wameshindwa. Wanataka walale nazo, waingize masanduku mapya, waombe zihesabiwe upya, ili watangaze mtu wao kesho. Katika baadhi ya maeneo, vijana wameshaanza kudai matangazo ya matokeo yao kwa nguvu: Matangazo rasmi kwa majimbo yote yanaendelea kutolewa:

Wapinzani walioshinda hawa hapa

1. Halima James Mdee .... Kawe (Chadema)
2. Tundu Lissu .... Singida Mashariki (Chadema)
3. Mustapha Quorro Akonaay ... Mbulu (Chadema)
4. Israel Yohana ..... Karatu (Chadema)
5. John Mnyika ..... Ubungo (Chadema)
6. Silinde David ...... Mbozi Magharibi (Chadema)
7. Felix Mkosamali ..... Muhambwe (NCCR-Mageuzi)
8. Salvatory Naluyaga Machemuli ...Ukerewe (Chadema)
9. Agripina Z. Buyogela .... Kasulu Vijijini (NCCR-Mageuzi)
10. Ole Sambu ...... Arumeru Magharibi (Chadema)
11. Augustine Lyatonga Mrema ..... Vunjo (TLP)
12. Salum Barwani ...... Lindi (CUF)
13. Joseph Mbilinyi ....... Mbeya Mjini (Chadema)
14. Philemon Ndesamburo Kiwelu ....... Moshi Mjini (Chadema)
15. Dk Antony Mbasa ....... Biharamulo Magharibi (Chadema)
16. Machali Moses John ......Kasulu Mjini (NCCR-Mageuzi)
17. Joseph Selasini ...... Rombo (Chadema)
18. Hezekiah Wenje ....... Nyamagana (Chadema)
19. Peter Msigwa ....... Iringa Mjini (Chadema)
20. Freeman Mbowe ....... Hai (Chadema)
21. Vincent Nyerere ...... Musoma Mjini (Chadema)
22. Godbless Lema ....... Arusha Mjini (Chadema)
23. Zitto Kabwe ....... Kigoma Kaskazini (Chadema)
24. Hayness Samson ...... Ilemela (Chadema)
25. John Shibuda ........ Maswa Magharibi (Chadema)
26. Meshack Opulukwa ....... Meatu (Chadema)
27. Sylvester Kasulimbayi Mhoja ....... Maswa Mashariki (Chadema)
28. John Cheyo ......... Bariadi Mashariki (UDP)
29. Bungaro Said ........ Kilwa Kusini (CUF)
30. David Kafulila ....... Kigoma Kusini (NCCR-Mageuzi)


Mengine baadaye

Uchakachuaji wa kura waanza

Taarifa zilizopo zinasema katika vituo vingi, kura za urais anaongoza Dk Slaa, lakini wanatangaza ya udiwani na ubunge tu. Eti ya urais yanasubiri baadaye. Njama za kuchakachua, kumuongezea JK! TUnasubiri.

Habari zinasema JK na Yusuf Makamba wamekimbilia Mwanza kumnusuru Masha, Nyamagana. Pale Ilemela, Anthony Diallo, amekubali kushindwa, akasaini fomu ya matokeo. Anataka kumwaga damu?

Sunday, October 31, 2010

Dk Slaa apiga kura

Dk Willibrod Slaa ameshapiga kura nyumbani kwake, Karatu; na sasa yuko njiani kuelekea Dar es Salaam kusubiri matokeo.







Hapa chini watazame Maalim Seif na Jakaya Kikwete wakipiga kura zao pia.



Hivi ndivyo Dk Slaa alivyofunga kampeni Mbeya




Picha ya kuchora inayomwonyesha pamoja Baba wa Taifa, Hayati Mwalimu Julius Nyerere na Dk Willibrod Slaa, iliyochorwa na Kasambara Joseph na Salim Ahamed. Dk Slaa alikabidhiwa picha hiyo katika mkutano wake wa kufunga kampeni uliofanyika kwenye Uwanja wa Ruanda Nzovwe jijini Mbeya, jana 31/10/2010



Pichani, Goodluck Haule, aliyekuwa mwanachama wa CCM, akimkabidhi Dk Slaa moja ya mavazi ya CCM baada ya kukihama na kujiunga na Chadema jana mjini Mbeya.



