Tunahitaji kujua kwa sababu hatujui; na hatuwezi kujua kama hatujui kwamba hatujui...Hatutajua chochote iwapo hatutahoji na kudadisi. Na kadiri tunavyojua, ndivyo tunavyogundua kwamba hatujui...
KILE zilichoshindwa timu zetu za soka, Coca-Cola imeweza: kulileta kombe la dunia Tanzania. Walau imetuwezesha kuliona, kulishika, kulinusa na kupiga nalo picha. Walau hili tumeliweza! Sijui uwezo wetu ndo umeishia hapo, au tumehamasika!
Nimechongwa na mambo haya: Falsafa, Fasihi, Muziki, Habari na Harakati. Sifuati mkumbo. Napenda kuhoji na kudadisi - hulka ya kifalsafa ya kuusaka ukweli - 'UKWELI ULIO UCHI.'