Friday, December 28, 2007

Matokeo ya Uchaguzi Kenya

Fuatilia matokeo ya Uchaguzi Mkuu wa Kenya 2007 hapa. Inaeleka wenzetu wameamua kufanya 'mapinduzi ya awali ya uongozi.' Hadi sasa Raila Odinga wa ODM anaongoza; Mwai Kibaki wa PNU anafuata nyuma. Kalonzo Musyoka wa ODM-Kenya yuko mbali sana. Muujiza alioutarajia haujatokea! Umebaki kanisani! KANU kimeanza kupotea katika historia ya utawala wa Kenya. Endelea. Linganisha na hii pia.

Monday, December 24, 2007

Krismasi Njema


Napenda kuwatakia Krismasi Njema! Krismasi ni tukio lenye maana mbalimbali kwa watu mbalimbali. Kwa wengine ni 'kumbukumbu' ya kiroho ya kuzaliwa kwa Yesu Kristo zaidi ya miaka 2007 iliyopita. Kwa wengine ni tukio kubwa lililoigawa historia katika ngwe mbili - Kabla ya Kristo na Baada ya Kristo. Kwa wengine (hasa Ulaya Magharibi) ni wakati wa kumaliza mwaka, kujipongeza na kujiandaa kwa mwaka mwingine; ni kipindi cha manunuzi na matanuzi. Kwa wengine halina maana kabisa, lakini wanajikuta wakiungana na wenzao wanaosherehekea Krismasi. Kwa wote hao, nasema Heri ya Krismasi na Mwaka Mpya 2008.

Wednesday, December 19, 2007

CHADEMA na CCM: nani mwizi wa sera?

Vyama vya siasa vinaposhutumiana kwa kuibiana sera maana yake nini? Je, kati ya CHADEMA na CCM, ni kipi kimedhihirika 'kuiba' sera za mwenzake? Kuna mifano hai? Inaaminika? Tutafakari.

Sunday, November 25, 2007

Tusiogope, Mapinduzi Yanawezekana


Nina hoja mbili. Kwanza, tuwe na rais wa kukaa mdarakani miaka mitano badala ya miaka kumi. Pili, tukubali kwamba maendeleo tunayotaka kuyafanya hayawezekani kama hatutakubali kuanza sasa kufanya mapinduzi. Wengine wana shaka, na wengine wanadhani haiwezekani. Lakini kama iliwezekana kwa Warumi, (mtazame Kaizari Julius pichani na utafakari yaliyomkuta) itashindikanaje kwa Watanzania? Na je, kushuka kwa umaarufu wa Kikwete kwaweza kuwa ishara mojawapo ya mwanzo mpya? Au ndiyo wanaanza kujifunza Afrika Kusini na Kenya, kujitambua na kugundua makosa?Tujadiliane.

Wednesday, November 07, 2007

Kuna ukweli gani katika hili?

Ujumbe huu unazunguka katika barua pepe za watu. Ulipofika kwangu nikaamua niuweke hapa tuujadili wazi wazi. Unasema hivi:

"Je tutafika? ...tuhuma zote za ufisadi zinazoikabili BoT, je unawajua walioajiriwa kusimamia uchumi wa nchi yetu na kutuletea mafanikio? Pokea taarifa ya wateule hawa. Ndani ya mtungi wa BoT walioqualify kuajiriwa kwa sifa na vigezo vinavyotambulika na BoT ni pamoja na hawa wafuatao:-

1. Pamella Lowassa,
2. Filbert Frederick Sumaye,
3. Zalia Kawawa,
4. Harieth Lumbanga,
5. Salama Ally Mwinyi,
6. Rachael Muganda,
7. Sylvia Omari Mahita,
8. Justina James Mungai,
9. Kenneth John Nchimbi,
10. Blassia Blassius William Mkapa,
11. Violeth Phillemon Luhanjo,
12. Liku Irene Katte Kamba,
13. Thomas Mongella,
14. Jabir Abdallah Kigoda etc.

Hapa nani atamwajibisha Dalali alas Balali? Je KAPUKU MWENDE(a.k.a KAYUMBA) ATAAJIRIWA KWELI HAPO? Hawa ni wale wenye uhusiano wa moja kwa moja na wazito wa nchi, wapo wengine ambao ni ndugu wa karibu au kabila moja na waheshimiwa. Ni vigumu kuamini kuwa hii ni bahati mbaya (mere coincidence). Mungu Ibariki Tanzania, Mungu Ibariki Afrika."

Tuesday, November 06, 2007

Mkaribisheni Peter Nyanje

Mkaribisheni Peter Nyanje, mhariri wa habari wa gazeti la Tanzania Daima katika ulimwengu wa blogu. Ameingia na kuahidi makubwa; na anatualika "tujadili hoja nzito." Tunaamini ataitumia blogu yake kuwaletea wasomaji kile wanachokikosa katika gazeti lake, yaani kile kilicho muhimu kinachobaki na kukosa nafasi katika habari za kawaida za kila siku. Blogu yake hii hapa. Mtembeleeni.

Kikwete mfa maji?


Usimshangae Rais Jakaya Kikwete. Huu ni mkakati wake. Wakati mawaziri wametoka mikoani majuzi kulaani kauli za wapinzani kwamba ni uzushi, yeye amesema wapinzani wasipuuzwe. Na baada ya kuona wananchi wanapuuza hoja za utetezi wa CCM na kukumbatia za wakosoaji kuhusu masuala ya madini, sasa rais anataka kuunda kamati ya madini itakayowashirikisha hata wakosoaji wake hao hao. Je, anataka kuwaziba mdomo wanaoikosoa serikali? Na tayari ameahidi kuwapa hela ya kutosha na ziara nje ya nchi kwa kazi hiyo. Ni hongo? Anataka kumaliza nguvu za upinzani kiujanja ujajanja? Au ndiko kutapatapa kwa mfa maji?

Sunday, October 28, 2007

Taarifa hizi zinatisha

Sasa tumeanza kuelewa kwa nini serikali inajikanyaga kuhusu tuhuma za ufisadi zilizoibuliwa na wapinzani. Taarifa mpya mpya zinaonyesha jinsi Benki Kuu ya Tanzania (BoT) ilivyotumika kuibia pesa kwa ajili ya Uchaguzi Mkuu wa 2005 ili mgombea urais wa CCM ashinde kwa kishindo. Binafsi naamini kwamba, kwa mazingira yaliyokuwapo, mgombea wa CCM angeshinda hata bila ya kununua kura. Soma mjadala hapa.

Friday, October 26, 2007

Habari Corporation yafungua tovuti


Kampuni ya Habari Corporation, inayomilikiwa na Mbunge wa Igunga na Mhazini wa CCM, Rostam Azizi (pichani kushoto), imefungua tovuti ya magazeti yake. Magazeti hayo yaliyowahi kutamba kwa uchambuzi mahiri na makini katika miaka ya 90 na kabla ya Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2005, yanapatikana hapa. Siku hizi inaitwa New Habari Corporation - yenye mmiliki mpya, sera mpya mikakati mipya na uongozi mpya.

Friday, October 19, 2007

Satan's benefit in our deeds

A man woke up early in order to have his morning
devotion (prayer) in the Lord’s house (church). He
got dressed, set on his way to the Lord’s house (church).
On his way to the church, the man fell and his clothes
got dirty. He got up, brushed himself off, and headed home.

At home, he changed his clothes, and was, again,
on his way to the Lord’s house. On his way to the
church, he fell again and at the same spot! He,
again, got up, brushed himself off and headed
home. At home he, once again, changed his
clothes and was on his way to the Lord’s house (church).

On his way to the house of God (church), he
met a man holding a lamp. He asked the man of
his identity and the man replied, "I saw you
fall twice on your way to the house of God (church),
so I brought a lamp so I can light your way.
The first man thanked him profusely and the two
were on their way to the house of God (church).
Once at the house of God (church), the first man
asked the man with the lamp to come in and
pray with him. The second man refused. The
first man asked him a couple more times and,
again, the answer was the same. The first man
asked him why he did not wish to come in and pray.

The man replied, "I am Satan". The man was shocked
at this reply. Satan went on to explain, "I saw you on
your way to the house of God (Church) and it was I
who made you fall. When you went home, cleaned
yourself and went back on your way to the house of God
(church), God forgave all of your sins. I made you fall
a second time, and even that did not encourage you to
stay home, but rather, you went back on your way to Church.
Because of that, God forgave all the sins of the people of
your household. I was afraid if I made you fall one more
time, then God will forgive the sins of the people of your village,
so I made sure that you reached the house of God (Church) safely.
" So do not let Satan benefit from his actions.

