Thursday, August 19, 2010

Mtikila akosa sifa kugombea urais


Mwenyekiti wa DP, Mchungaji Christopher Mtikila, ambaye alichukua fomu kugombea urais wa Tanzania, ameondolewa kwenye orodha ya wagombea urais. Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) imesema kwamba Mtikila alikosa sifa. Hakupata wadhamini kutoka mikoa 10 kama sheria inavyotamka. Mtikila aliwasili ofisi za NEC saa 10 jioni, kwa mbwembwe, kabla ya kupata habari mbaya, ambazo hata hivyo, kwa kuwa hakuwa amepata wadhamamini alizitarajia. Katika picha hii, Mtikila alikuwa anahutubia 'umati' ulikusanyika kumsikiliza katika viwanja vya Jangwani, Dar es Salaam, mwaka 2005 alipogombea urais. Wagombea mwingine ambao hawakutimiza masharti ni Paul Kyara wa SAU na wa Jahazi Asilia na Demokrasia Makini. Mgombea wa Demokrasia Makini na wa NRA hawakutokea kabisa kurejesha fomu.

Wagombea urais waliobaki hadi sasa ni Dk. Willibrod Slaa (CHADEMA); Prof. Ibrahim Lipumba (CUF); Jakaya Kikwete (CCM); Hashim Rungwe (NCCR-Mageuzi); Mutamwega Mgaywa (TLP); Sahma Dovutwa (UPDP); na Peter Kuga Mziray (APPT-Maendeleo).

No comments:

My photo
Nimechongwa na mambo haya: Falsafa, Fasihi, Muziki, Habari na Harakati. Sifuati mkumbo. Napenda kuhoji na kudadisi - hulka ya kifalsafa ya kuusaka ukweli - 'UKWELI ULIO UCHI.'