Monday, November 14, 2005

TEKNOHAMA Kazini; Sengerema Hadi Tunis


Felician Ncheye ni mkazi wa Sengerema, mkoani Mwanza. Kazi yake ni kutoa huduma ya mawasiliano kwa njia ya mtandao wa kompyuta kwa wakazi na wapita njia wa Sengerema kwa kutumia kituo chake, Sengerema Telecentre. Katika picha hii, yupo Tunis, kwenye Banda la Tanzania, katika mkutano wa dunia kuhusu Jamii ya Habari na Mawasiliano (WSIS), alikokwenda kuwaonyesha wananchi kutoka sehemu mbalimbali za dunia kwamba naye wamo katika mtandao. (Picha na Ansbert Ngurumo 14.11.2005)

3 comments:

Reggy's said...

Naamini kwamba upo hai, lakini sikuoni katika blogu. Ninakutembelea bila kukuta kitu kipya, ipo siku mimi na wenzangu tutakata tamaa ya kuja kwako

Ansbert Ngurumo said...

Nimekusikia mkuu. Usinikimbie. Nimerejea. Hebu nitembelee.

John Mwaipopo said...

Ngurumo kiunganishi cha maoni kwenye post za hapo juu kulikoni?

My photo
Nimechongwa na mambo haya: Falsafa, Fasihi, Muziki, Habari na Harakati. Sifuati mkumbo. Napenda kuhoji na kudadisi - hulka ya kifalsafa ya kuusaka ukweli - 'UKWELI ULIO UCHI.'