Monday, September 15, 2008

Zimbabwe kama Kenya


Mahasimu wa kisiasa nchini Zimbabwe, Rais Robert Mugabe na Kiongozi wa Upinzani, Morgan Tsvangirai, wamesaini makubaliano ya kugawana madaraka - baada ya usuluhishi uliofanywa na Rais wa Afrika Kusini, Thabo Mbeki. Mugabe ataendelea kuwa rais na mkuu wa nchi, huku Tsvangirai akiwa Waziri Mkuu na msimamizi wa Baraza la Mawaziri. Hata hivyo, hotuba za viongozi hao mara baadaya kusaini makubaliano hayo, zinaonyesha waziwazi tofauti walizonazo. Msikilize Mugabe hapa; na Tsvangirai hapa.

No comments:

My photo
Nimechongwa na mambo haya: Falsafa, Fasihi, Muziki, Habari na Harakati. Sifuati mkumbo. Napenda kuhoji na kudadisi - hulka ya kifalsafa ya kuusaka ukweli - 'UKWELI ULIO UCHI.'