Wednesday, August 25, 2010

Helikopta ya Kikwete yashindwa kutua


MWANABIDII mmoja, Leila Abdul, ameripoti kuwa helikopta inayombeba mgombea urais kupitia CCM Jakaya Kikwete, leo majira ya saa 10 imeshindwa kutua Ngara, mkoani Kagera, kutokana na hali ya hewa kutokuwa nzuri. Kwa sababu hiyo, mkutano uliopaswa kufanyika wilayani hapo uliahirishwa hadi kesho

"Kutokana na hali hiyo imembidi mwenyekiti wa CCM wilayani Ngara Hellena Adrian alilazimika kuwataarifu wananchi kuwa mkutano huo hautafanyika ikiwa ni majira ya saa 11:30 jioni na kueleza kuwa badala yake mkutano huo utafanyika kesho majira ya saa 2: 00, na kubainisha kuwa Kikwete amelazimika kusafiri kwa magari," aliandika Leila, katika waraka uliosambazwa kwa wanabidii wote.

No comments:

My photo
Nimechongwa na mambo haya: Falsafa, Fasihi, Muziki, Habari na Harakati. Sifuati mkumbo. Napenda kuhoji na kudadisi - hulka ya kifalsafa ya kuusaka ukweli - 'UKWELI ULIO UCHI.'