Wednesday, November 29, 2006

Kura Za Mzee Wa Kombati Zilikwenda Wapi?


CCM walidai kwamba Mbowe alipata watu wengi kwenye kampeni kwa sababu watu walikwenda kushangaa helikopta. Nikiitazama picha hii naona jambo tofauti. Helikopta ipo uwanjani lakini hawaitazami. Wameiacha nyuma, wanamkodolea macho Mbowe (hayupo pichani). Tazama nyuso zao. Waliofuatilia kampeni zake wanajua hali ilikuwa hivyo kila mkutano wake wa kampeni Oktoba - Desemba 2005. Tazama mmoja wa washindani wake. Nimesikia watu wakijiuliza. Nami najiuliza. Na sasa nawauliza nyie wasomaji. Tuulizane. Hivi kura za Mbowe zilikwenda wapi?

1 comment:

Anonymous said...

Huwajui CCM, nini! Na ujinga wa umma ulichangia. sasa walichochagua kiko wapi? Bomu, bomu!

My photo
Nimechongwa na mambo haya: Falsafa, Fasihi, Muziki, Habari na Harakati. Sifuati mkumbo. Napenda kuhoji na kudadisi - hulka ya kifalsafa ya kuusaka ukweli - 'UKWELI ULIO UCHI.'