Wafuasi na wanachama wa CHADEMA wakiwa wamebeba bango lenye ujumbe wakati wa mkutano wa kufunga kampeni za Dk Willibrod Slaa uliofanyika kwenye Uwanja wa Ruandanzovwe jijini Mbeya 30/10/2010

Monday, October 25, 2010

Dk Slaa awa kivutio Zanzibar



Mgombea wa Chadema Dk Willibrod Slaa, akihutubia mkutano wa kampeni uliofanyika katika viwanja vya Garagaza,vilivypo Mtoni, Unguja, Zanzibar. (Picha na Emmanuel Herman)

Mapokezi ya Dk Slaa jimboni Kawe





Friday, October 22, 2010

Slaa nyumbani kwa Lowassa



Hana kawaida y akupokea kadi za wana CCM wanaohamia Chadema, lakini naona hapa ameamua kuvunja mwiko. Katika picha hii, Dk Slaa amesimama na Amani Mollel ambaye ni mgombea ubunge wa Monduli kupitia Chadema, wakizichambua kadi za wana CCM 46 wa Monduli waliojiunga na Chadema kwenye mkutano wa kampeni uliofanyika kwenye Uwanja wa Bomani Polisi, Monduli mjini, mkoani Arusha.




Dk Willibrod Slaa akimpongeza mmoja wa kati ya vijana 46 wa kimasai wa Jimbo la Monduli waliojiunga na chama hicho wakitikea CCM, kwenye mkutano wa kampeni uliofanyika mjini Monduli, mkoani Arusha




Dk Willibrod Slaa akiwahutubia wakazi wa Monduli mjini kwenye mkutano wa kampeni uliofanyika leo Ijumaa asubuhi kwenye Uwanja wa Bomani Polisi mjini humo mkoani Arusha

Dk Slaa 'afanya kufuru' Mwanza



Hii ni sehemu tu ya umati wa wananchi wa Mwanza mjini waliofurika katika uwanja wa Magomeni, Kirumba, kumsikiliza Dk Willibrod Slaa juzi Jumatano jioni.

Monday, October 18, 2010

Slaa katika picha Bukoba - Kahama



Dk. Willibrod Slaa akihutubia maelfu ya wakazi wa mji wa Kahama mjini Kahama, mkoani Shinyanga jana jioni.




Dk. Willibrod Slaa akisalimiana na baadhi ya watawa waliohudhuria mkutano wa kampeni zake kwenya Uwanja wa Sabasaba mjini Nzega jana asubuhi.




Sehemu ya wakazi wa Nzega wakiagana na Dk. Willibrod Slaa mara baada ya mkutano wa kampeni kwenye Uwanja wa Sabasaba.





Dk. Willibrod Slaa akihutubia katika mkutano wake wa kampeni kwenye Uwanja wa Sabasaba mjini Nzega, Tabora.





Dk. Willibrod Slaa akihutubia wananchi wa kijiji cha Mganza, Jimbo la Chato.






Akinana mama wakazi wa mji wa Bukoba nao hawakuachwa nyuma katika mkutano wa kampeni za Dk Slaa mjini Bukoba. Katika picha hii wanalea watoto wao, huku wakimsikiliza Dk. Willibrod Slaa katika mkutano wa kampeni uliofanyika kwenye Uwanja wa Mashujaa (UHURU).







Dk. Willibrod Slaa akihutubia wakazi wa mji wa Bukoba na vitongoji vyake katika mkutano wa kampeni kwenye Uwanja wa Uhuru.

Monday, October 11, 2010

Slaa: Sitaki Urais wa Damu


Akiwa mwishoni mwa ziara yake mkoani Kigoma, Dk Slaa aliwataka wananchi kujihadhari na CCM na Kikwete kuhusu kauli za kuwamga damu zinazosambazwa na wanapropaganda wa CCM. Hii ndiyo kauli yake:

“Mimi sitaki kwenda Ikulu kwa kumwaga damu ya Mtanzania yeyote. Sijatamka hata siku moja kumwaga damu. Nataka uchaguzi wa amani na utulivu. Katika mikutano yangu zaidi ya 400 niliyofanya sasa, nimehimiza watu wangu kuzingatia amani…Nyie mkipigwa shavu hili geuza jingine, msiwe chanzo cha vurugu.

