My Photo
Ansbert Ngurumo
Maisha yangu yamezungukwa na kuchongwa na Falsafa, Fasihi, Muziki, Habari na Harakati. Sifuati mkumbo; siogopi wala kupendelea au kubagua binadamu yeyote. Tatizo langu: sivumilii ujinga na sina utii wa kikondoo kwa wenye mamlaka. Kuhoji na kudadisi ni sehemu ya maisha yangu itokanayo na hulka ya kifalsafa ya kuusaka ukweli - 'UKWELI ULIO UCHI.'
View my complete profile

Tuesday, June 23, 2009

Uingereza wapata Spika mpinzani

Baada ya Spika wa awali kujiuzulu kwa kashfa, Bunge la Uingereza limechagua Spika mpya John Bercow (46) ambaye anatoka chama cha upinzani cha Conservative. Mtazame hapa akitambulishwa na kutambuliwa rasmi baada ya kupata baraka za Malkia; na hapa akikubali majukumu ya kazi yake mpya n akuwashukuru wabunge. Hizi hapa ni hotuba za viongozi wa vyama vikuu Bungeni: 1. Waziri Mkuu , Gordon Brown (Labour). 2. Kiongozi wa Upinzani , David Cameron (Conservative). 3. Kiongozi wa chama cha upinzani , Nick Clegg( Lib Dem). Msikilize Spika mpya akimnanga mbunge mzee aliyekataa kumuunga mkono kwa kigezo cha umri. Huu ndiyo utaratibu wa kumpata Spika wao.