Do not put off the good you intended to do, as you never
know how much reward you might receive from the hardships
you encounter while trying to achieve that good. For your
righteousness can save your family and nation at large. Do
this and see the victory of the Lord.

Note: It was forwarded to me by a friend. I thought it might make a good reading for visitors of this blog. Stay blessed!

Sunday, October 14, 2007

Huyu ni Mwalimu wangu


Mama huyu ni mmoja wa walimu wangu. Anaitwa Prof. Susan Miller. Cheo chake ni MBA Academic Director, katika Chuo Kikuu cha Hull. Mpiga picha alinikamata nikiwa nasisitiza jambo - ona mikono, utadhani nasali vile! Teh! teh! teh! Picha hii ilipigwa Alhamisi wiki hii mara baada ya mlo wa jioni ulioandaliwa na Hull University Business School kwa ajili ya wanafunzi wote wa MBA chuoni hapo. Uwongo mbaya, kazi anaiweza.

Friday, October 12, 2007

Kikwete anasaidiwa na Ze Comedy?


Kauli ya Rais Jakaya Kikwete kuhusu vigogo wanaotuhumiwa kwa ufisadi (akiwamo yeye) haina 'mashiko.' Ukichanganya kauli yake, ya Kingunge Ngombale-Mwiru, na ya Jaji Joseph Warioba, utaona kwamba hapa kuna kutapatapa kwingi. Nashangaa magazeti yameandika JK ajibu mapigo. Nimesoma kwa makini, lakini sikuona hata pigo moja alilojibu. Hata waliosema ametoa majibu mazito wamemkweza bila sababu. Sikuyaona. Kama waliomtangulia kutoa kauli, analenga lakini ameshindwa kuwachanganya wananchi. Lakini kwa kuwa yeye alipewa muda mrefu kusoma alama za nyakati, na kwa kuwa yeye ndiye mkuu wao, wananchi walitarajia kauli pevu zaidi kutoka kwake. Haijapatikana.
Nadhani wapinzani wamemjibu vema. Ametonesha vidonda. Na bado yataibuka mengine tu. Rais ameibua maswali magumu. Nami bado ninaye; namtafakari. Katika hili, siko peke yangu. Tazama mchambuzi mwingine alivyomfanyizia Kikwete. Sasa nasikia wasanii wa Ze Comedy wameanza kuigiza tuhuma za vigogo, huku wakiwatetea watuhumiwa na kumsakama Dk. Slaa. Niko mbali na nyumbani. Wanaojua walete habari kamili. Inawezekana CCM imeamua kuwekeza katika Ze Comedy kuwapumbaza Watanzania, kuwatetea mafisadi?

Saturday, September 29, 2007

Warioba amekuwaje?


Sielewi Jaji Joseph Sinde Warioba amekuwaje. Kiongozi mstaafu, mwanasheria mstaafu na mtu aliyewahi kuongoza tume ya rushwa anaposema 'tuhuma hizi si mpya,' anataka kusema alitarajia kuona mpya zipi? Au alitaka hizi za zamani ziachwe tu? Simwelewi. Namshangaa pia anapoona kwamba kujadili rushwa ya wakubwa si muhimu kwa maendeleo ya nchi. Zaidi nipale anapopata shida kuelewa kwanini rais na rais mstaafu wanatuhumiwa. Nadhani angepaswa kuwashangaa wao na kujiuliza: "kwanini watuhumiwe? Kwanini wao na si wengine?" Badala yake, anawatetea kana kwamba anatoa 'hukumu kuwasafisha.' Bado simwelewi. Hivi hajui kwamba Tanzania itakuwapo bila yeye wala Jakaya Kikwete au Benjamin Mkapa?

Wednesday, September 19, 2007

Wonders of Mathematics

Bofya hapa uone maajabu ya HESABU - The Wonders of Mathematics. Nimetumiwa na rafiki yangu.

Kingunge ang'atuke


Pamoja na mambo mengine, natoa wito. Mheshimiwa Kingunge Ngombale-Mwiru ang'atuke. Badala ya kushauri vijana wake wajiheshimu n akutimiza wajibu wao, anafanya kazi ya mganga wa jadi kwenye masuala mazito! Naona Mpayukaji tayari ameniunga mkono.

Monday, September 17, 2007

Salva Rweyemamu ateuliwa mkurugenzi Ikulu


Salva Rweyemamu (pichani), aliyekuwa mkurugenzi wa Habari Corporation, ameteuliwa na Rais Jakaya Kikwete kuwa Mkurugenzi wa Kitengo cha Mawasiliano Ikulu. Anaziba nafasi iliyoachwa wazi na Balozi Peter Kallaghe aliyepelekwa Canada. Mwingine anayeonekana pichani kulia ni Dk. Gideon Shoo. Picha: Issa Michuzi

Dansi la Tanzania latesa majuu


The Ngoma Africa Band inayoongozwa na Ebrahima Makunja, a.k.a Ras Ebby Makunja "Bwana Kichwa Ngumu" imepata mashabiki wa kutisha jijini Frankfurt, Ujerumani. Msemakweli kaniandikia na kusema maelfu ya watu wa matabaka na mataifa mbalimbali jana usiku "walijikuta wanapelekwa mchaka mchaka na mlindimbo wa muziki huo Bongo Dance made in Tanzania... Nyimbo zao pia zinatesa katika redio mbalimbali Ulaya, Africa, Marekani na Canada...Unaweza kuwasikilza online hapa www.myspace.com/thengomaafrica"

Sunday, September 16, 2007

Hawa ndio wala nchi?


Hili ndilo linaitwa sasa kundi la wala nchi. Gazeti la Serikali, Habari Leo Jumapili, tarehe 16. Septemba 2007, limemnukuu Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Dk. Willibord Slaa, akiwataja 11 bora wanaodaiwa kushiriki katika ulaji na uuzaji nchi kwa namna moja au nyingine, kutokana na nyadhifa zao za kisiasa, kitaaluma au kwa sababu ya uwakala au ukaribu wao na wenye madaraka. Waliotajwa ni:
1. Rais Jakaya Kikwete

2. Rais Mstaafu Benjamin Mkapa

3. Waziri Mkuu Edward Lowassa

4. Waziri wa Nishati na Madini Nazir Karamagi

5. Waziri wa Miundombinu Andrew Chenge

6. Waziri wa Viwanda na Biashara Basil Mramba

7. Gavana wa Benki Kuu (BoT) Daudi Balali

8. Katibu Mkuu Wizara ya Fedha Gray Mgonja

9. Katibu Mkuu Wizara ya Maji Patrick Rutabanzibwa

10. Mbunge wa Musoma Vijijini Nimrod Mkono
11. Mbunge wa Igunga Rostam Aziz (pichani juu).
. Tuhuma zao kamili hizi hapa.
Je, unajua kuwa Mwalimu Nyerere alisema CCM sasa inatumia pesa za bangi kupata viongozi?

MAISHA: Enjoy the jokes

Someone sent me these 2 jokes, and I thought my readers would enjoy them.


A young man went to his father one day to tell him that he wanted to get married. His father was happy for him. He asked his son who the girl was and he told him that it was Samantha, a girl from the neighborhood. With a sad face, the old man said to his son, "I'm sorry to say this son but I have to, the girl you want to marry is your sister, but please don't tell your mother". The young man again brought 3 more names to his father but ended up frustrated because the response was still the same. So he decided to go to his mother. "Mama I want to get married but I can't marry any of the girls that I love because dad said they are my sisters and I must not tell you". His mother said to him with a smile, "Don't worry my son, you can marry any of those girls. You are not his son anyway, but please don't tell him".

The mathematics behind our life span.

God created the dog and said: "Sit all day by the door of your house and bark at anyone Who comes in or walks past. For this, I will give you a life Span of twenty years." The dog said: "That's a long time to be barking. Howabout only ten years and I'll give you back the otherten?" So God agreed.

God then created the monkey and said: "Entertain people, do tricks, and make them laugh. For this, I'llgive you a twenty-year life span."The monkey said: "Monkey tricks for twenty years?That's a pretty long time to perform. How aboutI give you back ten like the Dog did?" And God agreed.

God then created the cow and said: "You must go intothe field with the farmer all day long and suffer under the sun, have calves and give milk to support the farmer's family. For this, I will give you a lifespan of sixty years." The cow said: "That's kind of a tough life you wantme to live for sixty years. How about twenty and I'llgive back the other forty?" And God agreed again.