“Amani haihubiriwi, bali inajengwa kama vile Chadema inavyowajenga Watanzania katika sera zake. Tunaposema kutoa elimu bure, afya bure na kuboresha makazi ni kwa faida ya Watanzania wote, hatutaki kujenga matabaka….Lakini CCM imekuwa inapeleka vijana wake kwenye makambi kujiandaa kufanya fujo…Lakini wajue kuwa amani itakuwapo kama haki itatendeka.

Thursday, October 07, 2010

Dk Slaa akiwa Tunduma, Namanyere


Dk. Willibrod Slaa, akihutubia wakazi wa mji mdogo wa Namanyere katika Jimbo la Nkasi Kaskazini mkoani Rukwa, akiwa njiani kuelekea Mpanda nyumbani kwa Waziri Mkuu Mizengo Pinda. Kwa mujibu wa Evarist Shija, mmoja wa maofisa wa serikali waliohudhuria, JK alipofika hapa alipata karibu nusu ya umati huu, licha ya kuwasomba kwa mabasi na malori kutoka sehemu za mbali, tena baada ya matangazo ya nguvu.


Dk. Willibrod Slaa akihutubia maelfu ya wakazi waa mji wa Tunduma, katika mkutano wake wa kampeni, kwenye Uwanja wa Shule ya Msingi Tunduma


Sehemu ya maelfu ya wakazi wa mji wa Tunduma, wakipunga mikono kumpokea Dk. Willibrod Slaa, alipowasili kwenye Uwanja wa Shule ya Msingi Tunduma.

Monday, October 04, 2010

Dk Slaa akiwa Singida na Mbeya



Sehemu ya umati wa wakazi wa mji wa Mbalizi mkoani Mbeya, wakiwa na mabango yenye ujumbe mbalimbali, wakati wa mkutano wa Dk. Willibrod Slaa.



Mgombea ubunge katika jimbo la Mbeya Mjini kupitia CHADEMA, Joseph Mbilinyi (Mr Sugu), akiwatumbuiza wananchi wa mji wa Mbalizi, wakati wa mkutano wa Dk. Willbrod Slaa.



Dk. Willibrod Slaa akihutubia maelfu ya wakazi wa mji wa Mbalizi mkoani Mbeya, kwenye Uwanja wa Stendi ya Mabasi.



Mkuu wa wilaya ya Mbarali, Kanali Mstaafu Cosmas Kayombo (aliyeketi kulia), akisikiliza mkutano wa kampeni wa Dk. Willibrod Slaa katika eneo la Chimala mkoani Mbeya.



Mgombea ubunge Jimbo la Iringa kwa tiketi ya Chadema, Mchungaji Peter Msigwa akijinadi kwa wananchi mbele ya Dk Slaa.

Wednesday, September 29, 2010

Dk Slaa azungumzia mambo makuu matatu

Viti Maalumu

Kwanza amezungumzia suala la Viti Maalumu kupitia CHADEMA, akaweka wazi kilichoazimiwa na Kamati Kuu ya chama. Majina 105 kati ya 147 ya walioomba kuteuliwa viti maalumu, yamepitishwa; na sasa yatapelekwa Tume ya Uchaguzi kama sheria inavyodai. Walioteuliwa hawakutajwa majina kwa waandishi. Mfumo wa uteuzi ulizingatia vigezo sita (6) vilivyoainishwa na mtaalamu aliyeteuliwa na chama hicho ili kuifanya kazi hiyo, Dk. Kitila Mkumbo. Vigezo hivyo ni 1. Kiwango cha Elimu. 2. Uzoefu wa kazi ya kisiasa. 3. Uzoefu wa uongozi nje ya siasa. 4. Kugombea Jimbo. 5. Mchango wa mgombea katika chama na kampeni zinazoendelea. 6. Umri wa mtu katika chama. Kila kipengele kilikuwa na vigezo vidogo vidogo kama vinne, vyenye alama tofauti. Na kwa mujibu wa Dk Slaa na Kitila, viti hivyo vimetawanywa nchi nzima, kwa kuzingatia vigezo hivyo hivyo. Akahitimisha kwa kusema: "Ingawa kuna usemi kwamba siasa ni mchezo mbayan, kwa Chadema, siasa ni sayansi na unachezwa kisayansi." Alitumia pia fursa hiyo kusisitiza kuwa Chadema kimeweka wagombea 185 ambao ni ziaidi ya asilimia 75 ya wagombea ubunge nchi nzima; na kwamba idadi hiyo kinatarajia kuvuna wabunge wa kutosha, na kiko tayari kuunda serikali.

