Monday, June 09, 2008

Mtanzania afariki Italia


Raia mmoja wa Tanzania, Omar Jaffar Ngwaya (pichani), amefariki dunia leo Jumatatu Juni 09, 2008, nchini Italia kwa ajali ya gari. Kwa mujibu wa Katibu wa Jumuiya ya Watanzania waishio nchini Italia, Kaguta NM, mipango ya mazishi ya marehemu Ngwaya inafanyika kwa kushirikiana na Balozi wetu nchini Italia. Taarifa za nyongeza zinapatikana katika tovuti hiyo hapo juu. Mungu ailaze roho yake mahali pema peponi! Amina!

1 comment:

Anonymous said...

Poleni Watz wenzetu mlio Itali, ndugu na jamaa wa marehemu popote mlipo.

My photo
Nimechongwa na mambo haya: Falsafa, Fasihi, Muziki, Habari na Harakati. Sifuati mkumbo. Napenda kuhoji na kudadisi - hulka ya kifalsafa ya kuusaka ukweli - 'UKWELI ULIO UCHI.'