Monday, December 14, 2009

Waitaliano wambonda Waziri Mkuu wao

Nilipoandika kujadili tukio la msafara wa Rais Jakaya Kikwete kurushiwa mawe mkoani Mbeya, mwandishi mmoja aliandika kunijibu akisema, 'Ansbert, rais hapigwi mawe.' Hata hivyo, tayari rais alikuwa ameshapigwa mawe! Lakini wakati ule sikujua pia kwamba wapo wenzetu ambao wameshavuka enzi za mawe, sasa wanarusha hata makonde kwa 'marais' wao. Tazama Waitaliano walimvyomtwanga na kumtoa damu Waziri Mkuu wao, Silvio Berlusconi. Nadhani dunia ya kisiasa inabadilika kwa kasi ya ajabu!
My photo
Nimechongwa na mambo haya: Falsafa, Fasihi, Muziki, Habari na Harakati. Sifuati mkumbo. Napenda kuhoji na kudadisi - hulka ya kifalsafa ya kuusaka ukweli - 'UKWELI ULIO UCHI.'