Usalama wa Taifa

Dk. Slaa alitumia fursa hiyo kutamka kwamba ana taarifa za kikachero kuwa Rais Kikwete ameagiza wana usalama wa taifa wasambae nchi nzima kuhujumu uchaguzi. Akasisitiza kwamba, "kwa sura ya sasa, Kikwete ameshashindwa...na amani ya nchi ikivurugika, Kikwete ndiye atabeba lawama na laana.." Alisisitiza pia kuhusu waraka uliosambazwa nchi nzima ukiwataka wakuu wa mikoa, wakuu wa wilaya na wakurugenzi wa halmashauri nchi nzima kufanya kila wawezalo kulazimisha ushindi wa CCM. Akasema hujuma hii inaweza kusababisha umwagaji damu, na kwamba asingependa itokee.

Utafiti na vitisho vya Synovate

"Tunasubiri kusikia Synovate wamefungua kesi. Kama hawajaenda, waende sasa. Wasipofanya hivyo tutawaharibia credibility yao hapa nchini na kimataifa. Chadema tunapofanya kitu chetu huwa haturudi nyuma. Hatuna woga. Gazeti lililoshitakiwa nalo lisiwe na woga." Baada ya hapo alionyesha vielelezo vya utafiti uliofanywa na Synovate, ambao katika kipengele GPO 6 liliulizwa swali: "Kama ucahguzi ungefanyika leo, nani ungempigia kura ya urais?" ambalo Synovate walikanusha kwamba halikuwamo katika utafiti wao, wakidai wanataka kuufanya baadaye kabla ya uchaguzi mkuu. Ukweli ni kuwa walifanya utafiti lakini CCM iliingiza 'mkono' wake baada ya kubaini kuwa matokeo hayo yalikuwa yanaonyesha Kikwete yuko nyuma ya Dk Slaa.

Tahadhari ya Mbowe

Freeman Mbowe alitoa tahadhari kwa Rais Kikwete, Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi, na Msajili wa Vyama vya Siasa, akisema wamepewa mamlaka ya umma, ambayo wakiyatumia vizuri wanaweza kulipeleka taifa kwenye amani, na wakifanya makosa wanalitumbukiza kwenye ghasia. Akasema kinatokea sasa, CCM wameshindwa siasa za majukwaani, na watatu hawa wako katika mikakati michafu ya kuvuruga uchaguzi. Akasema kama wanatakua kuugeuza uchaguzi wa uchakachuaji, hapatatosha! Aliwaomba Watanzania kuwa tayari kulinda maamuzi yao, kura zao. Akasisitiza: "Tunaomba Watanzania na jumuiya ya kimataifa mtuelewe..."

Thursday, September 23, 2010

DK. Slaa akiwa Kilimanjaro



Dk. Slaa nyumbani kwa Mbowe

Akiwa katika Jimbo la Hai, mkoani Kilimanjaro, Dk Willibrod Slaa alifanya mikutano 12 kwa siku moja. Kesho yake akafanya mikutano katika majimbo ya Rombo na Vunjo. Akahitimisha kampeni za awali mkoani humo kwa kufanya kampeni katika majimbo ya Moshi Vijijini, Moshi Mjini, Same Mashariki na Same Magharibi.

Alichokifanya mkoani Kilimanjaro kimeelezwa vema na wale waliosema “ameiteka Moshi” kwa maandamano ya watembea kwa miguu, waendesha baiskeli, pikipiki na magari; huku yakisindikizwa na helikopta katika maeneo ya Moshi Mjini. Umati wa wakazi wa Moshi, uliandamana na kusimamisha shughuli zote za kijamii na kibiashara kwa zaidi ya saa nne – kuanzia saa 8 alasiri hadi saa 12 jioni.

