Wednesday, February 15, 2006

Nimerejea ulingoni

WAPENDWA wanablogu, nilipotokomea sikuaga, kwa sababu haikuwa nia yangu kujitenga nanyi. Sasa nimerejea. Kwa muda nilikuwa mafichoni. Baadhi ya walionikosa kwenye blogu walitumia njia nyingine za kuwasiliana nami, wakahoji kama niko uhamishoni! Hata bila kujibu nilikuwa wapi, nafurahi kuwatangazia maswahiba wote kwamba sasa nimo ulingoni. Nimefurahi kuwakuta wanablogu wapya, kina Jeff Msangi (niliyemuathiri binafsi kuingia kwenye blogu) wakiwa wanatamba. Picha za Muhidin Issa Michuzi zimekuwa kivutio kingine. Hoja tekenyo za Reginald Simon zimekuwa kiburudisho kikubwa, bila kusahau hoja nyeti za painia Ndesanjo Macha. Nakiri kwamba nilikosa mengi katika muda niliokuwa mbali na wanablogu. Yawezekana pia nimewanyima machache kadhaa niliyokuwa nayo. Tafadhari mnisamehe. Sasa nimerejea.
My photo
Nimechongwa na mambo haya: Falsafa, Fasihi, Muziki, Habari na Harakati. Sifuati mkumbo. Napenda kuhoji na kudadisi - hulka ya kifalsafa ya kuusaka ukweli - 'UKWELI ULIO UCHI.'