Friday, August 31, 2007

Hekalu la Manji?

Bwana ee! Tazama nyumba hii. Lakini Waswahili wanasema imevuka viwango vya kuitwa nyumba. Hili ni Hekalu. Na hizi hapa chini ni sehemu chache za hekalu hilo. La nani? Aliyetuma hizi ni la Yusuf Manji - yule mfadhili wa Klabu ya Yanga; "mgomvi" wa Regi Mengi (na sasa hivi Waislamu kuhusu kiwanja); mfadhili wa Chama Cha Mapinduzi (CCM); lakini mmoja wa wasomaji wa blogu hii anasema si kweli bali ni nyumba ya Rais Pervaiz Musharaf, mtu aniyejipenda kweli kweli, mchezaji hodari wa Badminton, Jenerali wa Pakistani. Iwe ya yeyote yule, inapendeza na kuvutia. Tazama!

5 comments:

Anonymous said...

Ansbert,
Nilipost comment lakini naona umeamua kuindoa kwa sababu zako.
Narudia tena, "Hilo jumba unaloliita la Manji Sio, nisingependa ndugu yetu uingie matatizoni kwa kuandika habari za UONGO".
Habari unazoandika ni za juzi ya juzi. Jumba limeshajulikana ni la President Musharaff.
Hii fitna ndugu yangu itakufikisha pabaya...

Ansbert Ngurumo said...

Ndugu yangu, nimekusikia. Sikuwa na lengo baya na Manji. Ndiyo maana hata headline yenyewe ina alama ya kuuliza. Hekalu la Manji? Lakini baada ya comment zako, niligundua makosa katika maandishi yangu. Nimeyarekebisha. Stori yangu ni uzuri wa nyumba, si nani anaimiliki. Maana inawezekana wala si ya Musharaf!

Ansbert Ngurumo said...

Ndugu yangu, asante kwa ushauri. Tangu awali, sikuwa na nia mbaya na Manji. Ndiyo maana nimetanguliza alama ya kuuliza katika headline. Nimegundua pia, baada ya ushauri wako, kwamba sikuwa nimeweka vema maelezo yangu chini ya picha. Nimeyarekebisha, na swali limebaki lile lile. Kwangu, stori ni uzuri wa nyumba, si nani anaimiliki; maana yawezekana wala si Manji wala Musharaf. Asante.

Anonymous said...

Kiasi cha fedha zetu za pension funds alizotutapeli Manji anaweza kuwa na hekalu zaidi la hili kwenye picha kwani nani anafahamu jinsi alivyoficha hiyo "loot" yake?.

Anonymous said...

ndugu ngurumo,
ANON wa hapo juu ni nani mbona ameonekana kuguswa sana na hiyo habari,na tahadhari anayokupa inathibitisha kauli aliyowahi kuitoa mzee regnald mengi dhidi ya manji kuwa kila aliyesikia ugomvi baina yao alimtahadharisha mzee mengi kuwa maisha yake yapo hatarini kwani manji ni mtu hatari,
hivyo baada ya kusoma hiyo tahadhari hapo juu nimemkumba mzee mengi siku hiyo kwenye taharifa ya habari ya itv akilalamika kuhusu manji.

awali ya yote manji ni miongoni mwa wabadhirifu wakubwa wa fedha za IMPORT SUPPORT,KAMPUNI ZA KITAPELI,NSSF na PPF kupitia biashara za majengo hivyo anaweza kuwa na jumba zaidi ya hilo tena hata lenye viwanja vya ndenge na boti za starehe .

My photo
Nimechongwa na mambo haya: Falsafa, Fasihi, Muziki, Habari na Harakati. Sifuati mkumbo. Napenda kuhoji na kudadisi - hulka ya kifalsafa ya kuusaka ukweli - 'UKWELI ULIO UCHI.'