Tuesday, December 23, 2008

Tunawataka vigogo

Vita dhidi ya mafisadi ndo inaanza kukolea. Baada ya shinikizo la wananchi, vigogo kadhaa sasa wanaanza kuadhirika kwa kufikishwa mahakamani. Huu ni ushindi wa wananchi, si wa serikali; kwa kuwa tangu awali ilikuwa haikubali kuwa kuna ufisadi, na kwamba walioufanya wamo au walikuwa serikalini. Wachunguzi wa mambo wanajua kuwa kinachofanyika sasa ni mchezo wa kisiasa unaolenga kulegeza hisia za wananchi kuelekea uchaguzi wa serikali za mitaa mwaka 2009 na uchaguzi mkuu mwaka 2010 kwa ajili ya CCM. Zaidi ya hayo, baadhi yetu tunasema, waliokamatwa hadi sasa ni DAGAA tu. Tunawataka vigogo wenyewe!

Sunday, December 21, 2008

Hata Bush kapigwa kiatu

Rais Jakaya Kikwete alirushiwa mawe akiwa ziarani Mbeya watu wakashangaa; na sasa Rais George W. Bush wa Marekani karushiwa kiatu katika mkutano na waandishi wa habari akiwa ziarani Iraq.
My photo
Nimechongwa na mambo haya: Falsafa, Fasihi, Muziki, Habari na Harakati. Sifuati mkumbo. Napenda kuhoji na kudadisi - hulka ya kifalsafa ya kuusaka ukweli - 'UKWELI ULIO UCHI.'