Saturday, March 21, 2009

Papa Benedicto XVI na Kondomu

KAULI ya hivi majuzi ya Papa Benedicto XVI kupinga matumizi ya kondomu katika vita ya UKIMWI imezua mjadala mpya, huku wengine wakimlaani kwamba anakwamisha mafanikio ya jitihada za kupambana na maambukizi ya UKIMWI na kwamba hakupaswa kutoa kauli hiyo. Wengine wamemkosoa kwamba si kweli kwamba matumizi ya kondomu yanaongeza kasi ya maambukizi ya UKIMWI kwa sababu taarifa za kitafiti zinaonyesha umuhimu wa kondomu katika kuzuia maambukizi. Hata hivyo, taarifa hizo hizo zinadai kwamba kinga ya kutumia kondomu si ya asilimia 100.

Lakini Papa ni kiongozi wa dini, na ujumbe wake unazingatia maadili yanayosimamiwa na madhehebu ya imani yake. Kama huo ndiyo msimamo wa kanisa lake, tulitarajia aseme nini? Ahubiri nini? Asiposema hayo aliyosema atakuwa Papa tena? Na kama kondomu haizuii kwa asilimia 100 Papa amekosea nini?

2 comments:

Reggy's said...

Kwani Papa haogopi kupigwa kofi kama Mwinyi? Thubutu!

Anonymous said...

Ni Kweli, Papa alisema msimamo wake, wa kanisa lake! Hakukosea.

Msemakweli.

My photo
Nimechongwa na mambo haya: Falsafa, Fasihi, Muziki, Habari na Harakati. Sifuati mkumbo. Napenda kuhoji na kudadisi - hulka ya kifalsafa ya kuusaka ukweli - 'UKWELI ULIO UCHI.'