God created man and said: "Eat, sleep, play, marry and enjoy your life. For this, I'll give you twenty years." But man said: "Only twenty years? Could you possibly give me my twenty,the forty the cow gave back, the ten the monkey gave back, and the ten the dog gaveback; that makes eighty, okay?" "Okay," said God, "You asked for it."

So that is why for our first twenty years we eat,sleep, play and enjoy ourselves. For the next forty years we slave in the sun to support our family. For the next ten years we do monkey tricks to entertain the grandchildren. And for the last ten years we sit on the front porchand bark at everyone. Life has now been explained to you.

Saturday, September 15, 2007

Pole Mheshimiwa Mudhihir


Mbunge wa Mchinga (CCM), Mudhihir Mohammed Mudhihir akipokewa kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere Dar es Salaam, Ijumaa septemba 14. 2007, akitokea Lindi alikopata ajali ya gari. Kulia ni Mkuu wa Mkoa wa Lindi, Saidi Mecky Sadick. Picha kutoka Daily News.

Ajali haina kinga. Yaliyompata Mudhihir yanaweza kumpata mtu yeyote. Zaidi ya hayo yanawapa abiria wengi katika ajali za barabarani na angani kila siku. La msingi, tumshukuru Mungu kwamba Mudhihir yuko hai. Tumpe pole na kumwombea apone haraka.

Hapa ilikuwa zamu yangu


Huyo aliyeketi kwenye kiti ni Profesa Guy Berger, mkuu wa kitivo cha uandishi wa habari katika Chuo Kikuu cha Rhodes. Ndiye alikuwa mwenyekiti wa mdahalo wetu. Ukutani ni picha kutoka kwenye Power Point presentation niliyokuwa natoa mimi. Huyo aliyesimama mbele kulia, ndiye mimi.
NETucation walinihoji kidogo na kutoa stori yao kwa Youtube.
Baadaye, AllAfrica walitoa stori yangu iliyoandikwa na Rebecca Wanjiku wa Kenya. BIZCOMMUNITY.com nao wakaitumia kwa headline tofauti.
David Musoke wa Uganda hakubaki nyuma. Sarah Bel wa APC alipendezwa na hoja yangu kuhusu haja ya kupeleka intaneti vijijini. Hii ndiyo stori yake. Mail&Guardian waliandika stori hii na kukosea jina langu.

Wajumbe wakitoka ukumbini baada ya kutusikiliza tukitoa mada zetu. Alianza Ndesanjo Macha, akafuatia Daudi Were, baadaye mimi. Tazama ratiba.

Wednesday, September 12, 2007

Mwanablogu mpya wa kike Mtanzania


Furaha Thonya, mwandishi wa kike wa kujitegemea wa magazeti ya ThisDay na Kulikoni, amejiunga na jamii ya wanablogu. Msome hapa. Pichani ni Ndesanjo Macha, Ansbert Ngurumo, Furaha Thonya na Philemon Msangi (Bob Sankofa) Jumapili 9. Septemba 2007, nje ya ukumbi wa mikutano.

Tuesday, September 11, 2007

Mtazame Ndesanjo akitoa mhadhara


Hii ilikuwa tarehe 9.9.2007 katika Ukumbi wa Barrat, Chuo Kikuu cha Rhodes, Afrika Kusini. Ndesanjo Macha (pichani kushoto) alikuwa anatoa hotuba ya ufunguzi wa mdahalo kuhusu kublogu katika kongamano lijulikanalo kama Digital Citizen Indaba, lililofanyika kwa siku moja kama sehemu ya kongamano mama la Highway Africa, 10-12, Septemba 2007. Kongamano hili hujadili matumizi ya ubunifu katika vyombo vya kisasa vya habari. Hii ilikuwa mara ya 11 kwa kongamano hilo.

Monday, September 10, 2007

Wameandika hivi juu yetu


Tukiwa Grahamstown, tulitumia vema fursa tuliyopata kuzungumza na Waafrika wenzetu katika midahalo,. mijadala na kongamano. Mara ya kwanza ilikuwa katika Digital Citizen Indaba, Jumapili asubuhi, ambapo mimi, Ndesanjo na mwandishi wa Kenya Daudi Were tulijadili mada ya fractured identities. Mimi nilizama katika kueleza umuhimu wa kublogu wa Kiswahili. Baadaye Mpiga Bob Sankofa alitoa mhadhara kwa nini anablogu kwa kutumia picha. Tumetoa ujumbe. Umefika. Baadhi ya waandishi waliokuwapo wameandika hivi juu yetu. Mwingine huyu hapa. Pia usikose stori hii. Kumbe hata wapiga picha hupendeza wakipigwa picha. Muone BOB SANKOFA akihojiwa na mapaparazi kama yeye. Pichani, kutoka kushoto ni Daudi Were kutoka Kenya, mimi na Ndesanjo Macha wakati wa maswali na majibu. Huyu hapa ni Mwandishi kutoka Zambia, Brenda Zulu, anatutwanga swali. Tazama na picha hii ya Nokia. Hapa Ndesanjo alikamatwa vizuri akisisitiza jambo.

Hii nayo kali

Zamani Shirika letu la Ndege (Air Tanzania Corporation), kwa sababu ya kutokuwa na huduma inayoaminika, liitaniwa na wabongo, likaitwa Any Time Cancellation (ATC). Wanigeria nao sasa wameibuka na mpya kuhusu 'TANESCO' yao. Kwa sababu ya mgawo wa umeme na matatizo yasiyoisha, mamlaka yao ya umeme iitwayo Nigerian Electric Power Authority (NEPA), imekuwa ikitaniwa na kuitwa Never Expect Power Always (NEPA).

Ili kukabiliana na tatizo la umeme, serikali imeifanyia mabadiliko ya kimfumo, kiutawala na kiuendeshaji, ikaundwa kampuni iitwayo
Power Holding Company of Nigeria (PHCN). Matatizo ya mgawo yamebaki pale pale, na sasa wanaiita Problem Has Changed Name (PHCN).

Sunday, September 09, 2007

Kutoka Grahamstown

Jamaa alinikamata vizuri na kamera yake nilipokuwa nawasilisha mada yangu. Leo Septemba 10. 2007 imekuwa siku ya michakariko. mimi, Ndesanjo na Bob Sankofa tumekuwa tunawasilisha mihadhara yetu kwa wasikilizaji waliokuwa katika Digital Citizen Indaba. Tumejumuika na waandishi wengi kutoka sehemu mbalimbali za Afrika. Hotuba ya ufunguzi wa mjadala wa leo katika Indaba imetolewa na Ndesanjo. Pata sehemu ya mhadhara wa Macha hapa. Nitawaletea taarifa nyingine baadaye. Zoopy wameweka hapa sehemu ya kilichotokea.

Saturday, September 08, 2007

Nimekutana na Ndesanjo

Tayari nimefika Grahamsatown, alasiri Jumamosi Septemba 9, 2007. Nimekutana na Ndesanjo Macha kwa mara ya kwanza, ana kwa ana. Muda wote tulikuwa tunafahamiana kupitia blogu na magazeti. Baadaye jioni tutakuwa kwenye hafla ya ufunguzi wa Digital Citizen Indaba kama nilivyoeleza hapo chini.

Friday, September 07, 2007

Naenda Bondeni

Wiki hii nitakuwa Bondeni kushiriki mkutano wa Highway Africa na wanahabari wengine kutoka pande mbali za Afrika na kwingineko duniani. Mojawapo ya majukumu yangu huko ni kuzungumzia uandishi mpya wa kijamii katika mkusanyiko ujulikanao kama Digital Citizen Indaba siku moja kabla ya mkutano wenyewe, ambako pia nitashiriki kujadili mada ya kublogu, nikiwa pia na gwiji wa kublogu, mwanablogu nambari wani wa Kiswahili, Ndesanjo Macha na wadu wengine. Msiwe mbali na blogu.

Sunday, September 02, 2007

Asante Lowassa, heko Nyamongo

HII ndiyo nukuu yangu kuu kutoka kwa Waziri Mkuu Edward Lowassa.

Makamanda wanyeshewa mvua Geita


Mvua haikuwazuia kufanya walichodhamiria. Hii ni sehemu ya umati wa waliohudhuria mkutano wa wapinzani Geita Mjini, Septemba 2).Anayehutubia ni Mwenyekiti wa Chama cha demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Freeman Mbowe.
(Picha kwa hisani ya Joseph Senga).

