Friday, August 06, 2010

Kikwete aogopa mdahalo tena

KAMA alivyofanya mwaka 2005, mgombea urais kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), Rais Jakaya Kikwete, ameogopa mdahalo na wagombea urais wenzake kutoka vyama vya upinzani. Taarifa ya Kikwete kuogopa mdahalo huo ilitolewa na Katibu Mkuu wa CCM, Yusuph Makamba na Naibu Mkuu wa Kitengo cha propaganda wa CCM, Tambwe Hiza, jana Agosti 05/08/2010, Dar es Salaam. Kikwete anakimbia mdahalo huo wakati maandalizi yakiendelea, huku mgombea wa Chama cha Wananchi (CUF) Prof. Lipumba na mgombea wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) Dk. Willibrod Slaa wakisisitiza kuwa wanataka mdahalo huo ili wananchi wawapime kwa hoja. Hata hivyo, kukimbia kwa Kikwete hakutazuia mdahalo kuendelea. Wenzake watapewa fursa hiyo adhimu, na iwapo watamjadili in absentia atakuwa amepoteza fursa muhimu sana ya kujenga hoja na kujitetea kwa hoja zinazoelekezwa kwake na chama chake. Mwaka jana, aliyekuwa Waziri Mkuu wa Uingereza, Gordon Brown wa Uingereza alianza kwa kukataa kushiriki mdahalo (ambao ulifanyika mwaka huu), lakini baadaye alikubali na kushiriki, na alifanya vizuri, ingawa hatimaye hakushinda uchaguzi. Lakini kwa jinsi washindi (Conservative) walivyokosa kura za kutosha kuunda serikali peke yao kama walivyotarajiwa, ni ishara kwamba mdahalo na utendaji wake waktia masuala mengine, hasa uchumi, vilimwinua Brown, akaungwa mkono na sehmu kubwa ya umma uliokuwa unambeza awali. Je, Kikwete ataendelea kuogopa na kupoteza fursa hii?

1 comment:

Anonymous said...

Kwa kukimbia mdahalo, Kikwete anakimbia kivuli chake mwenyewe.

My photo
Nimechongwa na mambo haya: Falsafa, Fasihi, Muziki, Habari na Harakati. Sifuati mkumbo. Napenda kuhoji na kudadisi - hulka ya kifalsafa ya kuusaka ukweli - 'UKWELI ULIO UCHI.'