Monday, November 14, 2005

Kazi na Tabasamu


Anaitwa Amissa Chayeb, mhudumu katika mgahawa mmojawapo katika kituo cha kumbi za mkutano, KRAMA Palexpo, Tunis, unapofanyikia mkutano wa Umoja wa Mataifa ulioikusanya dunia nzima kujadili namna ya kutumia TEKNOHAMA. Kazi ya Amissa ni kuwapatia wateja huduma- chai, kahawa, maziwa na vitafuno kidogo - lakini dakika hii, hawapo. Afanyeje? Sana sana kutabasamu, akimngoja mmoja mmoja anayeingia.

No comments:

My photo
Nimechongwa na mambo haya: Falsafa, Fasihi, Muziki, Habari na Harakati. Sifuati mkumbo. Napenda kuhoji na kudadisi - hulka ya kifalsafa ya kuusaka ukweli - 'UKWELI ULIO UCHI.'