Friday, August 06, 2010

Dk. Slaa afunika Moshi


Sehemu ya umati wa wakazi wa mji wa Moshi, wakisikiliza hotuba ya mgombea urais wa Jamhuri ya Muungano kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Dk. Willibrod Slaa (hayupo pichani), wakati wa mkutano wa kuomba udhamini, kwenye Uwanja wa Manyema mjini Moshi 05/08/2010. (Picha zote na Joseph Senga)


Mgombea urais wa Jamhuri ya Muungano, kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Dk. Willibrod Slaa, akihutubia katika mkutano wake wa hadhara wa kuomba kudhaminiwa, uliofanyika kwenye Uwanja wa Manyema mjini Moshi 05/08/2010.


Mwenyekiti wa CHADEMA), Freeman Mbowe, akihutubia maelfu ya wakazi wa mji wa Moshi, katika mkutano wa hadhara wa kuomba udhamini wa mgombea urais wa chama hicho, Dk. Willibrod Slaa, uliofanyika kwenye Uwanja wa Manyema mjini Moshi 05/08/2010.


Msafara wa mgombea urais kupitia CHADEMA, Dk. Willbrod Slaa, ukipita katikati ya mji wa Moshi, mara baada ya kuwasili kwenye Uwanja wa ndege mjini humo, ambako alihutubia mkutano wa hadhara wa kuomba kudhaminiwa, kwenye Uwanja wa Manyema jana, huku ukisindikizwa na helikopta (juu) 05/08/2010.


Makamu Mwenyekiti wa CHADEMA, Said Arfi, akihutubia maelfu ya wakazi wa mji wa Moshi na vitongoji vyake, katika mkutano wa hadhara wa kuomba udhamini kwa mgombea urais kupitia chama hicho, kwenye Uwanja wa Manyema 05/08/2010.

No comments:

My photo
Nimechongwa na mambo haya: Falsafa, Fasihi, Muziki, Habari na Harakati. Sifuati mkumbo. Napenda kuhoji na kudadisi - hulka ya kifalsafa ya kuusaka ukweli - 'UKWELI ULIO UCHI.'