Ndimara Tegambwage afungua blogu


Mwandishi mkongwe wa vitabu na magazeti; mchambuzi mahiri na mjenzi makini wa hoja kali; mmoja wa waasisi wa mageuzi ya vyama vingi nchini; mbunge mstaafu wa Muleba Kaskazini; Ndimara Tegambwage, anayeandika safu ya SITAKI (na hii hapa mpya) katika gazeti la Tanzania Daima Jumapili, ameingia katika ulimwengu wa blogu. Jina lenyewe la blogu ni dalili tosha kwamba kishindo chake kitakuwa kikubwa.

Wanablogu wengi ninaowajua ni vijana. Wazee wengi wa rika la Ndimara wamekuwa waoga wa teknolojia. Lakini Ndimara hazeeki. Hata katika dotikomu naye yumo. Na kwa wanaomfahamu, Ndimara ni kijana kuliko vijana wengi tulionao, waliozeeka kabla ya wakati wao. Msome hapa.


Mbowe, Zitto watua Mwanza


Wamo katika helikopta hii inayokaribia kutua katika uwanja wa Mirongo, Mwanza, wakiwa na viongozi wengine wa upinzani wanaoandamana nao. Umati wa wananchi, unaishuhudia inavyotua kabla ya mkutano kuanza. (Picha zote kwa hisani ya Joseph Senga)

Mresha katika Chopa ya Mbowe


Mheshimiwa Mrema ameshuka kwenye Chopa, ilipotua katika uwanja wa Mirongo, Mwanza.

Mrema naye atema tete


Mzee wa Kiraracha naye alikuwapo. Hapa anawapa shule wakazi wa Mwanza walioketi chini kumsikiliza.

People's Power


Mbowe 'akiwachochea' wananchi kutumia nguvu ya umma kuishikiza serikali adabu.

Friday, August 31, 2007

Hekalu la Manji?

Bwana ee! Tazama nyumba hii. Lakini Waswahili wanasema imevuka viwango vya kuitwa nyumba. Hili ni Hekalu. Na hizi hapa chini ni sehemu chache za hekalu hilo. La nani? Aliyetuma hizi ni la Yusuf Manji - yule mfadhili wa Klabu ya Yanga; "mgomvi" wa Regi Mengi (na sasa hivi Waislamu kuhusu kiwanja); mfadhili wa Chama Cha Mapinduzi (CCM); lakini mmoja wa wasomaji wa blogu hii anasema si kweli bali ni nyumba ya Rais Pervaiz Musharaf, mtu aniyejipenda kweli kweli, mchezaji hodari wa Badminton, Jenerali wa Pakistani. Iwe ya yeyote yule, inapendeza na kuvutia. Tazama!

Endelea


Sema mwenyewe


Quite Spacious


Hapa je?


Safi


Chunga, chini panateleza


mh


Mh!


Tuizunguke meza hii


Zungumza, ukichoka pumzika kidogo


Unataka kuogelea?



Labda haya ndiyo Maisha Bora. Tumuulize Kipanya hapo chini!

Thursday, August 30, 2007

Maisha Bora


Nimeipenda katuni hii ya Maosud 'Kipanya.' Wewe je?

Zitto apikiwa kashfa mpya


Habari zilizotapakaa ni kwamba wanamtandao, wakiongozwa na kinara wao, Rostam Azizi, wanapika kashfa mpya dhidi ya Zitto Kabwe (pichani kulia). Eti walitengeneza ya Amina Chifupa ikawalipukia na kuua mtu. Hawakuridhika. Wamejarbu kumdhalilisha Bungeni, akaibuka mshindi. Wananchi wanamshangilia, CCM wakazomewa. Sasa wamesikia Zitto na viongozi wa CHADEMA wanaanza kuzunguka mikoa 10 kuishitaki serikali kwa umma, wanamtandao wanakula njama mpya kwa kutumia baadhi ya vyombo vya habari 'kupika' kashfa mpya. Nia yao ni kupunguza imani ya wananchi na mvuto wa Zitto. Wamekiri, lakini inawauma, kwamba kwa sasa, Zitto amemfunika JK kwa mvuto.

Je, wahariri watakubaliana na mbinu za kina Rostam Azizi? Je, wananchi watamtosa Zitto? Kumkumbatia nani? Je, serikali itabadili sera zake kuhusu madini au itaendelea tu kuhangaika na namna ya kumsakama Zitto?

Tuesday, August 21, 2007

Uchumi ukue, bei zipande hivi?

Waziri Mkuu, Edward Lowassa, anasema uchumi unakua. Lakini wataalamu wanasema bei za bidhaa zinapanda kila siku. Ni ukuaji gani huu wa uchumi? Habari hii imeandikwa na gazeti la serikali, Daily News Agosti 21.08.2007. Soma mwenyewe uone hali ilivyo.

Inflation nears double digits

Overall inflation rate jumped to nine per cent in July, from 5.9 per cent in June, a trend which the National Bureau of Statistics (NBS) attributed to increased food and non-food prices.

“The July 2007 inflation rate has gone up by 3.1 percentage points compared to the June figure,” the Bureau said in a statement made available yesterday. “Some prices for both food and non-food items had gone up,” it added.

Analysts feared the impact of price hikes on the economy, with inflation, a key indicator for consumer comfort and investor confidence, nearly hitting the double digit mark, the highest in more than five years.

The government had for the last three years, targeted to push inflation to a manageable below 4.0 per cent, which could now prove to be quite an uphill task. Before, inflation had nearly dragged the economy to its knees with almost record over 30 per cent rate.

Planning, Economy and Empowerment Minister Professor Juma Ngasongwa told parliament in June that in 2006, average inflation was 7.3 per cent, compared to 5.0 per cent in 2005. In March, this year, inflation was recorded at 7.2 per cent.

The minister attributed the upswing in inflation to increased commodity prices, especially food and petroleum products which also led to high costs of transport and generation of thermal electricity.

The minister expressed optimism on declining inflation after some parts of the country started harvesting food crops, saying in April 2007, the inflation rate had declined to 6.1 percent, from 7.2 per cent registered in March 2007.

NBS said in the statement yesterday that hiked food prices were wheat flour, bread, spaghetti, potatoes and meat. Prices of bananas, fish, cooking oils, beans, cowpeas, sugar and meals in restaurants had also gone up.

It said non-food items that had increased prices were instant coffee, rent, kerosene, electric cookers, sewing machines, kerosene stoves, laundry soap (bar and powdered), scrubbing brush, broom head, tooth brush and hair creams.

Prices that have also gone up include those of car batteries, diesel, petrol, bus fares and private secondary school fees.

However, it noted that prices of clothing, footwear, watches and cell phones had gone down.


Daily News Reporter
Daily News; Tuesday,August 21, 2007 @00:02

Sunday, August 19, 2007

Picha nyingine za Zitto na waandamanaji

Bonyeza hapa uone picha na usome mjadala mwingine mpana.

Habari Leo waua stori ya Zitto Kabwe


Magazeti ya serikali, Sunday News and Habari Leo Jumapili, 'yalikataa' kuandika habari za maandamano na mkutano wa Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe, uliofanyika Dar es Salaam Agosti 18 kulaani hatua dhalimu ya Bunge dhidi ya mbunge huyo. AIBU!
Waandishi wao waliyashuhudia maandamano, mkutanoni walikuwepo, lakini walishindwa kutekeleza wajibu wao wa kitaaluma. UZALENDO uko wapi? Kama wanawadharau hao waliokusanyika kumsikiliza Kabwe, wanamwandikia nani?
Hata hivyo, mpiga picha wao aliweza kumshawishi mhariri wake kutumia walau picha inayoonyesha sehemu tu ya umati uliokusanyika Jangwani kumsikiliza Kabwe. Tazama mwenyewe.

Karamagi anasafiri na mihuri yetu?


KAMA Waziri wa Nishati na Madini, Nazir Karamagi, anaweza kusaini mkataba wa madini nje ya nchi, London, Uingereza, wakati yuko ziarani na Rais Jakaya Kikwete, ina maana anasafiri na mihuri yetu? Pata uchambuzi wa swali hili HAPA, na toa maoni yako chini.

Saturday, August 18, 2007

Kishindo cha Zitto Kabwe


Dar es Salaam inazizima. Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe, amegeuka shujaa wa mwaka. Habari kutoka Dar zinasema amekuwa gumzo kila kona, wala mvua nzito haikuweza kuwazuia wananchi kuandamana na kusukuma gari lake kutoka Ubungo hadi viwanja vya Jangwani, Jumamosi, Agosti 18, 2007, alikohutubia mkutano mkubwa na kusema Waziri wa Nishati na Madini, Nazir Karamagi, alisaini mkataba katika Hoteli ya Churchill, London, Uingereza.

