Friday, July 09, 2010

Dk. Shein apeta

CCM Zanzibar wamepata mgombea urais. Matokeo ya kura za NEC Dodoma yanasema hivi: Shein 117: Bilal 54: Nahodha 33.

Hata hivyo, taarifa kutoka ndani ya vikao vya CCM zinasema Dk. Bilali alipata kura 119 kutoka wa wajumbe. Akafuatiwa na Dk. Shein (63) na Nahodha (22). Hayo ndiyo maajabu ya CCM, ma ndiyo maana Wazanzibari hawakosi kulalamikia kitendo cha rais wao kuchaguliwa Dodoma badala ya Zanzibar. Na hivi ndivyo Dk. Bilali alivyozibwa mdomo kwa kupewa nafasi asiyoitaka ya kuwa mgombea mwenza wa JK.

No comments:

My photo
Nimechongwa na mambo haya: Falsafa, Fasihi, Muziki, Habari na Harakati. Sifuati mkumbo. Napenda kuhoji na kudadisi - hulka ya kifalsafa ya kuusaka ukweli - 'UKWELI ULIO UCHI.'