Ujumbe kutoka kwa Dk Slaa:

Watanzania wameshakubali kufanya mabadiliko makubwa. Rais Jakaya Kikwete ajiandae kuaga Ikulu, astaafu baada ya mika mitano ambayo haikuleta matumaini yaliyotarajiwa. Serikali isitumie mabavu kuumiza wananchi wanaotaka mabadiliko. Isimwage damu kwa ajili ya maslahi binafsi ya wanaotafuta madaraka au wanaong’ang’ania madaraka.
Rais Kikwete asiviingize vyombo vya ulinzi katika dhuluma inayoweza kusababisha damu ya Watanzania kumwagika kwa ajili ya madaraka ya wachache.

Ujumbe kutoka kwa Freeman Mbowe:

Hatuwezi kuwa na serikali inayoongozwa kwa nguvu za giza badala ya nguvu za Mungu; rais anayelindwa na majini badala ya vyombo ya ulinzi na usalama. Rais Kikwete ajitokeze, akanushe kuhusika na majini ya Sheikh Yahya Hussein, ambayo aliahidiwa kutumiwa yamlinde ili asianguke tena hadharani.

Katika picha hii, Mbowe anawaongoza wananchi wa Moshi Mjini kuzomea CCM kwa kilio huku wamejishika vichwa katika uwanja wa Mashujaa.

Saturday, September 18, 2010

Kampeni ya Dk. Slaa: Mpya Mpya Katika Picha



Mchumba wa Dk. Slaa, Josephine, akisalimia wananchi wa Karatu mkutanoni, juzi Alhamisi.



Dk. Slaa hatumii shangingi. Hiki ndicho kipanya anachotumia katika ziara zake za kampeni. Katika picha hii, wananchi wa Arusha Mjini wanasukuma kipanya hicho kuondoka viwanja vya mkutano kuelekea hotelini jana Jumamosi jioni.




Jina la shabiki huyu wa Dk. Slaa halikupatikana mara moja. Ni mkazi wa Arusha Mjini.




Dk. Willibrod Slaa, akimnadi mgombea wa ubunge katika jimbo la Karatu kupitia chama hicho, ambaye anatarajiwa kuwa mrithi wake wa ubunge jimboni humo, Mchungaji Israel Natse, wakati wa mkutano wa hadhara wa kampeni, uliofanyika kwenye Uwanja wa Bwawani mjini Karatu jana Ijumaa



Dk. Willibrod Slaa, akizungumza na Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Shinyanga, Daudi Siasi, mara baada ya kuhutubia mkutano wa kampeni zake kwenye Uwanja wa Sabasaba mjini Bariadi juzi Alhamisi.



Bendera za mashabiki Musoma Mjini: Dk. Slaa ni chaguo la vyama vyote



Wananchi Musoma: Dk Slaa ni Taa Mpya

Red Brigade wa Chadema Musoma Mjini



Red Brigade Musoma Mjini

Sunday, September 12, 2010

Hii ndiyo Bunda ya Dk. Slaa



Leo tuko Bunda. Acha picha hizi ziseme zenyewe. Maelezo mengine baadaye. Itoshe tu kusema kwamba miongoni mwa maelfu ya wana Bunda waliofurika kumsikiliza Dk. Slaa katika viwanja vya Sabasaba ni Mkuu wa Wilaya hiyo, Francis Isack. Alikaa jukwaa moja na Dk. Slaa, naye alimsifu kwa ukomavu wa kisiasa, lakini akamuonya kwamba kama alikuwa amekwenda pale kwa nia tofauti, atazame umma, apime nguvu yake na apeleke taarifa za kile anachosikia na kuona. Alimsimamisha DC huyo akawasalimia wananchi kwa kunyosha mikono juu.

Dk. Slaa acharuka Mwanza



Dk Willibrod Slaa amecharuka mkoani Mwanza. Akiwa katika majimbo ya Geita, Buchosa na Nyamagana, mgombea huyo ametoa changamoto kali kwa CCM, hasa mgombea urais Jakaya Kikwete ambaye Dk. Slaa alisema ni "saizi yangu." Halafu akatumia fusa hiyo kumshughulikia, akisema rais huyo wa awamu ya nne hana mpango mkakati wala visheni ya kuwakomboa Watanzania. Badala yake, Kikwete amekuwa akitekeleza maagizo yake (Dk Slaa) katika kipindi cha miaka minne iliyopita, hasa kwa kudai anapigana na ufisadi (ulioibuliwa na Dk. Slaa). Hata katika tukio la juzi la Kikwete kumchukulia hatua Meneja wa kiwanda cha Turiani, Morogoro, Dk. Slaa alisema hatua ya Kikwete ilitokana na msisimko wa siasa za uchaguzi, hasa baada ya Dk Slaa kutembelea Turiani, wiki mbili zilizopita, na kutoa kauli kwamba atashughulikia matatizo yao katika siku 100 za kwanza za utawala wake.