Watawala wameduwaa. Bomu walilompasulia Zitto kumdhalilisha limewalipukia wenyewe! Hiki ndicho kishindo kinachozungumzwa. Anasema "tusikumbatie walioshiba" Ipate pia kwa kimombo Hoja kamili na mjadala wake Bungeni HII HAPA. Baadaye, wawekezaji wenyewe, Barrick walijitokeza kutoa maelezo HAYA, lakini Zitto akayachambua pia maelezo hayo na kubainisha uhusiano wa karibu sana kati ya waziri na wawekezaji, huku wakitoa maelezo yanayojikanganya zaidi.

Tuesday, August 14, 2007

Nauliza Kujibiwa

Mpendwa msomaji, nakamilisha mada yangu katika mazungumzo nitakayoshiriki kwenye kongamano la Highway Africa litakalofanyika Septemba 10-12, 2007, Rhodes University, Afrika Kusini. Nimefikiri kwamba ni vema kupata na kutumia mawazo ya wanablogu wenzangu na wasomaji wa blogu hii katika maswali kadhaa ninayojiuliza. Naomba ushiriki wako kwa kujibu maswali yafuatayo kwa kadiri unavyoona inafaa. Nakuhakikishia kwamba nitakapohitaji kutumia mawazo yako mahali popote, nitakunuu bila kuongeza chumvi. Asante. ANSBERT NGURUMO.

1. Kama wewe ni mwanablogu, kwa nini unablogu? Kama si mwanablogu, kwanini unasoma blogu?

2. Je, ni vema wanablogu (na wachangiaji wa maoni) watumie majina yao halisi? Faida na hasara zake ni nini?

3. Je, matumizi makubwa ya blogu yanamaanisha enzi za vyombo vya habari vya kale (redio, magazeti na TV) vimepitwa na wakati?

4. Je, wanablogu wanawajibika kwa nani?

Sunday, August 12, 2007

CCM inaandaa mapinduzi?

MAISHA magumu, kauli na uamuzi tata wa viongozi, mwafaka usiofikika? Vinatupeleka katika mapinduzi mengine? Hilo ndilo swali lwa wiki hii. Soma hapa.

Saturday, August 11, 2007

Wafanyakazi waitolea uvivu serikali


Haijapata kutokea. Terehe 11.Agosti.2007 iliandika historia mpya Tanzania. Wafanyakazi wameandamana na kuilaani serikali ya awamu ya nne kwa kuwadhalilisha, kuwasahau na kuwafanya watumwa katika nchi yao. Ujumbe wao ulifikishwa kwa maandamano, nyimbo, mabango na hotuba kali. Gazeti la Mwananchi Jumapili linaripoti hivi:

Wafanyakazi wampa Rais Kikwete siku 30

*Wamtaka Katibu wao kumwona na kurejesha majibu
*Wadai matumizi ya sheria kudai haki yameshindikana
*Walalamikia mishahara ya wabunge na ununuzi wa mashangingi

WAFANYAKAZI mkoani Dar es Salaam, wamempa siku 30 Katibu Mkuu wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi nchini (Tucta), Nestory Ngulla, kufikisha malalamiko yao kwa Rais Jakaya Kikwete na kurejeshewa majibu, kuhusu nyongeza duni ya mishahara, ili kuepusha hatua nyingine watakazotumia kudai mishahara.

Tamko hilo lilitolewa na wafanyakazi hao kupitia risala yao iliyosomwa katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika Viwanja vya Jangwani, jijini Dar es Salaam baada ya kuhitimisha maandamano ya amani yaliyoandaliwa na vyama 18 vya wafanyakazi nchini kupinga kima cha chini cha mshahara wa serikali, kilichopitishwa na bunge hivi karibuni.

Baadhi ya vyama hivyo, ni pamoja na cha Walimu (CWT), Sekta ya Afya (Tughe), Migodi, Nishati, Ujenzi (Tamico), Serikali za Mitaa (Talgwu), Mabaharia (Tasu), Walinzi binafsi (Tupse), Mashambani (Tpawu), Shughuli za Meli (Dowuta), Mawasiliano (Tewuta), Taasisi za Elimu ya Juu, Sayansi, Teknolojia, Habari na Utafiti (Raawu), Waandishi wa Habari (TUJ) na Chodawu.
Akisoma risala hiyo kwa niaba ya wafanyakazi hao, Katibu wa Raawu, Kanda ya Mashariki, Evarist Mwalongo alisema wamefikia hatua hiyo wakiamini kwamba, matumizi ya kisheria kudai mishahara yatawafikisha katika hali mbaya.

"Hali hiyo itakuwa imelazimishwa na serikali. Wafanyakazi hatutaki kufikia hali hiyo kwani Uhuru wa nchi hii tuliutolea jasho sisi wenyewe," alisema Mwalongo na kushangiliwa na umati wa wafanyakazi waliohudhuria mkutano huo.

Mwalongo alisema, wafanyakazi mwaka huu, wanadai nyongeza ya mishahara kutokana na kukithiri kwa shida baada ya nyongeza hiyo kulimbikizwa kwa miaka zaidi ya 13 iliyopita, hali ambayo imesababisha makali ya maisha kutovumilika tena.

Kutokana na hali hiyo, alisema serikali imekosa huruma na kuacha kutambua kuwa wafanyakazi nchini ndio waliodai Uhuru wakisaidiana na wakulima, badala yake imekuwa ikiwajali wafanyabiashara peke yake kwa kuwafanya kama ndio mhimili wake wa kusimamia sera, uchumi na siasa za nchi.

Mbali na hilo, Mwalongo alisema serikali imefikia kupuuza hata sheria zilizotungwa kusimamia na kulinda masilahi na masuala ya wafanyakazi.

Alisema inasikitisha kuona Wizara ya Utumishi chini ya Waziri wake, Hawa Ghasia, imeamua kudharau sheria namba 19 ya mwaka 2003 inayohusu majadiliano na vyama vya wafanyakazi kupanga mishahara ya watumishi wa serikali.

"Mheshimiwa Ghasia ameamua kupuuza utawala wa sheria na kuanza ukurasa mpya. Amepanga mishahara ya watumishi kadri alivyoona yeye kutoka Sh75,000 hadi Sh84,000.
Mshahara wa Sh84,000 unakatwa kodi ya Sh 600 kama kodi ya PAYE na akiba ya uzeeni Sh8,400, zinabaki Sh 75,000 ambazo ndiyo mshahara wa zamani.

"Mshahara huo ukigawa kwa Sh 30 utaona mfanyakazi ataishi kwa Sh2,500 kila siku ambazo zitumike kama matumizi mengine ya lazima kila siku. Kwa mantiki hiyo ndiyo maana vyama vya wafanyakazi vilipendekeza kima cha chini kiwe Sh315,000 sawa na Sh10,500 kwa siku," alisema Mwalongo.

Alisema inasikitisha pia kuoana Wizara ya Kazi, Ajira na Maendeleo ya Vijana chini ya Waziri wake, Kapteni John Chiligati, imeamua kulala usingizi kwa kutosimamia sheria namba 6 ya mwaka 2004 inayotakiwa kuunda Baraza la kupanga kima chini cha mishahara kwa ajili ya sekta binafsi ambako kuna hali mbaya kupindukia kwa kuendelea kupata mshahara wa Sh48,000 tangu mwaka 2002.

"Sisi wafanyakazi hatuelewi kama serikali ipo kwa ajili ya Watanzania kwani kwa mshahara wa Sh84,000 ukigawa kwa Sh10,500 kama matumizi kwa mahitaji ya lazima ya kila siku utadumu siku nane na kama mfanyakazi atakula mlo mmoja kwa siku utadumu siku 16 tu.

"Mshahara huo wa Sh84,000 ni asilimia 50 au nusu ya posho ya mbunge anayopata katika kikao cha siku moja na mshahara wa mbunge wa mwezi mmoja ambao ni Sh1,500,000 unaweza kumlipa mfanyakazi huyo kwa miezi 17.

Uchambuzi kama huu ukiwekwa watumishi wa kima cha Sh84,000 inasikitisha kiasi cha kujenga hasira mbaya katika jamii ya Watanzania," alisema Mwalongo.

Alisema pamoja na shida za mishahara duni, serikali imetengeneza mzigo mzito unaotokana na bajeti ya mwaka huu wa fedha wa 2007/08, iliyokuja na kodi kubwa katika mishahara, mfumuko wa bei uliotokana na bei kubwa ya mafuta ya dizeli, petroli na vilainishi vya mitambo na kwamba, usafiri wa kwenda kazini na kurudi nyumbani umekuwa pia gharama kubwa inayowatesa wafanyakazi maradufu.

