Friday, April 03, 2009

Vituko vya kidiplomasia vya Berlusconi


Wapo viongozi wa nchi wanaofahamika kwa vituko vya kidiplomasia. Kwa Ulaya, nadhani Waziri wa Italia, Silvio Berlusconi, anaongoza. Mwaka 2005 aliiudhi serikali ya Finland kwa 'mizaha ya kitoto' aliyomfanyia rais Tarja Halonen. Mwaka mmoja baadaye aliingia kwenye mgogoro na serikali ya China baada ya kudai kwamba chini ya utawala wa Mao Zedong, Wachina walikuwa 'wanachemsha watoto wachanga.' Kuna wakati aliwahi kuangusha kichwa cha mimbari mbele ya Rais George Bush na waandishi wa habari. Aliwahi kutoa kauli tete juu ya rangi ya ngozi ya Barack Obama, mara alipochaguliwa Novemba mwaka 2008 kuwa rais wa Marekani. Mwaka jana alimchezea Kansela wa Ujerumani, Angela Merkel, mchezo ule ujulikanao kama 'hide-and-seek.' Hata juzi akiwa jijini London kwenye mkutano wa G20, Berlusconi alipayuka hadharani akimuita Rais Obama mara baada ya kupiga picha ya pamoja na Malikia wa Uingereza, Elizabeth II, jambo ambalo hata malkia mwenyewe anasemekana hakulipenda! Ikumbukwe kuwa huko nyuma aliwahi kujikuta kwenye mzozo na Wajerumani kwa utani wa KINAZI dhidi ya mbunge mmoja wa Ujerumani. Aliwahi pia kumsifia waziri Mkuu wa Denmark kuwa ni handsome kuliko viongozi wote wa Ulaya! Hata majuzi katika mkutano wa NATO alichelewesha ufunguzi wa mkutano huo baada ya kuganda kwenye simu nje ya ukumbi, huku mmoja wa wenyeji wa mkutano, Merkel, akimsubiri bila mafanikio. Mtazame hapa. Una kituko kingine cha Berlusconi au kigogo yeyote? Kwa Afrika ni kiongozi gani 'anasifika' kwa vituko vya kidiplomasia?

1 comment:

Mzee wa Taratibu said...

Nafikiri huyu jamaa hua hazimtoshi maana vituko vyake hachugui sehemu popote pale.

My photo
Nimechongwa na mambo haya: Falsafa, Fasihi, Muziki, Habari na Harakati. Sifuati mkumbo. Napenda kuhoji na kudadisi - hulka ya kifalsafa ya kuusaka ukweli - 'UKWELI ULIO UCHI.'