Friday, September 07, 2007

Naenda Bondeni

Wiki hii nitakuwa Bondeni kushiriki mkutano wa Highway Africa na wanahabari wengine kutoka pande mbali za Afrika na kwingineko duniani. Mojawapo ya majukumu yangu huko ni kuzungumzia uandishi mpya wa kijamii katika mkusanyiko ujulikanao kama Digital Citizen Indaba siku moja kabla ya mkutano wenyewe, ambako pia nitashiriki kujadili mada ya kublogu, nikiwa pia na gwiji wa kublogu, mwanablogu nambari wani wa Kiswahili, Ndesanjo Macha na wadu wengine. Msiwe mbali na blogu.

No comments:

My photo
Nimechongwa na mambo haya: Falsafa, Fasihi, Muziki, Habari na Harakati. Sifuati mkumbo. Napenda kuhoji na kudadisi - hulka ya kifalsafa ya kuusaka ukweli - 'UKWELI ULIO UCHI.'