"Kukosekana kwa vyombo vya usafiri, suala hili halishughulikiwi na serikali kwa vile wakuu wote wanatumia magari ya gharama za kutisha yanayowalaza usingizi wasione kuna nini kwa wananchi. Inasikitisha kuona kiongozi anapita na VX ya Sh150 milioni bila hata ya huruma kwa mtoto au watoto wa shule kama hapendi kuwapa msaada wafanyakazi wenzie ingetosha kuwaonea huruma watoto wa shule.

"Gari aina ya VX moja ingeweza kununua gari la kubebea wafanyakazi zaidi ya 100. Mfano huu ukizidishwa kwa namba ya magari ya mawaziri na watendaji wakuu wa serikali yetu utaona serikali inao uwezo mkubwa sana wa kugawa mshahara wa kuishi wa Sh 315,000 bila kikwazo," alisema Mwalongo.

Alisema mishahara midogo wanayolipwa wafanyakazi, inaleta uhafifu katika malipo ya uzeeni kwa wastaafu ambao wametumikia serikali kwa uadilifu mkubwa.

Mwalongo alisema bila kujali kuwa mishahara ni midogo, serikali bado inaendelea kuwaonea wafanyakazi kukopa kwa nguvu jasho la wanyonge, kwa kulimbikiza madai ya nauli, likizo, malimbikizo ya mishahara ya wafanyakazi, kama vile walimu wa Mkoa wa Dar es Salaam na watumishi wengine wa manispaa na mashirika mbalimbali.

Alisema wakati hali ikiwa hivyo, soko la ajira limetekwa na wageni kwa visingizio na kejeli dhidi ya wafanyakazi wazalendo, kwamba Watanzania ni wavivu, wazembe, hawajui Kiingereza na kadhalika.

"Inasikitisha wanaotoa kauli hizo ni Watanzania wenzetu bila kutambua kuwa dawa za kutibu uzembe, uvivu na kutojua Kiingereza ni malipo mazuri, mbona Watanzania wanang'ang'aniwa nchi za nje kwa bidii ya kazi na kuzungumza Kiingereza chenye fasihi tamu?

"Tunasema waache kutukejeli kuanzia sasa, iwe mwisho kuuza nafasi zetu za kazi ovyo, waone aibu wawekezaji wao wameanza kuwekeza mpaka katika vibanda vya kukaanga viazi na maua ya plastiki, watainuaje uchumi wetu?" alihoji Mwalongo.

Kutokana na hali hiyo, alisema iwapo mishahara haitaongezwa italeta athari kubwa, ikiwamo wafanyakazi kushindwa kushiriki katika vita dhidi ya rushwa, kiwango cha umaskini kitakithiri katika jamii, kipindupindu, ujinga, kukosekana tija ya taifa na nidhamu ya kazi.

Akizungumza katika mkutano huo, Mhadhiri Mstaafu wa Sheria wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Profesa Issa Shivji, aliishangaa serikali kuona ikikataa kutambua kwamba, wananchi hivi sasa wanakabiliwa na kipindi kigumu kutokana na kujenga mgawanyiko na mpasuko katika jamii ya Watanzania.

"Kuna kundi la matajiri na maskini, tuna tabaka la walala heri na walala hoi. Kama tutaendelea katika mwelekeo huu kwa kasi, tutajikuta tuna mataifa mawili," alisema Profesa Shivji na kushangiliwa na umati wa wafanyakazi waliohudhuria mkutano huo.

Katibu wa Kanda ya Dar es Salaam wa Chama cha Wafanyakazi wa Mawasiliano na Uchukuzi nchini (Cotwu), Buhari Semvua, akizungumza katika mkutano huo, alipinga msimamo wa serikali wa kuendelea na majadiliano Septemba, mwakani na wafanyakazi kuonya kuwa iwapo serikali itapuuza malalamiko yao nchi haitakalika.

"Hatukubali hiyo mwakani na wajue kuwa wananchi wakikata tamaa, hatua watakazochukua, patakuwa hapakaliki, hapatoshi. Siku 30 tusipojibiwa, hizi (maandamano) za leo ni rasharasha," alisema Semvua.

Naye Ngulla ambaye alikuwa mgeni rasmi katika mkutano huo, aliwataka wafanyakazi kutobabaishwa na wabunge na kuahidi kwamba, atahakikisha anafikishia serikali malalamiko yao ndani ya muda aliopewa.

Mkutano huo ulitanguliwa na maandamano ya wafanyakazi hao yaliyoanzia katika Ofisi za Makao Makuu ya Tucta, Mnazi Mmoja saa 2:00 asubuhi na kupita katika Barabara za Bibi Titi Mohamed na Morogoro na kuishia katika Viwanja vya Jangwani, huku waandamanaji wakiwa wamebeba mabango na kuimba nyimbo zenye ujumbe wa kuilaani serikali.

Baadhi ya mabango yalisomeka: "Walalahoi Sh84,000 kwa mwezi, mbunge Sh120,000 kwa siku, haki iko wapi?" "Mshahara huishia nauli ya daladala, vigogo kwenye mashangingi, kima cha chini kiongezwe, hii ni haki", "Mishahara iendane na hali halisi ya uchumi wa nchi kwa sasa", "Bila walimu Rais Kikwete ungekuwa wapi? Mbona hutukumbukwi?"

"Nauli za likizo hazitolewi kwa wakati kwa nini? Walimu tunateseka", "Haturidhiki na waraka mpya wa mshahara", "RAAWU Taasisi ya Watu Wazima. Kwa ari hii, kasi hii, nguvu hii na mishahara hii ya wafanyakazi tumekwisha!" "Kuna siri gani kati ya sekta binafsi na serikali kuhusu mishahara?"

Mbali na mabango hayo, waandamanaji hao walikuwa wakiimba kwa kusema: "Na sisi hatulali, bado mapambano, mpaka kieleweke", "Kilio, kilio, kilio, tutamlilia nani?"

Sunday, August 05, 2007

Sunday, July 22, 2007

Tanzania isiyo na UKIMWI inawezekana?

Soma hapa.

Serikali Kupinduliwa

HABARI hii ilileta kizaazaa kati ya serikali na gazeti la MwanaHALISI Jumatano 18.07.2007. Serikali inagombana na maoni ya wakili na mwanasiasa maarufu, mmoja wa waasisi wa mageuzi ya kisiasa nchini, Mabere Nyaucho Marando.

Marando anasema serikali inaweza kupinduliwa, iwapo wananchi watajua haki zao.

“Wewe unatumia lugha ya kupindua. Kwa lugha ya kawaida, kupindua ni kutumia nguvu za kijeshi. Lakini yapo mapinduzi mengine yanayowezekana. Ni yale yanayotokana na mwamko wa wananchi,” amesema.

Katika mahojianao maalum na MwanaHALISI juu ya miaka 15 ya kurejeshwa kwa mfumo wa vyama vingi, Marando amesema, “Wananchi wana uwezo wa kuipindua serikali kupitia njia halali ya sanduku la kura.”

Akihusisha hasa na madai ya wabunge wa CCM, Job Ndungai na Janet Masaburi wakati wa mjadala wa bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi, kwamba elimu inayotolewa na HakiElimu inaweza kusababisha serikali kupinduliwa, Marando alisema:

“Hili linawezekana kabisa. Kinachohitajika ni mwamko zaidi kwa umma. Wananchi wakipata mwamko, wanaweza kuipundua serikali kwa njia ya kura.
Marando amesema serikali ya sasa imeshindwa kuwajibika na hivyo inaweza kung’olewa kwa nguvu za umma.

Amesema HakiElimu inafanya kazi nzuri na inaifanya vizuri na kwamba vyama vya upinzani havina budi kujifunza kutoka HakiElimu, hasa katika suala la utafiti wa hoja muhimu za haki za binadamu na maslahi ya jamii.

“Unajua, CCM inaumwa ugonjwa wa kusinyaa. Ugonjwa huu huvipata vyama vilivyokaa madarakani kwa muda mrefu. Chama kikikaa madarakani kwa muda mrefu, kinasinyaa. Kinakuwa na mchoko,” anasema.

Katika mahojiano ambayo yamechapishwa katika toleo hili, Marando anasema, sababu za kuchukia CCM bado zipo, “Hiki bado ni chama cha kidkteta. Matumaini ya wananchi bado yapo, kwamba kuna siku watajikomboa kutoka udikteta huu.”

