Saturday, September 18, 2010

Kampeni ya Dk. Slaa: Mpya Mpya Katika Picha



Mchumba wa Dk. Slaa, Josephine, akisalimia wananchi wa Karatu mkutanoni, juzi Alhamisi.



Dk. Slaa hatumii shangingi. Hiki ndicho kipanya anachotumia katika ziara zake za kampeni. Katika picha hii, wananchi wa Arusha Mjini wanasukuma kipanya hicho kuondoka viwanja vya mkutano kuelekea hotelini jana Jumamosi jioni.




Jina la shabiki huyu wa Dk. Slaa halikupatikana mara moja. Ni mkazi wa Arusha Mjini.




Dk. Willibrod Slaa, akimnadi mgombea wa ubunge katika jimbo la Karatu kupitia chama hicho, ambaye anatarajiwa kuwa mrithi wake wa ubunge jimboni humo, Mchungaji Israel Natse, wakati wa mkutano wa hadhara wa kampeni, uliofanyika kwenye Uwanja wa Bwawani mjini Karatu jana Ijumaa



Dk. Willibrod Slaa, akizungumza na Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Shinyanga, Daudi Siasi, mara baada ya kuhutubia mkutano wa kampeni zake kwenye Uwanja wa Sabasaba mjini Bariadi juzi Alhamisi.



Bendera za mashabiki Musoma Mjini: Dk. Slaa ni chaguo la vyama vyote



Wananchi Musoma: Dk Slaa ni Taa Mpya

No comments:

My photo
Nimechongwa na mambo haya: Falsafa, Fasihi, Muziki, Habari na Harakati. Sifuati mkumbo. Napenda kuhoji na kudadisi - hulka ya kifalsafa ya kuusaka ukweli - 'UKWELI ULIO UCHI.'