Wednesday, October 28, 2009

Sasa tumejua, tatizo ni rais

Baada ya Rais Jakaya Kikwete kukiri kwamba wasaidizi wake walimshauri apumzike akakataa, ndiyo sababu akazidiwa hadharani pale Mwanza, sasa kumeibuka hoja mpya. Je, kama rais anadiriki kuwapuuza wasaidizi wake katika suala nyeti la afya yake, nao wananywea; atawezaje kuwasikiliza wasaidizi na washauri wake katika masuala ya uchumi, siasa, usitawi wa jamii na mengine? Si inawezekana rais ana washauri wazuri wa mambo mengi tu lakini hawasikilizi? Hii si sehemu ya ushahidi kwamba rais ndiye tatizo?
My photo
Nimechongwa na mambo haya: Falsafa, Fasihi, Muziki, Habari na Harakati. Sifuati mkumbo. Napenda kuhoji na kudadisi - hulka ya kifalsafa ya kuusaka ukweli - 'UKWELI ULIO UCHI.'