Kuhusu mafanikio ya upinzanai katika kipindi hiki, Marando anasema, “uwanja wa demokrasia umepanuka. Serikali inachukua hatua, japo kwa kiwango kidogo na bila upinzani serikali ingefanya itakavyo. Siridhiki, lakini angalau tumepata mahali pa kuanzia.”

Alipoulizwa CCM inaweza kujivunia nini katika miaka hiyo, Marando alisema, “Wanaweza kujivunia bahati yao nzuri ya kushikilia madaraka bila kuwa na sababu za msingi za kutawala na kuendelea kubaki madarakani wakati hawastahili kuwapo.”

Marando amesema CCM haina zaidi cha kujivunia, “Labda ujinga wanaowalisha kwa Watanzania kwamba CCM ndiyo baba na ndiyo mama, wakati si kweli. Wanaweza kujivunia pia rushwa ambayo wameifanya kuwa sera ndani ya CCM na serikali yake. Basi!”

Kuhusu uwezo wa vyama vya upinzani kifedha, Marando anasema, ni kweli vyama havina fedha wala wafadhili, “Lakini lazima wafanye kazi hiyo. Waende kwa Watanzania wenzao… kuomba msaada. Hilo ni jukumu lao na hawawezi kulikwepa hata kidogo.”


Soma Mahojiano na Marando

MwanaHALISI, Serikali wakaribia kuzichapa

Serikali ya awamu ya nne bado inaendelea kukosa uvumilivu. Huku rais Jakaya Kikwete akidai haogopi kukosolewa, matendo ya serikali yake yanaonyesha tofauti. Baada ya kulikosakosa Tanzania Daima mara kadhaa, sasa imeamua (kwa mara nyingine) kulivalia njuga gazeti la kila Jumatano la MwanaHALISI. Soma hapa. Kutokana na sakata hilo, Mchambuzi na Mwandishi mkongwe, Ndimara Tegambwage, anaipatia serikali TUISHENI ya bure.

Sunday, July 15, 2007

Marais wastaafu wafe au washitakiwe?

Rais mstaafu anapokufa taifa haliyumbi. Lakini wapo wanaosema kwamba akishitakiwa kwa makosa aliyofanya akiwa madarakani taifa litayumba. Hii ni kweli au kuna linalofichwa nyuma ya hoja hii? Soma mjadala.

Sunday, July 01, 2007

Amina aliiogopa CCM kuliko wauza mihadarati

Alisema: "nawajua ni watu wa namna gani...wanaweza kunidhuru...”

Buriani Amina Chifupa; umekwenda kishujaa




Na Ansbert Ngurumo, Hull
1.
Amina Mpakanjia;
Nani asiyekujua?
Nani hajakusikia?
Nani hakukutambua?

2.
Eti umetukimbia?
Sikubali nakataa;
Nani kakuondoa?
Lipi umemfanyia?

3.
Amina, mi siamini;
Kwamba tena sikuoni;
Haraka hiyo ya nini?
Wakimbia ‘fanya nini?

4.
Najua hukuwa radhi;
Kwenda chini ya aridhi;
Yatoka wapi maradhi;
Bila idhini ya Kadhi?

5.
Bado ulikuwa dogo;
Miongoni mwa vigogo;
Yako marefu malengo;
Sasa wayapa kisogo.

6.
Umekwenda kwa lazima;
Siku zote tutasema;
Umeondoka mapema;
Nani amekusukuma?

7
Mungu ndiye anajua;
Kwanini watangulia;
Ameshindwa kuzuia;
Majonzi ya Tanzania.


8
Kama angetuuliza;
Nani kumtanguliza;
We tusingekupoteza;
Kura tungezipunguza.


9
Si wewe mwenye hatia;
Ulopaswa tangulia;
Wapo walokuvizia;
Sasa umewakimbia!

10.
Wapo waliokubeza;
Mwenyewe ukanyamaza;
Pole pole ukaanza;
Hadi wao kushangaza.

11.
Kisomo chako kidogo;
Si kama chao vigogo;
Kiliyabeba magogo;
Kuwaachia usongo.

12.
Woga ‘liweka pembeni;
Na nchi yako usoni;
Lionekana makini;
Kama vile wa zamani.

13.
Vijana uliwawaza;
Hata wale wasocheza;
Sumbawanga hadi Mwanza;
Ulisema: ‘hawa kwanza.’

14.
Soka ulishangilia;
Timu yetu saidia;
Nguvu kuiongezea;
Us’okuja shuhudia.

15.
Watoto ulitetea;
Kama mama asilia;
Ulijua Tanzania;
Hao yawategemea.

16.
Yatima ‘lisaidia;
Tumaini ‘liwatia;
Wagonjwa ‘lisalimia;
Wote uliwawazia.


17.
Tabasamu lilijaa;
Huruma lilichochea;
Urembo ulitumia;
Wengi kuwahudumia.

18.
‘Liitwa Mama shughuli;
Kwa kazizo mbalimbali;
Hata kuwapamba wali;
Mambo yako kali kali.

19.
Kikwete anauliza;
Sitta huyo kanyamaza;
Chifupa amepoteza;
Nani ‘tambembeleza?

20.
Wapo ul’oshambulia;
Kwa haki nakutetea;
Mihadarati bugia;
Hukutaka kusikia

21.
Nyota yako iliwaka;
Hata kwa wasoitaka;
Haya sasa umetoka;
Lije walilolitaka?

22.
Sadaka uliyotoa;
Sote tunaitambua;
Hata walokusumbua;
Hili watalijutia.

23.
Hatuwezi simangana;
Sasa twafarijiana;
Ila twaweza ‘onyana;
Hata kushauriana.

24.
Amina umetoroka;
Waacha moto wawaka;
Umejitoa sadaka;
Tutakayoikumbuka.

25.
Twajua ‘metangulia;
Sote tutaelekea;
Ila moja twatambua;
Umekwenda kishujaa!

26.
Umekimbia kwa kasi;
Kuliko hata ya fisi;
Vijana watakumisi;
Wabunge hata na sisi.

27.
Kina mama wanalia;
Mwenzao wakumbukia;
Wasanii nao pia;
Nyimbo wanakuimbia.

29.
Maisha yako twakiri;
Ni mafupi na ya heri:
Marefu yaliyo shari;
Umeachia wapori.

30.
Tulia na Malaika;
Pale atapokuweka;
Tabasamu cheka cheka;
Yametimu, yamefika.

31.
Ukiukuta mpira;
Cheza na Hawa na Sara;
Shambulia mduara;
Hata mbinguni, ahera.

32.
Mpakanjia na mwana;
Baba na Mama Amina;
Kubali ya Maulana;
Itikieni: Amina.

Thursday, June 28, 2007

Sunday, June 24, 2007

Nauli nafuu kwenda popote

Ni kama tangazo vile, lakini ni huduma muhimu kwa wasafiri. Soma hapa.

Uzalendo wa Meghji unatia shaka

Tuhoji upeo wa Waziri wa Fedha, Zakhia Meghji, katika suala la uzalendo.

Wednesday, June 20, 2007

Furaha ya Stars, ulevi wa watawala

Watawala wetu wanataka kufunika machungu ya bajeti ya serikali kwa chereko za ushindi wa Taifa Stars dhidi ya Burkinafaso? SOMA HAPA

Sunday, June 03, 2007

Watanzania wataacha lini kuwashabikia 'manabii'?

'Nabii' mmoja wa Tanzania aliyedai ametokewa na Roho Mtakatifu, alioa wanawake wote kijijini kwake, akazaa nao watoto 59 ambao hakuwasomesha! Aliwaahidi wafuasi wake kwamba wangepaa kwenda mbinguni baada ya miaka 70, akafa kabla ya unabii wake kutimia. sasa limekuwa zogo. Watanzania tunapata somo gani? SOMA hapa.

Wednesday, May 30, 2007

Wanamtandao waanza kunijibu

Wa Kwanza amesema hivi. Kwa bahati ya ajabu, alikutana na makala yangu inayomhoji yeye binafsi na wenzake siku hiyo hiyo, katika gazeti hilo hilo. What a coincidence! Majibu yangu kwa baadhi yao ni haya.

Monday, May 28, 2007

Tumeshindwa Real Madrid, Tutaweza MKUKUTA?

REAL Madrid 'imetema' mwaliko wa JK. Ina maana gani? Soma UCHAMBUZI HUU.

Sunday, May 20, 2007

Serikali ishindwe, mamluki waweze?

