Saturday, July 11, 2009

Obama anatazama nini?


Macho ya Rais Barack Obama yanatazama nini? Ndiye pekee anayeweza kujua. Lakini haituzuii kufuatilia na kujadili.

4 comments:

Subi Nukta said...

(wacha nijaribu) nadhani alikuwa akisubiri mkono wa dada aliyeko nyuma yake akawa hauoni akageuka kidogo kama kuupokea wakati huyo dada mwingine anapita basi ndo hata taswira ionekane kama vile anamtizama huyu mdada anayeelekea kule... sijui lakini alikuwa akitizama nini kwa hakika, yeye ndo ana ukweli rohoni mwake...
na huyo wa Ufaransa sijui alipatwa na butwaa ya kuona nini haswa, sijui kwa kweli hawa waitu...

Mzee wa Changamoto said...

Obama alikuwa akishuka na hiyo picha iliyoonekana kuzusha maswali mengi kuliko majibu kwa upande wa Obama imeeleweshwa na Video hii inayopatikana http://www.youtube.com/watch?v=-kKK66gpVLo ambapo yaonesha kuwa Obama hakuna na mpango na kile kinachoonekana kuangaliwa hapo, japo swali bado labaki kwa Rais wa Ufaransa.
Tazama hiyo Video kujibu swali hili muhimu.

Anonymous said...

hii picha imetengenezwa,that gal amewekwa hapo from other events,kuna kampeni kubwa inafanywa na wazungu wabaguzi wa marekani kumchafua Barack Obama, na kuonesha dunia kuwa black can not do it better like white .
and this and other photoz like this intend to do the same!
weusi tuamkeni kumekucha!
jingo.

Anonymous said...

Duh, kweli watu mnafuatilia, sikufikilia kama itaweza kuwa imetengenezwa kama jamaa hapo juu alivodai. Mi nlihisi Mr President amemuangalia tu huyo mdada. Sasa na Srkozy nae mbona anacheka na kujishika kama asiye na kazi ? Amekaa ki'mea mbea sana hapo !
Nsajigwa.

My photo
Nimechongwa na mambo haya: Falsafa, Fasihi, Muziki, Habari na Harakati. Sifuati mkumbo. Napenda kuhoji na kudadisi - hulka ya kifalsafa ya kuusaka ukweli - 'UKWELI ULIO UCHI.'