Sunday, September 07, 2008

Nipo Highway Africa

Wiki (6.9.2008 - 13.9.2009) hii nitakuwa Afrika Kusini, katika Chuo Kikuu cha Rhodes, kuhudhuria kongamano la kila mwaka la Highway Africa linalojadili matumizi ya teknolojia za kisasa katika kukuza mawasiliano na kuboresha maisha. Mada kuu ya mwaka huu ni Uandishi wa Kiraia: Uandishi kwa Manufaa ya Raia. Wapo Watanzania kadhaa nimekutana nao hapa, wakiwamo Mhariri Mtendaji wa Mwananchi, Theophil Makunga; Mtangazaji wa DTV, Dina Chahali; Mpiga picha na mwanablogu, Philemon Msangi (Bob Sankofa); Mwandishi anayeibukia, Furaha Thonya; Mhariri wa Mtanzania Jumapili, Eric Anthony na Ofisa Uhusiano wa CRDB, David Mbulumi. Habari zaidi za Highway Africa zinapatikana hapa. Sikiliza na matangazo mafupi ya redio kuhusu dhana ya mkutano.

1 comment:

Anonymous said...

Kzi njema

My photo
Nimechongwa na mambo haya: Falsafa, Fasihi, Muziki, Habari na Harakati. Sifuati mkumbo. Napenda kuhoji na kudadisi - hulka ya kifalsafa ya kuusaka ukweli - 'UKWELI ULIO UCHI.'