KUNA mkakati mpya wa 'kazi' uliobuniwa na baadhi ya viongozi wa serikali yetu pale wanaposhindwa kujibu hoja za wakosoaji zinazoibuliwa katika vyombo vya habari. Hawatoi majibu, lakini wanaandaa mamluki kushambulia wakosoaji wa 'wakubwa.' Serikali iliyoanzia magazetini, imerudi tena magazetini? Mamluki hawa wanaweza kutoa majibu ya serikali? Serikali yenyewe inafanya nini? Soma UCHAMBUZI HUU, na toa maoni yako.

Sunday, May 13, 2007

Mwanza ina nini na Rais Kikwete?

Kwanza kuvamiwa jukwaani; pili mapanki; na sasa Chitalilo. Kwa NINI?

Wednesday, May 09, 2007

Karibu Katika Nyumba Mpya

Kwa sababu za msingi kabisa, nami nimejenga nyumba mpya mpya. Wengine wanasema ni kiota. Unataka kuingia? Bofya hapa

Sunday, May 06, 2007

Kina Chiluba Wengi Afrika

Tunazungumzia kupiga vita rushwa? Zambia imetoa mfano na funzo kwetu. Nasi Tanzania tunao kina Chiluba wengi. Badala ya kuwachukulia hatua tunawalinda. BOFYA HAPA.

Sunday, April 29, 2007

Boyz II Men wanaogopa kuitwa wasanii?


Soma Maswali yangu kwa serikali ya JK inayong'ang'ania kufuga na kutisha vyombo vya habari na wanahabari. Hii Hapa.

Thursday, April 12, 2007

Watawala wafe, taifa lifufuke

Hizi ndizo salaam zangu za Pasaka mwaka huu 2007 kwenu wasomaji. Zipo HAPA.

Sunday, March 18, 2007

Inatekenya mbavu, au vipi?




MARA moja moja ni vema kujiburudisha kidogo, kucheka, kulegeza misuli na kupunguza tension. Katuni hii imetumwa kwangu na Peter Nyanje, ambaye ameipokea kutoka kwa wengine katika mzunguko wa kutumiana vichekesho. Nikaona vema niipatie mahali pa kutulia, ili wasomaji wa blogu hii, hasa wale ambao hawakupata na hawatapata 'bahati' ya kutumiwa katuni hii, nao wapate uhondo huu. BOFYA kwenye picha usome maelezo yake.

Monday, March 12, 2007

Makala za kihistoria juu ya Chifu Marealle

Historia ni mama wa elimu yote. Zisome makala hizi mbili, utakiri hii ni sehemu nyeti ya historia yetu, katika nafsi ya Hayati Chifu Thomas Marealle. Anza na hii ya Kibanda, halafu malizia na hii hapa ya Halimoja.

Sunday, March 11, 2007

Friday, March 09, 2007

Eti Pombe ina homoni za kike?

Hii imenifikia katika mzunguko wa kutumiana meseji za utani, nikaona niiweke hapa kwa faida ya wasomaji. Nadhani huu ni utani tu, usioweza kusababisha ugomvi kwa wanaharakati wa jinsia.

Last month, National University of Lesotho scientists released results of a recent analysis that revealed the presence of female hormones in beer. Men should take a concerned look at their beer consumption. The theory is that beer contains female hormones (hops contain phytoestrogens) and that by drinking enough beer, men turn into women. To test the theory, 100 men drank 8 pints of beer each within an hour period. It was then observed that 100% of the test subjects:

1) argued over nothing.
2) refused to apologize when obviously wrong.
3) Gained weight.
4) Talked excessively without making sense.
5) Became overly emotional.
6) Couldn't drive.
7) Failed to think rationally
8) Had to sit down while urinating.

No further testing was considered necessary.

Wednesday, March 07, 2007

TUENDAKO: Uchambuzi Bora kwa miaka 10

Nimesoma makala nyingi za Kibanda, kwa miaka 10 iliyopita. Ni mwandishi mzuri na makini. Lakini sijawahi kusoma makala yake nzuri kuliko hii hapa. Ameikuna akili yangu. Bofya hapa chini usome mwenyewe.

http://www.freemedia.co.tz/daima/2007/3/7/makala7.php Soma pia nondo za Kibanda kwa JK katika mfululizo wa makala za TUENDAKO.

Sunday, March 04, 2007

Tukubaliane, hatuna Wimbo wa Taifa

Unajua kwamba Watanzania hatuna Wimbo wa Taifa? Bofya hapa uone sababu.

Saturday, March 03, 2007

Zama mpya, majibu ya kizamani

Majibu ya kizamani, zama mpya! Inakubalika? Bofya hapa.

Thursday, February 22, 2007

Soksi za Rais Zimetoboka: Vidole Vinachungulia

World Bank President Paul Wolfowitz may be dedicated to freeing the world from poverty - but he seems unable to afford a new pair of socks!!Mr. Wolfowitz's sartorial deficiencies were revealed when he took his shoes off while visiting a mosque in Edirne, western Turkey. The guy's torn socks were there for all to see!!......By the way, zako zikoje leo!!? For records purposes, the last World Bank annual report, for 2006, puts the president's salary as of 1 July, 2005, at $391,440 (£200,279)....... An almost/equivalent of Tshs. 300,020,925 per month!!........

(Imetumwa kwangu na mtu aliyekuwa anaizungusha kwa marafiki)

Monday, February 19, 2007

'Mchemsho' wa Uhuru: Uingereza yawa Marekani


JUMAMOSI Februari 17, 2007 Rais Jakaya Kikwete alikuwa nchini Uingereza na alikutana na badhi ya Watanzania waishio nchini humo na kuzungumza nao. Cha kushangaza, gazeti la Uhuru linalomilikiwa na Chama Cha Mapinduzi (CCM) ambacho yeye ni mwenyekiti, lilitumia picha zake na kuwaeleza Watanzania na dunia nzima kwamba Rais alikuwa Marekani, na kwamba Balozi wa Tanzania nchini Marekani ni Mwanaidi Maajar. CAPTION ya picha unayoona hapa iliyotumika katika tovuti ya gazeti la Uhuru 19.02.2007 ilisema hii:
RAIS Jakaya Kikwete akisisitiza jambo alipozungumza na Watanzania waishio Marekani, kwenye hoteli ya London's Royal, juzi Kushoto ni mke wa Rais, Mama Salma Kikwete na kulia ni balozi wa Tanzania nchini Marekani, Mwanaidi Maajar. (Picha na Freddy Maro).

Sunday, February 18, 2007

Ndiyo. Tuchukie, Tuchukue Hatua

Ndesanjo ametema cheche katika gazeti la Mwananchi Jumapili Februari 18, 2007. Makala yake niliiunganisha hapa, lakini baada ya Jumapili kupita, ikawa haipatikani tena. Sasa ukibofya, inakuja nyingine mpya; nikaamua kuhariri na kuiondoa. Nadhani wataalamu wa tovuti ya Mwananchi wanapaswa kujua kuwa tovuti yao haitunzi kumbukumbu za nyuma; warekebishe kasoro hiyo. Lakini hoja ya Ndesanjo ni kwamba Watanzania wasiwe wanachukia tu maovu ya watawala wao, wanalalamika, halafu uchaguzi ukifika wanawarejesha madarakani. Wawaondoe. Anasema ni vema waanzie kwenye serikali za mitaa, si Ikulu tu. Makala inasisitiza kile ambacho mwandishi mwingine, Ndimara Tegambwage, hupenda kukiita 'kuchukia na kuchukua hatua.' Kama unaweza itafute uisome mwenyewe. Ni tamu!

Saturday, February 17, 2007

Sijanuna; natafakari

Usitazame glasi. Mtazame huyo anayekutazama, mwenye glasi. Unaweza kumtambua katika picha ya pili? Hiyo ilikuwa Novemba 11, 2006 baada ya mkutano na mafunzo ya uandishi wa habari za sayansi ulioandaliwa na kudhaminiwa na Shirikisho la Waandishi wa Habari za Sayansi duniani (WFSJ), 4-10 Novemba, 2006 Nairobi, Kenya. Nilirejea UK kesho yake. Washiriki wengine, katika matukio tofauti, wapo hapo chini. Picha kwa hisani ya WFSJ.






My photo
Nimechongwa na mambo haya: Falsafa, Fasihi, Muziki, Habari na Harakati. Sifuati mkumbo. Napenda kuhoji na kudadisi - hulka ya kifalsafa ya kuusaka ukweli - 'UKWELI ULIO UCHI.'