Tuesday, July 01, 2008

Kikwete na wenzake wamshindwa Mugabe

Mkusanyiko wa marais wa Afrika uliotarajiwa kumdhibiti Rais wa Zimbabwe Robert Mugabe kuhusu uchaguzi wake wenye utata umeshindwa kumdhibiti wala kumkemea. Wakati jumuiya ya kimataifa inafanya kila liwezekanalo kumwekea Mugabe vigezo kwa kuongoza nchi yake kidikteta, viongozi wetu wa Umoja wa Afrika (AU) wamemuita shujaa. Hii ni aibu kwa Bara la Afrika.

No comments:

My photo
Nimechongwa na mambo haya: Falsafa, Fasihi, Muziki, Habari na Harakati. Sifuati mkumbo. Napenda kuhoji na kudadisi - hulka ya kifalsafa ya kuusaka ukweli - 'UKWELI ULIO UCHI.'