Monday, February 19, 2007

'Mchemsho' wa Uhuru: Uingereza yawa Marekani


JUMAMOSI Februari 17, 2007 Rais Jakaya Kikwete alikuwa nchini Uingereza na alikutana na badhi ya Watanzania waishio nchini humo na kuzungumza nao. Cha kushangaza, gazeti la Uhuru linalomilikiwa na Chama Cha Mapinduzi (CCM) ambacho yeye ni mwenyekiti, lilitumia picha zake na kuwaeleza Watanzania na dunia nzima kwamba Rais alikuwa Marekani, na kwamba Balozi wa Tanzania nchini Marekani ni Mwanaidi Maajar. CAPTION ya picha unayoona hapa iliyotumika katika tovuti ya gazeti la Uhuru 19.02.2007 ilisema hii:
RAIS Jakaya Kikwete akisisitiza jambo alipozungumza na Watanzania waishio Marekani, kwenye hoteli ya London's Royal, juzi Kushoto ni mke wa Rais, Mama Salma Kikwete na kulia ni balozi wa Tanzania nchini Marekani, Mwanaidi Maajar. (Picha na Freddy Maro).

No comments:

My photo
Nimechongwa na mambo haya: Falsafa, Fasihi, Muziki, Habari na Harakati. Sifuati mkumbo. Napenda kuhoji na kudadisi - hulka ya kifalsafa ya kuusaka ukweli - 'UKWELI ULIO UCHI.'