Vile vile, alisema Rais Kikwete amevunja rekodi ya kudanganywa kuliko marais wote duniani katika miaka mitano iliyopita. Alisema mwaka mwaka 2007, JK alifungua mradi hewa wa maji huko Pwaga, Dodoma; mwaka 2009 Rais Kikwete aliletewa Ikulu mkurugenzi wa halmashauri isiyohusika na kukabidhiwa gari la wagonjwa; na alizindua hoteli moja ya kitalii mkoani Arusha, kesho yake ikavunjwa uzio na TANROADS, na mwaka huu alisaini kwa mbwembwe sheria iliyochomekwa vipengele ambavyo havikujadiliwa Bungeni; na kwamba hata baada ya matukio yote hayo, hakuna mtu aliyewajibishwa.

Mwaka huu, siku alipozindua kampeni za CCM mkoani Mwanza, JK aliwaeleza wananchi kwa mbwembwe, kuwa Mbunge wa Nyamagana, Lawrence Masha, alikuwa amepita bila kupingwa; jambo ambalo Dk. Slaa alisema si kweli kwani mgombea wa Chadema alikuwa ameweka pingamizi, ambalo hatimaye limemrejesha ulingoni. “Ama JK alidanganywa na Masha au alijidanganya mwenyewe au hakuwa makini…Kikwete si makini. Awaombe radhi wananchi wa Nyamagana kwa kuwadanganya.”

Alisema Kikwete amekuwa rais wa majaribio, na kwamba miaka mitano inatosha. "Imetosha, Kikwete aende akapumzike, muda wake umekwisha, miaka mitano inamtosha. “Hatuwezi kwa miaka mitano kuendelea kuwa na rais mtalii, asiyejua matatizo ya wananchi wake, anayetetea maslahi ya wawekezaji badala ya wananchi, asiye na visheni,” alisema.Dk Slaa alidai hata mipango mkakati kama MKURABITA, MKUKUTA na hata MINI-Tiger, hata na barabara anazojivunia JK kujenga ni za awamu ya tatu ya Rais Mstaafu Benjamin Mkapa, si zalo la awamu ya nne.

Akiwa jijini Mwanza, alisisitiza juu ya umuhimu wa viwanda katika kujenga uchumi, ajira na ujira bora; akasema CCM iliua viwanda na makampuni ya umma zaidi ya 450 yaliyoanzishwa na Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere, na hivyo kuua ajira na uchumi wa taifa. Alisema Chadema kinadhamiria kuanzisha viwanda vinavyotegemea mazao ya kilimo na mifugo, ili kuimarisha uchumi wa watu maskini, kwani raslimali zipo. Kilichokosekana, hadi sasa, ni ubunifu kwa upande wa watawala. Alisisitiza pia sera za elimu, afya, na makazi bora wa mujibu wa ilani ya Chadema.

Baada ya mkutano alisindikizwakwa maandamano na umati wa watu wazima na vijana, wakisukuma gari alilopanda kutoka uwanja wa Mirongo hadi Hoteli ya Nyumbani - umbali kwa kilometa zipatazo 5. Polisi walijitahidi kuwadhibiti wananchi hao, ikawa kazi bure. Hakukuwa na fujo yoyote. Walikuwa wakiimba, "rais, rais, Slaa; tumechoka mafisadi..." huku baadhi yao wakiwa na mabango yenye maandishi kuwa, "hatukubebwa na magari, tumekuja ejnyewe."

