Monday, October 23, 2006

Walimu mavumbini, wanafunzi wanaozwa


Haya jamani. Ona shule zetu zilivyo, miaka 45 baada ua uhuru. Yameenea nchi nzima. Wakubwa wanajisifu, na wanayataja na haya kama mafanikio ya MMEM. Haya yanatokea pia kwingine katika hali tofauti. Hata Dar es Salaam yapo, mita chache kutoka nyumbani na ofisini kwa Rais, Ikulu. Na hili la wanafunzi kujisaidia vichakani katika karne ya 21 tunaizungumziaje? Eti na ukosefu wa VYOO unasababisha shule kufungwa; huku baadhi ya walimu wakiiba fedha za MMEM. Huko Musoma, wanafunzi 600 wanasota. Ndiyo maana hata wazazi hawaamini kwamba watoto wao wasiojua hata kuandika majina yao wameshinda mtihani wa darasa la saba na kuchaguliwa kwenda sekondari. Tuko makini kweli? Si hivyo tu. Wazee hawa maskini, wamefungwa jela kwa sababu serikali imeshindwa kujenga shule, na inawalazimishwa wachangie hata kama hawana pesa!

No comments:

My photo
Nimechongwa na mambo haya: Falsafa, Fasihi, Muziki, Habari na Harakati. Sifuati mkumbo. Napenda kuhoji na kudadisi - hulka ya kifalsafa ya kuusaka ukweli - 'UKWELI ULIO UCHI.'