Monday, September 17, 2007

Salva Rweyemamu ateuliwa mkurugenzi Ikulu


Salva Rweyemamu (pichani), aliyekuwa mkurugenzi wa Habari Corporation, ameteuliwa na Rais Jakaya Kikwete kuwa Mkurugenzi wa Kitengo cha Mawasiliano Ikulu. Anaziba nafasi iliyoachwa wazi na Balozi Peter Kallaghe aliyepelekwa Canada. Mwingine anayeonekana pichani kulia ni Dk. Gideon Shoo. Picha: Issa Michuzi

23 comments:

Anonymous said...

Hongera Salva uwezo wako tunaujua, msaidie JK kutimiza ahadi zake, lakini usiingie kwenye dhambi ya kutetea uoza wa serikali. Wakikutuma kusema uwongo kacha. heri urudi kwenye ajira yako binafsi kuliko kufanyw akibarua msema uwongo.

Anonymous said...

Tunasubiri kuona utaanza na nini maana mambo mengi yako shagalabaghala.

Anonymous said...

Mambo ya Mtandao hayo...hivi huyu jamaa si ndio alishiriki katika kuua himaya ya Generali Ulimwengu na Habari Corporation yake ambayo sasa inamilikiwa na Mwanamtandao nambari moja Rostam? Ambapo sasa yemekuwa magazeti ya udaku, badala ya hoja? Yetu macho!

Anonymous said...

ndiye huyu bingwa mpya wa propaganda za CCM ya Mtandao. Tulijua angepewa nafasi hiyo maana aliwasaidia sana kuingilia vyombo vya habari na kujipenyeza kwa umma, ila walimchelewesha kupoteza maboya. Wenzetu bado wanapangana, kazi haijaanza, na muda unakaribia kufika katikati. wapi maisha bora?

Anonymous said...

Sawa kabisa bi Salma huyu ndiye Spin Doctor wa mtandao sasa imebidi wamzawadie kwa kazi nzuri ya upigaji debe wake wakati wa mchakato. Nadhani huko Ikulu ataendelea kumwambia Jakaya kuwa kavaa nguo kumbe yuko uchi!! Nasema hivyo kwasababu ndiyo kazi aliyokuwa anafanya siku za karibuni kwa kupindisha ukweli kuwa mambo yako swali PSRC aliko mwanantandao maslahi mwingine , kumbe huku anauza viwanja na mali za umma bila kufuata utaratbu na kwa bei poa. Umamluki si kitu cha heshima, kwasababu mtu unauza utu wako.!!

Anonymous said...

Nakumbuka wakati ule wa uchagusi alijifanya kuwa anawachambua wagombea wote wa urais. Akawaponda wote (akina Salim, Sumaye etc) kisha wa mwisho akamsifu na kumsifu na kumkuza JK. Bila ya aibu wala kufuata maadili ya uandishi!! Kweli kazawadiwa kwa kazi nzuri ya kutetea mtandao!
Na hii kampuni yake ya S & G ni Salva and Gideon Shoo wakishirikiana na Prince Bagenda. Waliajiriwa na Ikulu !

Anonymous said...

Makubwa! Kumbe ndiyo maana Bagenda alikuwa analumbana na Ngurumo alipoambiwa anaomba kazi! Nasikia naye (Bagenda) anasubiri kuteuliwa na JK kuwa DC...

Anonymous said...

hawa walinunuliwa(HABARI CORPORATION LIMITED) kwenye uchaguzi mkuu na sasa wanalipwa fadhila kwa kufanikisha ushindi wa wanamtandao.
Inasikitisha sana kwani ni waandishi wenye vipaji na uwezo mkubwa wa kuandika na kuchambua habari na walipata mafanikio makubwa lakini wamesaliti fani na taaluma zao!

Ansbert Ngurumo said...

Maoni ya JINGO hapo juu yamenigusa kweli! Naijua Habari Corporation kwa sababu ndiyo imenilea kitaaluma. - Ngurumo

Anonymous said...

Watu wote tunajua wamenunua Habari Corporation ni watu wa maslahi kwa CCM na ndio sasa unafanyika mpango wa kurudisha fadhila toka huko. kama naye atafanya kazi ya kuisemea CCM tutaone maana haya yote ni matunda yao.. watu tunashangaa nini sasa wakati ndio mtandao halisi.
JoHN Said Dar

Anonymous said...

Huyu mtu alikuwa mwandishi mzuri wa kupamba sifa za kikwete kwenye kampeni na kufanya kuchambua wakti mwingine alikuwa mpiga debe mzuri wa JK sasa ndio matunda yake ya kufanya kazi na CCM hivyo afanye nini. Ndio maana tunaona kuwa watu na waandishi wa habari wa Tanzania wote wameolewa na serikali kwa sasa huu ndio wa magazeti kuandika kama vile hakuna makosa ni mchezo mchafu sana, Hivyo Siamini waandishi uchura wa watanzania. Kumbuka Makala zake wakati wa kampeni.tutaona mengi na yeye JK amefanya hivyo makusudi ili apate habari nzuri na kujibizana na watu wanaopenda kuonyesha njia mbadala kwa watu wote na kukosoa makosa yao
John Mpangule

Anonymous said...

Alaah, Kumbe huyu ndiye aliyemwumba JK kwa kupitia media. Akawadanganya wadanganyika kuwa JK ndiye atakayewaletea maendeleo kwa nukta moja tu kwa tabasamu lake la kimwinyi. Alaa kumbeee!!

Naona kampeni za uchaguzi wa 2010 zimeanza. Sasa hivi utakuwa ushindi wa asilimia 92 na si 82 kama 2005.