Friday, September 10, 2010

Dk. Slaa akemea majini ya Sheikh Yahya Hussein


Dk. Willibrod Slaa amemkemea mnajimu Sheikh Yahya Hussein (pichani) aliyeahidi kumpa Rais Jakaya Kikwete 'ulinzi wa majini,' ili kukabiliana na nguvu za giza zinazomwandama na kumwangusha majukwaani. Akihutubia mkutano wa hadhara katika mji wa Katoro, jimbo la Busanda, Mwanza, Dk. Slaa alisema "nchi haiwezi kuongozwa na uchawi. Haiongozwi na imani za watu, kila mtu ana imani yake, lakini tusifike mahali tukaongoza nchi kwa uchawi."

Alimtaka Rais Jakaya Kikwete kumkemea Sheikh Yahya kwa kauli hiyo iliyotolewa juzi Dar es Salaam, la sivyo wananchi wataamini mnajimu huyo anatumiwa na CCM kuleta hofu katika jamii. Aliwakumbusha wananchi kuwa mwanzoni mwa mwaka huu, Sheikh Yahya alisema mtu yeyote atakayegombea urais na Kikwete, atakufa. Dk. Slaa alisema: "Sisi wengine ni majabali, hatuogopi."

Thursday, September 09, 2010

Nukuu ya Leo kutoka kwa Dk. Slaa



"Simamia, Dhibiti, Wajibisha."
Hii ni kauli nzito iliyotolewa na mgombea urais kupitia Chadema, Dk. Willibrod Slaa, akisisitiza umuhimu wa uongozi unaowajibika na kuwajibisha, ili kuokoa raslimali za taifa na kuzielekeza katika huduma za jamii. Akasema anahitajika kiongozi anayeweza kufanya mambo hayo matatu, ili kuwezesha serikali kuokoa pesa na kuziingiza katika kulipia elimu na afya. Alitoa kauli hii mjini Ngudu, Mwanza, katika mkutano wake wa tano leo, mara baada ya kuwaeleza wananchi kuhusu sera za afya na elimu, kwamba zitalipiwa na serikali, na kwamba vyanzo vya mapato ya kulipia huduma hizo vipo, na kwamba serikali ya JK inashindwa kuyatekeleza hayo kwa sababu inaishi katika anasa. Meneo mengine aliyotembelea leo ni Itinge, Mwandoya, Hungumalwa na Mwamashimba.

Alizungumzia umuhimu wa serikali kufumua mikataba yote mibaya, hasa ya madini, inayopoteza mabilioni ya shilingi kila siku, ili kumpunguzia Mtanzania mateso yanayosababisha na uongozi usiojali wananchi. Amekuwa akisema kila mahali kuwa serikali ya sasa inakumbatia wawekezaji, inatelekeza wananchi.

Dk Slaa pia alizungumzia pia suala la mishahara ya wafanyakazi, akisema iwapo ataingia madarakani, ataiboresha kwa kufanya kima cha hini kiwe Sh 315,000; huku akiwaongezea marupurupu ma maslahi ya nyongeza katika huduma za ujenzi wa makazi bora na bima za afya. Huku akiwakumbusha hongo iliyotolewa na JK mwezi uliopita kwa kuwaingizia wafanyakazi nyongeza katika mishahara, kinyume cha bajeti iliyopitishwa na Bunge, Dk. Slaa alisema hawataiona nyongeza hiyo baada ya uchaguzi kwa kuwa si rasmi. Alisema kwamba katika majibu ya Msajili wa Vyama vya Siasa kwa Chadema kuhusu pingamizi walilomwekea JK wakidai ameongeza mishahara kinyemela, hakuna mshahara wowote ulioongezwa rasmi, hivyo msajili akakosa kigezo cha kisheria cha kumtia JK hatiani. Lakini nyongeza hiyo ilikuwapo. Aliwakumbusha kuwa JK alikataa kura za wafanyakazi; akasema yeye (Slaa) anazitaka. Kuhusu pesa hizo zilizoongezwa kinyemera, alimalizia kwa nukuu nyingine muhimu, akiilekeza kwa wafanyakazi:
"Zimeingizwa sasa, baada ya uchaguzi hamzioni. Mlizoingiziwa...mmeliwa."
My photo
Nimechongwa na mambo haya: Falsafa, Fasihi, Muziki, Habari na Harakati. Sifuati mkumbo. Napenda kuhoji na kudadisi - hulka ya kifalsafa ya kuusaka ukweli - 'UKWELI ULIO UCHI.'