
Taarifa nilizopata sasa hivi (28.07.2008 saa 3:15 usiku) kwa simu kutoka kwa Mhariri wa RAI, Deodatus Balile, Tanzania, ni kwamba mpambanaji, Mbunge wa Tarime, Chacha Wangwe, (pichani kushoto) amefariki dunia katika ajali ya gari maeneo ya Panda Mbili akitokea Bungeni Dodoma njiani kuelekea Dar es Salaam. Mungu ailaze roho yake mahali pema peponi. Amin! Kwa habari zaidi za kifo chake SOMA hapa.