Yetu macho. Utandawazi unalipa. Tena sana. Jaribu usikie kama hujapata UDC kama Betti Mkwasa.

Anonymous said...

Maadam huyu kaanza basi spin doctors wote wa mtandao nao wako njiani kuambulia vyeo!! Ngojea baada ya uchaguzi wa ccm Taifa utasikia "KAMANDA" Manyerere nae kakumbukwa kawa DC na Bagenda kaukwaa ubalozi!! Hayo ndio ya Mussa ya firauni bado. Kwa mtindo huu maisha bora kwa wote ni ndoto za alinacha tu.

Anonymous said...

Siriha,

Manyerere ni mweupe mno kichwani hana kitu hapa, alitumika tu kama kondomu na amepewa ajira Mtanzania, basi. Kama walishindwa kumpa Muhingo watampaje Manyerere? Kama ni kupta angepata mwanzoni, lakini sasa JK ameanza kuwatambua watu na uwezo wao, wakti huo huo serikali yake inashindwa kutekeleza kila inachoanzisha, halafu achukue mtu mtupu kama Manyerere ampe uongozi! Manyerere uwezo wake utaishia katika kupewa elfu 20.

Salva ni kichwa, licha ya uzandiki aliofanya. Hata Bagenda anaweza kupata maana ndio hao hao waliojidhalilisha kwa sababu ya urafiki na njaa. Tungoje tuone JK anavyoendelea kuchemsha.

Anonymous said...

Tutaona Mamruki Kibao wakati huu na ndio tunashuhudia kuwa Waandishi wa Tanzania kuwa Wasemaji wa Serikali na Huku kuna Idara zinahusika na hivyo. Wanajifanya hao ni wanasiasa wa Kizazi hiki. huu ni Undumilakuwili.
JohN

Anonymous said...

Dawa pekee ni kugeukia blogu. Citizen Journalism. Tuachane na magazeti ya enzi ambayo hata ufikishaji wake wa habari una mizengwe kibao. Huwezi chapisha makala bila watu kuichunguza kama itawajengea sifa kwa viongozi wao au la, yaani ili wajikombe.

Jamani, tuingie kwenye zama za blogu kwa nguvu.

Blogu ndiyo teknolojia itakayoing'oa sisiemu hapo 2010. Ngojeni msikie.

Halafu mmesikia ya kandoro, eti anataka kutuchanja na kodi nyingine kwenye vimishahara vyetu duchu. Tunalipa kodi lukuki kwa huduma ambazo wala hatuzipati, sasa hivi wanataka kuongeza kutuchanja ili waje kwenye uchaguzi mkuu waseme, ooh tumejenga madarasa laki tano, dispensari milioni. TUSIKUBALI. Kodi tunalipa nyingi, huduma hatupati, kisha wanataka kuendelea. NO. Bw Kandoro, NO. NO. NO. NO. HATUTAKI, kwanza serikali yenu ituongeze mshahara mpaka walau 315,000/-, baada ya hapo tuzungumze.

Anonymous said...

Dawa ni kugoma kabisa, yaani kusema NO kwa vitendo.

Anonymous said...

Samson, hata kama Manyerere ni mweupe kisi cha wakin Betty Mkwasa na Sara Dumba Kumpiku!!! Aliambulia Safari ya Cuba na U.s.A. Mtawala wetu alipokwenda baada ya ushindi wa Kishindo

Anonymous said...

Siriha,

Manyerere hana exposure kama Sara Dumba wala Betty. Hiyo safari yenyewe aliishia Cuba, hakwenda Marekani, lakini baso haitoshi kumfanya astahili fursa ya kukabidhiwa hatima ya watu 500 au 700 wa wilaya, ingawa kwa serikali ya Kikwete hilo linawezekana maana ni usanii na urafiki tu unazingatiwa. Labda ndiyo sababu mambo yote yanakwama.

Anonymous said...

yah,msimsahau ba kijana mwingine Deo Balile aliyepo masomoni uk naye ni vibara waliotumika kama spin dr as anon said above.

Anonymous said...

EDITED VERSION:
yah,msimsahau na kijana mwingine Deo Balile aliyepo masomoni uk nae ni miongoni mwa waandishi vibaraka waliotumika kama(spin dr as anon said above)na wanamtandao.

Anonymous said...

Salva Rweyemamu hana tofauti na malaya au changudoa yeyote. Ni mtu mbinafsi mnafiki muongo na mpuuzi na swahiba yake Dr. Gideon Shoo.
Hawa sawa na Kikwete ni watu wa hovyo wanaotembeza chupi zao kila kona.
Namjua akiwa Habari Corporation alivyokuwa kichaa cha kukwepea madhambi ya serikali yalipoanikwa na waandishi wake.
Kwanza ni muathirika wa ukimwi wa muda mrefu anayeishi katika leo kesho itajijua.
Salva ni alama ya unafiki na ujambazi wa serikali ya Lowassa anayoiendesha nyuma ya pazia.

Anonymous said...

ndio ivyo jamani mi sina mengi wenzangu mmeongea yote,km bosi wa salva bwana rostam ni mwana mtandao sasa tunategemea nin kutoka kwa huyu salva,na km mlivyosema hii ndio zawadi yake baada ya kuchafua wengine,ila mi nafurahi kikwete kuweka marafiki sababu ndio hao watakaochangia mambo yake yaharibike na kung'oka hapo alipo,mwenzake lowassa kishaanza bado yeye.

My photo
Nimechongwa na mambo haya: Falsafa, Fasihi, Muziki, Habari na Harakati. Sifuati mkumbo. Napenda kuhoji na kudadisi - hulka ya kifalsafa ya kuusaka ukweli - 'UKWELI ULIO UCHI.'