
Nina hoja mbili. Kwanza, tuwe na rais wa kukaa mdarakani miaka mitano badala ya miaka kumi. Pili, tukubali kwamba maendeleo tunayotaka kuyafanya hayawezekani kama hatutakubali kuanza sasa kufanya mapinduzi. Wengine wana shaka, na wengine wanadhani haiwezekani. Lakini kama iliwezekana kwa Warumi, (mtazame Kaizari Julius pichani na utafakari yaliyomkuta) itashindikanaje kwa Watanzania? Na je, kushuka kwa umaarufu wa Kikwete kwaweza kuwa ishara mojawapo ya mwanzo mpya? Au ndiyo wanaanza kujifunza Afrika Kusini na Kenya, kujitambua na kugundua makosa?Tujadiliane.