Sunday, September 02, 2007

Ndimara Tegambwage afungua blogu


Mwandishi mkongwe wa vitabu na magazeti; mchambuzi mahiri na mjenzi makini wa hoja kali; mmoja wa waasisi wa mageuzi ya vyama vingi nchini; mbunge mstaafu wa Muleba Kaskazini; Ndimara Tegambwage, anayeandika safu ya SITAKI (na hii hapa mpya) katika gazeti la Tanzania Daima Jumapili, ameingia katika ulimwengu wa blogu. Jina lenyewe la blogu ni dalili tosha kwamba kishindo chake kitakuwa kikubwa.

Wanablogu wengi ninaowajua ni vijana. Wazee wengi wa rika la Ndimara wamekuwa waoga wa teknolojia. Lakini Ndimara hazeeki. Hata katika dotikomu naye yumo. Na kwa wanaomfahamu, Ndimara ni kijana kuliko vijana wengi tulionao, waliozeeka kabla ya wakati wao. Msome hapa.


1 comment:

Anonymous said...

karibu mzee Ndimara. Tutakusoma sana.

My photo
Nimechongwa na mambo haya: Falsafa, Fasihi, Muziki, Habari na Harakati. Sifuati mkumbo. Napenda kuhoji na kudadisi - hulka ya kifalsafa ya kuusaka ukweli - 'UKWELI ULIO UCHI.'